• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UMEME WA REA KUUNGANISHWA NYUMBA KWA NYUMBA, MASASI

Posted on: September 28th, 2018

Mhe. WAZIRI wa Nishati, Dk. Medard Kalemani ameeleza kuwa,  serikali kupitia mradi wa REA III unaotekelezwa nchini imedhamilia kuweka umeme nyumba kwa nyumba kuanzia nyumba ya nyasi hadi ya ghorofa kwa gharama ya shilingi 27,000 tu.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mpeta wilayani masasi wakati wa ziara yake mkoa wa Mtwara, alisema kuwa Serikali pamoja na watalaamu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa kushirikiana na REA wamekuwa wakifanyakazi usiku na mchana ili kuhakikisha kazi ya uunganishaji umeme inafanyika kwa haraka ili  wananchi wapate umeme na pia kuchochea uanzishwaji wa viwanda

Mhe. Kalemage amewahakikishia wananchi kuwa “wewe mwananchi sema unataka uunganishiwe umeme wapi iwe kwenye nyumba ya majani, tembe, makuti au ghorofa zote zitawekewa umeme, haturuki nyumba na nitasimamia” 

Mwananchi atalipia shilingi 27,000 kwa ajili ya kuunganishiwa umeme ila gharama za kuweka miundombinu ya ndani (wiring) itakuwa nje ya fedha hiyo, ili kupunguza gharama mwananchi anaweza kununua kifaa ambacho hakihitaji kuweka miundombinu ya ndani.

 Ili kuwezesha zoezi la uunganishaji wa umeme kwa haraka Mhe. waziri amewaagiza kuweka ofisi  ngazi ya kata ili kuwarahisishia wananchi kulipia gharama za kuunganishiwa umeme kwenye kata badala ya kwenda Ofisi za makao makuu hali ambayo inaongeza gharama kwa wananchi.

 Aidha, Dk. Kalamage amewaeleza wananchi kuwa wanaweza kulipia kidogo kidogo gharama za kuunganishiwa umeme  na pindi wanapofikisha Shilingi 27,000 wataunganishiwa huduma hiyo, lengo la serikali ni kuhakikisha kila mwananchi anapata umeme ndani ya kipindi cha mradi.

Wakiongea mbele ya Mhe. Waziri, wananchi wa mpeta wameishukuru serikali kwa kupeleka huduma ya umeme vijijini maana ni huduma muhimu kwani itasaidia kuanzisha shughuli mbaimbali za kiuchumi na hivyo kuboresha maisha yao.

Aidha Dkt. Kalemani amewataka watanzania kuchangumkia fursa ya kuunganishiwa umeme kwa kutumia kifaa kinachojulikana kama Umeme Tayari (UMETA) kwani mtumiaji hatatakiwa kuweka miundombinu ya umeme yaani wiring na hivyo kupunguza gharama za kuunganishiwa umeme kwa matumizi ya nyumbani sio viwandani.

Mhe. Waziri ameshauri kuwa kutokana na urahisi wa kifaa hichi nashauri kitumike kwenye majengo ya taasisi za Umma ikiwemo  ofisi za vijiji kata, vituo vya afya , zahanati, vituo vya polisi, na maeneo mengine ambayo hayana ulazima wa  kuweka miundombinu ya umeme yaani wiring.”  Kwani garama yake ni shilingi 36,000 tu.


Mradi wa REA III kwa mkoa wa Mtwara ulizinduliwa Agositi mwaka 2017  ambao kwa  Wilaya ya Masasi vijiji 52 vitaunganishwa

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa