• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MITI 3800 YAPANDWA KATIKA KAMPENI YA UPANDAJI WA MITI MASASI DC

Posted on: February 17th, 2026

Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mhe.Rachel Kassanda leo tarehe 17 Februari 2026 amezindua rasmi zoezi la  upandaji wa miti kwa lengo la kuendelea kuhifadhi Mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Amewataka pia Wananchi kupanda miti kwa wingi, kuitunza na kuacha tabia ya kukata miti hovyo ili kulinda vyanzo vya maji, na kuboresha hali ya hewa kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika Shule mpya  ya Sekondari ya Mlingula na Chikunja zilizopo  katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, mhe.Kassanda amesema kuwa Wilaya imejiwekea mkakati wa upandaji wa miche ya miti kila mwaka na kupitia Halmashauri iwe imepanda miti milioni 1.5 ili kurejesha hali ya miti iliyopotea ambayo imesababishwa na baadhi ya Wananchi kuwa na tabia ya kukata miti hovyo kwa ajili ya matumizi ya kuchoma mkaa na kwa mahitaji ya kuni kwa biashara.

" Ili kuendelea kuunga mkono ajenda ya kitaifa ya utunzaji wa Mazingira, sisi wana Masasi  lazima

 tuwe sehemu ya kutengeneza Masasi ya kijani na hili linawezekana kama tutashiririkiana katika zoezi la upandaji miti katika maeneo mbalimbali , Wananchi muwe na desturi ya kupanda miti kwani ni alama kubwa"

Amesema zoezi hilo litakuwa ni endelevu ili kuunga mkono kwa vitendo jitihada za kutunza na kuhifadhi Mazingira hivyo amewasisitiza Wakala wa Misitu Tanzania ( TFS) Wilayani Masasi kuendelea kutoa elimu kwa jamii umuhimu wa upandaji wa miti isiyopungua mitano kwa kila kaya  sanjari na kusambaza miche ya miti hiyo katika maeneo mbalimbali ikiwemo mashuleni na kuhakikisha wanaisimamia miti  inapandwa na hasa  katika msimu huu wa  mvua za masika.

Aidha Mhe. Kassanda amehitimisha mazungumzo yake kwa kutoa rai kwa Wanafunzi kuhakikisha kila mmoja atambue analojukumu la kupanda miti na kuisimamia kikamilifu, ili iweze kuwaletea tija katika maisha yao na hususani wanapokuwa katika mazingira ya shule wanaweza kupata vivuli, matunda ( lishe) n.k

Jumla ya miche 3800 imepandwa ikiwemo miche ya Mipapai, Mipera na Mikongo, ambapo katika shule ya Sekondari Mlingula imepanda miti 1800 na Chikunja ikipanda miti 2000.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MITI 3800 YAPANDWA KATIKA KAMPENI YA UPANDAJI WA MITI MASASI DC

    February 17, 2026
  • MASASI DC YAFANYA MKUTANO WA ROBO YA PILI WA BARAZA LA MADIWANI

    February 05, 2026
  • MKUU WA WILAYA YA MASASI AFUNGUA MAFUNZO KWA WAHESHIMIWA MADIWANI HUKU AKISISITIZA UWAJIBIKAJI WA PAMOJA.

    January 30, 2026
  • NDWIKA: MRADI HUU WA MABWENI MAWILI TUMEPATA FAIDA YA KUPUNGUZA MLUNDIKANO WA WANAFUNZI MABWENINI.

    January 16, 2026
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa