• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MWENGE WA UHURU WAZINDUA NA KUTEMBELEA MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI MILLIONI 482,100,000/= HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI

Posted on: April 9th, 2022

KIONGOZI wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2022 Ndugu Sahil Nyanzabara Geraruma amekagua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Halmashauri ambapo Mwenge wa mwaka huu 2022 umeambatana na kauli mbiu inayosema   “Sensa ni Msingi wa mipango ya maendeleo shiriki kuhesabiwa tuyafikie malengo ya Taifa”. Mwenge ukiwa katika Halmashauri ya Wilaya Masasi umekimbizwa umbali wa kilomita 118.5 kwa kupita katika vijiji 13, kata 10 na tarafa 3. Aidha Mwenge wa Uhuru Kitaifa umepita katika miradi minne (4) ambapo kati ya hiyo, mradi mmoja (1) utawekewa jiwe la msingi, mradi mmoja (1) utakaguliwa na kuonwa, na miradi miwili (2) itazinduliwa.  Gharama za miradi iliyopitiwa na mbio za Mwenge wa Uhuru ina thamani Tshs. 482,100,000/= Serikali Kuu  Tshs. 290,000,000 sawa na asilimia 69.59 Halmashaur Tshs.  5,000,000 sawa na asilimia 0.79 Wananchi  Tshs.187,100,000  sawa asilimia 29.61 

Miradi hiyo 4 iliyoandaliwa ambayo imepitiwa na Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya wilaya ya Masasi, imegawanyika kisekta kama ifuatavyo;Sekta ya Afya mradi1,Sekta ya Elimu mradi 1,Sekta Binafsi mradi1,Shughuli za vijana mradi 1 Aidha katika miradi hiyo 4, Msafara wa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2022 umefanya kazi kama ifuatavyo; Kuweka jiwe la msingi mradi   1 Kuzindua miradi  2 Kuona, kukagua na kupata taarifa mradi   1 Jumla miradi-4

JENGO LA WAGONJWA WA NJE (OPD)

JENGO LA MAABARA

Tarehe 21.10.2021 shule ya Sekondari Chiungutwa ilipokea jumla ya Tshs 40,000,000/= kutoka Serikali Kuu (Mradi Na 5441 TCRP) kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa ,Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa shule ya Sekondari Chiungutwa ulianza rasmi mwezi Oktoba Mwaka 2021, na kukamilika Mwezi Januari 2022. Aidha Majengo haya yamejengwa kwa kutumia utaratibu wa (Force account) ambao ni mafundi wa kawaida (local fundi) wametumika na vifaa kununuliwa moja kwa moja kutoka viwandani na maduka ya jumla. Gharama kuu za Mradi ni shilingi 40,000,000/= Mradi umekuwa shirikishi mbali na ushiriki wa Kamati zilizopo kwenye mwongozo, Pia Jamii imeshiriki katika kuchimba msingi ambayo thamani yake ni Tshs100,000 .Mradi umegharimu kiasi cha fedha za Kitanzania Shilingi 38,628,828.92 na pesa iliyobakia ni kiasi cha shilingi 1,376,171.08 .

Hii ni kilabu ya wanafunzi wapinga rushwa ambapo mkimbiza mwenge wa uhuru 2022 NduguSAHILI NYANZABARA GERARUMA   alipata pia fursa ya kuitembelea na kujua namna inavyojiendesha katika shule ya sekondari ya chiungutwa

Kikundi cha vijana cha Tuinuane kilianza rasmi tarehe 10/08/2019 kikiwa na wanachama watano (4 Ke na 1 Me). Shughuli kuu za kikundi zikiwa ni Utengenezaji wa batiki na kusuka makapu ,Kupitia mradi wa utengenezaji wa Batiki pamoja na Makapu kikundi kilifanikiwa kukusanya shilingi 1,100,000 kama faida ya mradi huo ndipo mnamo mwezi Novemba 2020 kikundi kilinunua Ng’ombe mmoja wa Maziwa aliyezaa aina ya Frisian hivyo kikundi kinaendelea kukamua maziwa na kuyauza kwa jamii kiasi cha Lita 10 kwa Siku.

Kituo cha mafuta Engen kipo katika kijiji cha Nagaga kata ya Namalenga Mradi huu umejengwa na kukamilika kwa gharama ya Tshs. 185,000,000/= na  umefuata sheria zote za usajili wa kituo na malipo yote ya Serikali yamefanyika kikamilifu na kupewa ruhusa ya kuendesha mradi huu katika kijiji cha Nagaga ,mafanikio yanayotokana na kufungua mradi huu katika kijiji cha Nagaga.Kupunguza tatizo la uhaba wa upatikanaji wa mafuta katika kijiji cha Nagaga na vijiji jirani,Kutoa ajira za muda mrefu na muda mfupi,Mradi huu umeongeza mapato kwa serikali kwa kulipa kodi mablimbali kulingana na uhitaji.








Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa