• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI HALMASHAURI YA WILAYA MASASI ATOA MAELEKEZO KUHUSU UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA MWAKA 2024

Posted on: September 26th, 2024

Msimamizi wa uchaguzi Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Bi.Beatrice Mwinuka leo tarehe 26/09/2024 ametoa maelekezo muhimu kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao unatarajia kufanyika Nov 27,2024.

Aidha maelekezo hayo yamelenga Kutoa mwongozo ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa uwazi haki na usawa kwa kuzingatia sheria na taratibu za Uchaguzi zilizowekwa.

Akitoa maelekezo hayo kwenye kikao kifupi kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo uliopo mbuyuni Masasi ambacho kimewakutanisha kwa pamoja viongozi wa Vyama vya Siasa, viongozi wa dini, mamwenye, wazeee maarufu, wenyeviti kutoka vikundi vya Wanawake na Vijana, uongozi wa Kijiji na Kata ya Mbuyuni, wajumbe wa Kamati ya Uchaguzi, pamoja na Watumishi kutoka kada mbalimbali ngazi ya Halmashauri hiyo.

Amesema " leo Tanzania nzima tunatoa maelezo ya uchaguzi kwaiyo katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi tumewaalika kwa ajili ya kusaidia maelezo haya Lakini pia kwenda kuhamasisha jamii yetu tumefanya uhamasishaji mbalimbali kwa kutumia vyombo vya habari, mitandao ya kijamii, Lakini nasi tuliopo hapa twende tukaieleze Jamii inayotuzunguka "

Amesema kikubwa anachozungumza leo akiwa ndiye msimamizi wa uchaguzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi ni maelezo yakutoa ratiba nzima ya Zoezi litakalofanyika, maeneo ambayo watafanyia uchaguzi na nini ambacho kinatakiwa kufanyika kwenye zoezi hilo.


Bi.Mwinuka ameendelea kuelezea kuwa kwa mujibu wa Kanuni ya 9 kifungu (cha 1 -2) cha Kanuni ya uchaguzi wa mwenyekiti wa kijiji, kitongoji na Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji katika Mamlaka za Serikali za Mitaa Kwa mwaka 2024, msimamizi wa uchaguzi amepewa Mamlaka ya Kutoa maelekezo kuhusu uchaguzi, na maelekezo hayo yanatolewa siku 62 kabla ya uchaguzi kwa lengo la kuhakikisha kuwa taratibu zote zinafuatwa na kwamba wapiga kura pamoja na wagombea wanapata taarifa zote zinazohitajika kwa wakati.


"Maelekezo haya pia yanafafanua hatua zinazoongoza mchakato wa uchaguzi kuanzia uandikishaji wapiga kura, uchukuaji na urejeshwaji wa fomu kwa wagombea, uteuzi wa wagombea na tarehe siku ya Uchaguzi."


Amesema kwa mujibu wa tangazo la uchaguzi lililotolewa kwa kuzingatia Kanuni namba 4 ya Uchaguzi wa viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, tangazo linaeleza kwamba Uchaguzi huo utafanyika tarehe 27 Nov 2024, huku ikitanguliwa na zoezi la uandikishaji wapiga kura litakalofanyika tarehe 11-20 Oktoba 2024 katika vituo 886 vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.


Akielezea zoezi la kuchukua na kurudisha fomu kwa wagombea Mwinuka amesema fomu za kugombea zitatolewa kuanzia tarehe 1-7 Nov 2024 kwa msimamizi msaidizi wa uchaguzi, huku zoez la uteuzi wa wagombea kwa mujibu wa Kanuni namba 18 uteuzi utafanyika tarehe 08 Nov 2024, wakati pingamizi dhidi ya uteuzi kwa mujibu wa Kanuni namba 23 ni kuanzia tarehe 8-9 Nov 2024 huku uamuzi wa pingamizi utatolewa tarehe 8-10 Nov 2024 .


"Rufaa dhidi ya uamuzi kuhusu pingamizi ya uteuzi zitapokelewa kuanzia Nov 10-13, 2024, ikiwa kampeni za Uchaguzi kwa mujibu wa Kanuni namba 27 zitaanza tarehe 20-26 Nov 2024 .


Hata hivyo msimamizi huyo wa uchaguzi Halmashauri ya Wilaya Masasi amehitimisha maelekezo yake kwa Kutoa wito kwa wananchi wote wenye sifa kushiriki kikamilifu katika mchakato huo wa uchaguzi kuanzia hatua ya kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura ambayo ni hatua muhimu inayompa haki ya kushiriki katika uchaguzi kama mpiga kura au mgombea, hivyo Wananchi wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha ili kutimiza haki yao ya kupiga kura au kugombea uongozi.


Nafasi zinazogombewa kwenye uchaguzi huo ni nafasi ya Mwenyekiti wa Kijiji, nafasi ya Mwenyekiti wa kitongoji, Wajumbe wa Halmashauri kundi mchanganyiko na wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji kundi la Wanawake.

26/09/2024

@.. Masasi DC

Kazi iendeleeee!

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa