• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Elimu Sekondari

  • UTANGULIZI

Idara ya Elimu ya Sekondari ni moja ya idara za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Idara hii ilianzishwa mwaka 2009 baada ya  Serikali kugatua usimamizi na uendeshaji wa shule za sekondari kutoka kwenye Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwenda  na kusimamiwa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa (Halmashauri za Wilaya/Miji/Manispaa/Majiji).

Halmashauri ya Wilaya ya Masasi ina Jumla ya shule za sekondari 27, kati ya hizo shule 26 ni za Serikali na shule 1 ni ya mtu  binafsi. Kati  ya  shule za Serikali 26, shule 23 ni shule za kutwa na shule 3 ni shule za bweni ikiwa mojawapo ni shule ya kidato cha tano na sita. Jumla ya wanafunzi wa shule za  sekondari za Serikali ni 7293 wakiwemo wavulana 3965 na wasichana 3,328 na shule ya binafsi ina jumla ya wanafunzi wavulana 501. Halmashauri ina jumla ya wanafunzi kwa shule zote za Serikali na binafsi 7794 wakiwemo wavulana 4466 na wasichana 3328.

2.     DIRA NA MWELEKEO

2.1    DIRA, DHIMA NA MALENGO YA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA 2014

Msingi wa elimu na mafunzo utajikita katika kumjengea Mtanzania misingi bora ya malezi, maadili, ujuzi,umahiri na kumwezesha kujitegemea. Elimu ya kujitegemea itaendelea kuongoza utoaji wa elimu na mafunzo kwa kuzingatia mabadiliko yanayotokea katika jamii, kisiasa, kiuchumi, kisayansi na kiteknolojia.

2.1.1 DIRA

Kuwa na Mtanzania aliyeelimika na mwenye maarifa, stadi, umahiri, uwezo na mitazamo chanya ili kuweza kuchangia katika kuleta maendeleo ya Taifa.

2.1.2 DHIMA

Kuinua ubora wa elimu na mafunzo na kuweka mifumo na taratibu zitakazowezesha kupata idadi kubwa ya Watanzania walioelimika na wanaopenda kujielimisha zaidi ili waweze kuchangia katika kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa letu.

2.2    LENGO LA JUMLA LA SERA YA ELIMU NA MAFUNZO

Kuwa na Watanzania walioelimika na wenye maarifa na ujuzi kuweza kuchangia kwa haraka katika maendeleo ya Taifa na kuhimili ushindani.

3.     ELIMU YA SEKONDARI

3.1    MATAMKO YA SERA KUHUSU ELIMU YA SEKONDARI

3.1.1 SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 1995 

Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 1995 ilifafanua kuwe Elimu ya Sekondari ina maana ya  Programu (Mpango)  kamili wa elimu inayotolewa kulingana na Mitaala ya Serikali na kupatikana kwa wanafunzi ambao watakuwa wamemaliza elimu ya msingi.

Nchini Tanzania elimu rasmi ya shule za Sekondari ina ngazi mbili. Ngazi ya kwanza ni elimu ya sekondari ya Ngazi ya Kawaida  ya miaka  minne, ambapo ngazi ya pili ni Programu ya Miaka miwili ya elimu ya Sekondari ya ngazi ya Juu. Ngazi ya kawaida huanzia kidato cha I na kuishia kidato cha 4, wakati Ngazi ya Juu ina kidato cha 5 mpaka cha 6

3.1.2         SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014

Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 imerekebisha muda wa elimu na mafunzo katika ngazi mbalimbali ili kuleta tija, ufanisi na matumizi bora ya rasilimali

                TAMKO

3.1.2.1      Serikali itaweka utaratibu wa elimu ya awali kuwa ya lazima na kutolewa kwa watoto wenye umri kati ya miaka mitatu hadi mitano kwa kipindi kisichopungua mwaka mmoja.

3.1.2.2      Serikali itaweka utaratibu wa elimumsingi kuwa ya lazima kuanzia darasa la kwanza hadi kidato ha nne; na kutolewa kwa miaka kumi na umri wa kwanza darasa la kwanza kuwa kati ya miaka minne hadi sita kulingana na maendeleo na uwezo wa mtoto kumudu masomo katika ngazi husika.

3.1.2.3      Serikali itaweka utaratibu wa kuhakikisha muda wa kukamilisha elimu na mafunzo katika ngazi mbalimbali za elimu baada ya elimumsingi unalenga mwanafunzi kupata ujuzi stahiki kulingana na Mfumo wa Tuzo wa Taifa.

3.1.2.4      Serikali itahakikisha kuwa elimumsingi katika mfumo wa umma inatolewa bila ada. 

4.     LENGO LA IDARA

Kutoa nafasi ya upataji maarifa, ujuzi na kuelewa ili wanafunzi wajiunge na taasisi za ufundi na mafunzo ya kitaalamu ya elimu ya juu.

5.     VITENGO VILIVYOPO KATIKA IDARA

Idara ya elimu ya sekondari ina jumla ya vitengo viwili (3) ambavyo hufanya shughuli zake kwa ushirikiano na kumsaidia mkuu wa idara ambaye ni msimamizi mkuu wa shughuli za idara katika kuleta matokeo tarajiwa.  Vitengo vya idara ni pamoja na kitengo cha Taaluma kinachosimamiwa na Afisa Elimu Taaluma Wilaya,  kitengo cha Vifaa na Takwimu kinachosimamiwa na Afisa Elimu Vifaa na Takwimu Wilaya na kitengo cha ufundi kinachosimamiwa  na Afisa Ufundi wa Wilaya na   vyote vikiwa chini ya mkuu wa idara ambaye ni Afisa Elimu Sekondari wa Wilaya.

5.1   MAJUKUMU YA VITENGO

5.1.1        MAJUKUMU YA AFISA ELIMU TAALUMA (W)

Kusimamia masuala yahusuyo maendeleo ya taaluma na michezo katika shule za sekondari wilayani.

5.1.2        MAJUKUMU YA AFISA ELIMU VIFAA NA TAKWIMU (W)

Kukusanya kuchambua na kuunganisha  takwimu mbalimbali zinazohusu elimu ya sekondari.

5.1.3        MAJUKUMU YA AFISA ELIMU UFUNDI

Kusimamia upanuzi wa elimu ya sekondari kusimamia ujenzi wa  majengo mapya katika shule za zamani au katika kuanzisha Shule mpya.

kwa maelezo zaidi bofya hapa

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA NeST NA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI

    March 12, 2025
  • KAMATI YA SIASA YA CCM WILAYA YA MASASI YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    March 06, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI YANATOA FURSA KILA MMOJA KUJUA HAKI YAKE YA MSINGI: MHE MAJALIWA

    March 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa