• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA AWEKA JIWE LA MSINGI ZAHANATI YA MAPARAWE

Posted on: October 9th, 2024

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Dkt.Stergomena L.Tax katika muendelezo wa ziara yake ya siku tano  katika Mkoa wa Mtwara ya kutembelea, kukagua, kuzindua na kuweka mawe ya msingi katika miradi mbalimbali ya Maendeleo pamoja na kuzungumza na wananchi kupitia mikutano mbalimbali ya hadhara leo tarehe 09/10/2024  ameweka jiwe la msingi katika jengo la Wagonjwa wa nje OPD katika Zahanati ya  Maparawe, Kata ya Mchauru Halmashauri ya Wilaya Masasi.

Akizungumza na Wananchi ambao wamejitokeza kushuhudia tukio hilo, Waziri Tax amewashukuru na kuwapongeza wakazi wa Maparawe kwa kushiriki kikamilifu katika hatua zote za utekelezaji wa mradi huo wa zahanati ambao unakwenda sasa  kuwanufaisha  wakazi zaidi ya elfu nne (4000)

ambao kabla ya mradi huo wakazi wa Kijiji hicho walikuwa wakitembea umbali mrefu takribani kilomita 10 hivi kufuata huduma hiyo katika vijiji jirani.

Amesema "nipo hapa kumwakilisha mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kujionea jinsi mnavyoendelea pia kuona kero za Wananchi zinatatuliwa na mahitaji yote ya kuwaletea maendeleo Wananchi yanafanyika, basi mimi binafsi nimefarijika kuona mlivyotoa michango yenu, hivyo nawashukuru sana na kuwapongeza kwa kazi kubwa mnayoifanya si katika zahanati hii tu bali katika miradi mbalimbali ya maendeleo, nimetembea kote nilikozindua miradi lakini huu ndio mradi wa mfano kwasababu mmeweka nguvu kubwa sana, hongereni sana na hivi ndivyo inavyotakiwa twende na katika miradi mingine"...alisema Waziri Tax

Aidha, Mheshimiwa Tax ameongeza kuwa  "mmeweka nguvu ya takribani milioni 11 na Serikali baada ya kuona dhamira yenu ya dhati mheshimiwa Rais akaelekeza kiasi cha shilingi Milioni 50 zifike hapa, kwaiyo hapa mmechangia takribani asilimia 15 hadi 20, kwaiyo niwapongeze sana".

Hata hivyo pamoja na pongezi hizo, mheshimiwa Waziri ametumia fursa hiyo kuwaomba Wananchi wa Maparawe kuitumia vizuri zahanati hiyo (waitunze) huku naye akihaidi kuwachangia shilingi Milioni 2 ili waendelee na ujenzi wa eneo la kukaa Wagonjwa wanaposubiria kupatiwa huduma.

Ifahamike kuwa kabla ya mradi huo wa zahanati wakazi wa kijiji hicho walikuwa wakitembea umbali mrefu wa takribani kilometa 10 kwenda vijiji jirani kufata huduma hiyo ya Afya, Bi.Suzan Khatib  ni miongoni mwa wakazi wa maparawe ameishukuru serikali kwa kuwajengea Zahanati hiyo ambayo itakuwa msaada mkubwa kwa jamii nzima hususani wanawake kwani kabla ya kukamilika kwa zahanati hiyo walilazimika kufuata huduma za afya kwenye vijiji vya jirani.

Aidha zahanati hiyo  inatoa huduma mbalimbali ikiwemo huduma za Wagonjwa wa nje, Vipimo vya maabara, huduma ya kujifungua, huduma za Watoto, upasuaji mdogo,huduma za sindano na huduma za uzazi wa mpango.

Katika hatua nyingine waziri huyo, amezulu kaburi la aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa katika kata  ya Lupaso Halmashauri ya Wilaya Masasi.


09/10/2024

@.. Masasi DC

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa