• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WADAU WA ELIMU HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI WATAKIWA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA SHULE

Posted on: July 14th, 2018

Katika kuboresha utoaji wa elimu bora katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi wadau wote wa elimu ikiwemo Wazazi, Viongozi wa ngazi zote, Jamii  na mashirika kwa ujumla lazima kushirikiana kwa pamoja katika kuhakikisha mazingira ya kujifunza na kujifunzia yanakuwa bora ikiwemo kujenga miundombinu na utoaji wa chakula shuleni hasa kwa shule za kutwa ili kuwawezesha wanafunzi kusoma vizuri.

Mkuu wa Wilaya wa Masasi Mhe Selemani Mzee (aliyesimama) akiongea na wadau wa elimu baada ya kupokea ripoti ya ufuatiliaji wa rasilimali fedha za umma kwa shule 20 za Masasi iliyowasilishwa na shirika la Haki Elimu kupitia mtandao wa Marafiki  Elimu wa masasi (MEMA)  katika ukumbi wa halmashauri 

Hayo yamebainishwa leo na Mkuu wa Wilaya ya Masasi mhe. Selemani Mzee baada ya kupokea taarifa ya ufuatiliaji wa fedha za umma  kwa shule 20 za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi  iliyotolewa na shirika la Haki Elimu kupitia Mtandao wa Marafiki wa Elimu Masasi (MEMA) ambayo pamoja na mambo mengi imebainisha  kuwa moja ya changamoto inayozikumba shule za msingi na sekondari ni upungufu na uchakavu wa miundombinu ikiwemo madarasa na  ameeleza kuwa, ujenzi wa miundombinu ya shule unahusisha wadau wote wa elimu yaani serikali na jamii kwa ujumla

“Kila mmoja aone kuwa suala la  wanafunzi kusomea nje au kwenye miti halikubaliki, hivyo shule ambazo zinachangamoto ya wanafunzi kusomea nje zitatafutiwa ufumbuzi wa haraka wakati ujenzi wa madarasa unaendelea” alisema Mkuu wa Wilaya.

Wadau wakimsikiliza mgeni rasmi (hayupo pichani) baada ya kupokea ripoti

Kuhusu matumizi sahihi ya fedha za ruzuku ambazo zina kipengere cha ukarabati wa miundombinu  Selemani amewakumbusha walimu kufanya matumizi kwa kuzingatia miongozo ili fedha hizo ziweze kutekeleza shughuli zilizopo kwenye mpango ikiwemo kukarabati miundombinu  na shughuli zingine za elimu na si vinginevyo.

Pia Mkuu wa Wilaya amefafanua kuwa,  Wazazi wataendelea kushirikishwa kuchangia kwa hiari katika maeneo ambayo fedha ya ruzuku hazigusi ikiwemo utoaji wa chakula  cha mchana kwa wanafunzi wa shule za kutwa, mavazi, na mambo mengine ambayo wazazi kupitia kamati za shule itaona inafaa kwa malengo ya kuboresha elimu katika shule zao.  

Mdau wa elimu   akitoa mchango wake 

Akitoa maelezo ya awali katika kikao hicho Mratibu wa Programu ya Haki Elimu Joyce  Mkina alieleza kuwa ripoti hiyo inalenga kuwaeleza wadau wa elimu Masasi changamoto zilizopo kwenye shule ili kuona namna ya kuzitatua na hatimaye utoaji wa elimu kuwa bora jambo ambalo ndilo lengo kuu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi mhe. Juma Satmah amewaeleza wadau wa elimu wakiwemo Wazazi, Walimu, Wajumbe wa bodi na kamati za shule, Watendaji wa Kata na Vijiji kuwa kwa muda mrefu hali ya miundombinu ya shule imekuwa si mizuri kutokana na mfuko wa elimu kusitishwa  lakini kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri imeweza kukusanya na  kupeleka milioni 494 kwenye shule kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya shule kupitia mfuko wa elimu, hivyo baada ya muda tatizo la upungufu miundombinu na ile michakavu katika shule litakwisha kabisa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi  mhe. Juma Satmah akichangia jambo  kwenye kikao cha wadau wa elimu

Satmah amewashukuru shirika la twaweza kwa ripoti yao ya utafiti katika shule 20 kwani imetusaidia kuona mapungufu yaliyopo na kuweza kuyajadili kama wadau na hatimaye kuchukua hatua ya kutatua ikiwemo kusimamia matumizi ya fedha kwa kufuata miongozo, ubovu wa miundombinu na utoaji wa taarifa za fedha katika shule ambayo ni mambo ya kuyafanyia kazi na wadau wote ili kuwa na ustawi wa elimu.


Wadau wakimsikiliza mgeni rasmi (hayupo pichani) baada ya kupokea ripoti

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi  ndugu Jeremiah Lubeleje akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa kikao cha wadau wa elimu kilicholenga kupokea taarifa ya utafiti wa  ufuatiliaji wa Rasilimali fedha za umma kwa shule 20 uliofanywa na Shirika la Haki Elimu kupitia mtandao wa marafiki wa elimu Masasi (MEMA) tarehe 13.07.2018


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa