• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAZIRI TAX AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI KUTENGA FEDHA ZA MAPATO YA NDANI KUJENGA KITUO CHA MIONZI

Posted on: November 13th, 2024

Waziri wa Ulinzi na jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mhe.Stergomena Lawrence Tax Leo Tarehe 13/11/2024 akihitimisha ziara yake Mkoani Mtwara ameweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa kituo Cha Mionzi (x-ray) kilichopo katika Kata ya Chiwale Halmashauri ya Wilaya Masasi Mkoani Mtwara.


Ziara hii ni muendelezo wa ziara ambazo alianza kuzifanya Tarehe 6/10/2024 Mkoani Mtwara, Lakini alilazimika kukatisha ziara baada ya kuwa amepewa majukumu mengine ya Kitaifa hivyo alilazimika kuondoka na kuhaidi atarudi tena.

Akizungumza mara baada ya kuweka jiwe hilo la msingi katika Jengo la  Mionzi kwenye kituo Cha Afya Chiwale mhe.Tax amesema kwamba madhumuni ya ziara hiyo ni maagizo ya mhe.Rais Dokta Samia Suluhu Hassan ya kuwataka watembelee na kuangalia miradi iliyotekelezwa inaendeleaje na hatua gani imefikia, na Kama Kuna changamoto imesalia basi ziweze kutafutiwa ufumbuzi.


Amesema, mhe.Rais ana nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba anawaletea Wananchi wake Maendeleo na anatatua changamoto zao, ha hii ameona katika miradi mbalimbali kwamba kuna fedha nyingi zimeletwa kwa kipindi cha uongozi wake tangu aingie madarakani.

"Mkoa wa Mtwara umekwisha pokea kiasi cha shilingi bilioni 740, Lakini kwa Masasi pekee imepokea  kiasi cha shilingi bilioni 18.6 na hizo ndizo zimewezesha kutekeleza miradi mbalimbali ambayo nimeisikia katika sekta ya Afya, Elimu, Maji,barabara, umeme japo bado kuna changamoto Lakini si fedha hizi tu ambazo katika Jimbo hili la Ndanda, Wilaya hii imeendelea kunufaika na miradi mbalimbali kupitia katika fedha zinazopitia sekta nyinginezo".


Aidha, akizungumzia Jengo hilo la Mionzi mhe.Stergomena Tax ameendelea kuelezea kuwa kilichomleta hapo ni kuweka jiwe la msingi kituo Cha Mionzi" hii ni hatua kubwa sana kwasababu huduma zitakazotolewa katika kituo hiki ni za kisasa mno, ni huduma ambazo zinapatikana katika hospitali kubwa kubwa hivyo nimemuelewa vizuri mhe.mbunge Cecil Mwambe kwamba kituo hiki kwa ujumla wake ni kikubwa na kinaweza kupandishwa hadhi ya kuwa hospitali japo kuna baadhi ya changamoto ikwemo ukosefu wa wodi ya akina baba,hivyo nimelipokea na mimi nitayafikiaha kwa viongozi wangu wa juu".....alisema Waziri Tax


Hata hivyo mhe.Tax amehitimisha hotuba yake kwa kuipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Masasi kutenga fedha za mapato ya ndani na kuwezesha ujenzi huo wa kituo Cha Mionzi na hivyo amesisitiza kukamilisha haraka ujenzi huo ili wananchi wanufaike na mradi huo.


Hata hivyo ifahamike kuwa mradi unalenga Kutoa huduma ya Mionzi inayojumuisha huduma ya x-ray, ultrasound, mammography na kipimo Cha Moyo (ECG) hii inatokana na ongezeko la Wagonjwa wanaopata ajali, shida ya utumbo na uvimbe mbalimbali wa Ndani ya tumbo.


Aidha mradi huu utakapokamilika utahudumia Wananchi wapatao 50,163 wa Kata ya Chiwale na Kata jirani.


Mradi huu mpaka kukamilika kwake utagharimu kiasi cha shilingi 150,000,000.00 na Sasa tayari shilingi 130,000,000.00 zimetolewa Kutoka fedha za mapato ya ndani kwa awamu 3.

Pia mradi huu ambao kwasasa upo katika hatua ya umaliziaji unatekelezwa kwa mfumo wa force akaunti na ujenzi wake awamu ya Kwanza ulianza tarehe 19/04/2024 na kuisha tarehe 19/07/2024, awamu ya pili umeanza tarehe 13/09/2024 na unatarajia kukamilika Tarehe 13/12/2024


13/11/2024

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa