• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Maendeleo ya Jamii

UTANGULIZI

Idara ya Maendeleo ya Jamii ni miongoni mwa Idara 13 na vitengo 6 katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.

DIRA YA IDARA: (VISION)

Kuhakikisha jamii inaondokana na janga la umaskini na kujenga jamii yenye fikra ya kujitegemea kiuchumi na kijamii kwa kujishughulisha na shughuli za kiujasiriamali ili kujiongezea kipato

MWELEKEO WA IDARA: (MISSION)

Kuwa miongoni mwa idara inayotoa huduma kwa ubora na ufanisi kwa kujiunganisha, kuisimamia na kuiwezesha jamii ili iweze kufanya shughuli zamaendeleo ili kuondokana na umaskini.

VITENGO NA MAJUKUMU YAKE: 

Idara ya Maendeleo ya Jamii ina vitengo vikuu sita (6)

a) Kitengo cha mfuko wa maendeleo ya wanawake (WDF)

b) Kitengo cha kupambana na kudhibiti Ukimwi.

c) Kitengo cha kuratibu Asasi za kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s)

d) Kitengo cha mfuko wa maendeleo ya vijana (YDF)

e) Kitengo cha Ustawi wa Jamii.

f) Kitengo cha mipango, ufuatiliaji na utafiti.

MAJUKUMU YA VITENGO VYA IDARA YA MAENDELEO YA JAMII

a) Kitengo cha uratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake (WDF) na

b) Kitengo cha Uratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya Vijana (YDF)

Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake na Vijana ni mfuko ya masharti nafuu iliyoanzishwa na serikali kuongeza mitaji kwa Wanawake na Vijana wajasiliamali. Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake (WDF), na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana (YDF) uliyoanzishwa na serikali kwa azimio la Bunge kwa Mujibu wa “exchequer and Audit Ordinance” ya mwaka 1961.

LENGO LA VITENGO VYA WANAWAKE (WDF) NAVIJANA (YDF)

· Kuwezesha kundi la Wanawake na Vijana kupataajira hatimaye kujitegemea kiuchumi na kijamii kupitia mikopo ya masharti nafuu, ambayo huwawezesha kukuza mitaji kupitia kufanya kazi hai za uzalishaji mali, ambapo huondoa utegemezi, wakati huohuo huchangia kukuza uchumi na kuondoa umasikini mahalia, familia na Taifa.

WALENGWA WA MFUKO WA MAENDELEO YA WANAWAKE (WDF) WALENGWA WA MFUKO WA MAENDELEO YA VIJANA (YDF).

· Wanawake na Vijana wote wenye uwezo wa kufanya kazi na ambao tayari wanaonyesha jitihada, nia ya kuchangia na pia uzalendo wa kurejesha kwa kadri ya makubaliano, aidha lazima wawe katika kukundi rasmi chenye lengo kinalolingana, vina kazi zenye tija na zenye matokeo, Katiba (Makubalinao kukifanya kuwa endelevu), kuwa na kinachotambulika toka ngazi ya Kitongoji Kijiji, Kata na Wilaya (Kimesajiliwa), kuwa na michanganuo.

BAADHI YA SIFA ZA MIRADI INAYOOMBEWA

  • Uthubutu wa mjasiria mali
  • Bidhaa yenye Ubora
  • Bidhaa yenye soko inayouzika ndani na nje
  • Mradi wenye mchanganuo unaolipa gharama hatimaye kuleta faida
  • Mradi unaorudisha mkopo kwa wakati
  • Mradi unaofurahisha mteja unajitangaza wenyewe ndani na nje
  • Mradi unafanya watu wengine wajifunze toka mradi
  • Kuelewa nani washindani wako
  • Mradi wenye kuleta matokeo na kujenga maisha mazuri na ya kujivunia kwa wanakikundi
  • Mradi wenye kukuza mtaji kwa haraka, pia kuwezesha kuweka akiba
  • Fedha zanazokopewa katika mradi wa biashara lazma utekeleze mradi kulingana na mchanganuo bila kubadili
  • Usafi wa Usalama wa bidhaa inapowezekana kuwa viwango bora vya Kitaifa na Kimataifa
  • Kuwa na uhakika wa ukubalifu kwa kuwa na liseni kuharalisha biashara
  • Kujituma na uaminifua wa kila Mwanachama.

c) Kitengo cha Utafiti,Takwimu na Mipango.

Ni kitengo ambacho kinajishughulisha na shughuli mbalimbali;-

i) Kufanya utafiti wa shughuli mbalimbali za maendeleo ya Jamii na kujenga uelewa kwa jamii kuhusu Fursa na Vikwazo vya Maendeleo (O&OD)

ii) Kukusanya na kutunza taarifa na takwimu mbalimbali za Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa ajili ya matumizi ya idara.

iii) Kuandaa na kupendekeza mipango na mikakati ya kubadili fikra za watu ili waweze kuwa ana mawazo ya maendeleo sawia na sera za serikali.

iv) Kupanga mipango mbalimbali ya idara kwa ajili ya Maendeleo ya Jamii.

d) Kitengo cha kupambana na kudhibiti Ukimwi

i. Kuhamasisha jamii juu ya kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) na UKIMWI.

ii. Kuhamasisha jamii kuondokana na unyanyapaa.

iii. Kutoa usaidizi katika makundi tete.

e) Kitengo cha Uratibu wa Asasi.

i. Kutoa ushauri kwa NGO’s, CBO’s juu ya uundaji wa katiba uanzishwaji wa vikundi pamoja na ubunifu wa miradi.

ii. Kusimamia na kuratibu Asasi za kiraia na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s) ili ziweze kufanya kazi zake kwa ufanisi.

iii. Kutoa elimu juu ya kuandaa maadhiko ya miradi (Project Proposal) kwa vikundi na mshirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s).

f) Kitengo cha Watoto

i. Uratibu wa mabaraza ya watoto.

ii. Utambuzi wa watoto waishio katika mazingira hatarishi.

MAJUKUMU YA JUMLA YA IDARA YA MAENDELEO YA JAMII

g) Kupitia mbinu shirikishi kuiwezesha jamii kuanzisha miradi ya kijamii kama vile usafi wa mazingira, ujenzi wa nyumba bora, shule, zahanati na majosho.

h) Kuelimisha viongozi wa serikali ya vijiji, dini na mashirika yasiyo ya kiserikali kuhusu sera mbalimbali za wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto kuhusu sera mbalimbali za wizara.

i) Kuwawezesha wananchi kupambana na mila zenye madhara kwa afya za wananchi hasa kwa wanawake na watoto wa kike, kuenea kwa virusi vya Ukimwi na magonjwa ya mlipuko.

j) Kutoa huduma kwa jamii kwa vipengele vya Ustawi wa Jamii na msaada wa kisaiklojia

k) Kutoa elimu juu ya kupambana na Virusi vya Ukimwi (VVU) na ugonjwa wa Ukimwi pamoja na kutoa msaada kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi (inategemea na bajeti)

l) Kuwezesha na kuimarisha shughuli za mfuko wa wanawake na vijana kwa kuvipatia mkopo wa masharti nafuu kwa vikundi vya kiuchumi.

m) Kuratibu maadhimisho ya sherehe mbalimbali za kitaifa.

HUDUMA ZINAZOTELEWA NA IDARA KWA SASA.

Huduma zinazotolewa na Idara ya Maendeleo ya Jamii mara kwa mara ni:

a) Kutoa ushauri kwa NGO’s, CBO’s juu ya uundaji wa katiba na uanzishaji wa vikundi pamoja na ubunifu wa miradi

b) Kuratibu mfuko wa Maendeleo ya Wanawake na Vijana au kuviwezesha vikundi vya wanawake na vijana mikopo ya masharti nafuu.

c) Kuratibu maadhimisho ya sherehe mbalimbali za Kitaifa

d) Kutoa huduma kwa jamii kwa vipengele vya ustawi wa jamii, ushauri na msaada wa kisaikolojia.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA NeST NA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI

    March 12, 2025
  • KAMATI YA SIASA YA CCM WILAYA YA MASASI YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    March 06, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI YANATOA FURSA KILA MMOJA KUJUA HAKI YAKE YA MSINGI: MHE MAJALIWA

    March 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa