• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MSIMU WA KILIMO KWA MWAKA 2024/2025 MKOA WA MTWARA UMEZINDULIWA RASMI LEO TAREHE 30/12/2024 MPINDIMBI -MASASI

Posted on: December 30th, 2024

WANANCHI/ WAKULIMA WOTE MKOANI MTWARA TUMIENI VIZURI FEDHA MLIZOPATA KWENYE MAUZO YA KOROSHO KWA KUJIANDAA KUTOA HUDUMA KWA WATOTO WENU WATAKAOJIUNGA NA MASOMO KUANZIA JAN 13/2025: RC SAWALA

Wananchi/ Wakulima wote Mkoani Mtwara wametakiwa kutumia vizuri fedha ambazo wamezipata kwenye mavuno ya korosho huku  wakijiandaa na Kutoa huduma kwa Watoto wao watakaojiunga na masomo kuanzia shule za awali, Msingi, na Sekondari ifikapo jan 13/2025


Pia wamekumbushwa kuwa na nidhamu ya matumizi mazuri ya fedha hizo walizopata kwa kujiandaa na msimu unaofuata wa Kilimo ili kuongeza uzalishaji.

Hayo yamejiri Leo tarehe 30/12/2024 katika hafla ya uzinduzi wa msimu wa Kilimo kwa mwaka 2024/2025 Kwa Mkoa wa Mtwara, ambao uzinduzi huo umefanyika katika Kijiji Cha Mpindimbi Kata ya Mpindimbi Halmashauri ya Wilaya ya Masasi huku Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu mhe.Christopher Magala ndiye mgeni rasmi akimwakilisha mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Kenani Sawala.


Amesema hawatapendezwa kuona Wakulima/ Wananchi ambao wamepata fedha nyingi katika msimu unaoishia  kwenye mauzo ya korosho na akashindwa kumuhudumia mtoto wake kwenda shule .


"Kuna wakati mwingine mnajisahau sana, toeni kipaumbele kwenye mambo ya Elimu kwa Watoto wenu, Wakulima walio wengi kwasasa wamepata fedha nyingi Sana, tutashangaa kuona pia mtoto wa mkulima aliyepata fedha nyingi anatembea umbali mrefu Kwa miguu kama km.10- 25 kwenda shuleni kufuata Shule ilipo, sisi sote ni mashahidi shule zetu zimejengwa kwenye kila kata tena kuna baadhi ya kata ina shule zaidi ya moja na kata nyingine zina Shule moja na Watoto wengi hutembea umbali mrefu kwenda shuleni kutafuta Elimu, tumieni fedha hizi mlizopata kununua baiskeli ili Watoto waweze kuhudhuria masomo Yao" alisisitiza Mhe.Magala....


Ameongeza kuwa mafanikio hayo sasa Kwa Wakulima yametokana na Sera nzuri ya Serikali ya awamu ya sita chini ya Uongozi shupavu wa Dkt.Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuweka mazingira mazuri katika maeneo yanayoruhusu uwekezaji kwenye Kilimo na masoko ya mazao.

" Katika msimu 2023/2024 Serikali kupitia TARI NALIENDELE ilitoa mbegu za ufuta tani 10 ambazo zilisambazwa kwenye Halmashauri zote na Wakulima walipokea pembejeo za korosho, pembejeo za ruzuku, aina ya salfa ya unga tani 21,382 na viutilifu vya Maji.


Aidha ameendelea kuelezea kuwa mifumo ya masoko ya mazao imeboreshwa Kwa kutumia minada ya wazi kwa njia ya mtandao ambayo imesaidia kuimarisha bei za ushindani na ndio maana tumeshuhudia bei imekuwa nzuri .


"Vile vile bandari yetu ya Mtwara imeendelea kusafirisha korosho zinazozalishwa kwenye mkoa wetu wa Mtwara na mikoa ya jirani, (Lindi, Mtwara na Ruvuma) kwenda kwenye masoko ya nje na kuongeza ajira na mapato ndani ya Mkoa wetu wa Mtwara ".


"Ndugu Wananchi katika kuondoa changamoto ya upatikanaji wa mbolea za mazao mchanganyiko, Serikali ya awamu ya sita imeandaa mpango wa ruzuku kwa Wakulima kwa msimu wa mwaka 2023/2024 ambapo jumla ya Wakulima 11,605 wamenufaika kwa kununua jumla ya tani 4513 na mbolea yenye thamani ya sh.bilioni 7.9 ambapo Wakulima wao walichangia sh. Bilioni 5.9 ambapo pia kwa mwaka huu 2024/2025 Serikali inaendelea tena na mfumo huu ambapo pembejeo zitatolewa kama msimu uliopita, hivyo nichukue fursa hii kuhamasisha Wakulima wote kuendelea kujisajili Kwa maafisa Kilimo ili isaidie na hatmaye kuongeza uzalishaji wa mazao."

Mwisho mhe.Magala  akahitimisha  Kwa Kutoa rai kwa mawakala/ wazabuni ambao wamepewa kazi ya kusambaza na kuuza pembejeo za ruzuku kuhakikisha wanafika Kila eneo walilopangiwa kwasababu Kuna tabia imejengeka kwa baadhi ya mawakala kuchagua baadhi ya Maeneo, hivyo " nitoe tahadhari hakikisheni mnatoa huduma katika Kila wilaya uliyopangiwa .


Hata hivyo uzinduzi wa msimu wa Kilimo mwaka 2024/2025 Kwa Mkoa wa Mtwara umeenda sambamba na kuzindua mafunzo kwa njia ya mashamba darasa yakuhamasisha matumizi ya mbolea na mbegu Bora, Kuzindua zoezi la ugawaji na upandaji wa Miche ya minazi, Kuzindua zoezi la ugawaji na upandaji wa mikorosho mipya, Pamoja na kukabidhi zawadi Kwa Wakulima washindi.


30/12/2024

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa