• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MIRADI YA AJIRA YA MUDA INAYOTEKELEZWA NA TASAF YATATUA CHANGAMOTO YA MAJI KIJIJI CHA MWENA

Posted on: March 28th, 2018

Kwa muda mrefu wananchi wa masasi wamekuwa na tatizo la uhaba wa upatikanaji wa  maji safi na salama hali inayosababisha wananchi hao kutumia muda mwingi kutafuta maji katika visima vya asili ambavyo sio  salama badala ya kufanya shughuli za maendeleo

Kutokana na tatizo hilo, Serikali imekuwa ikiweka jitihada za kuhakikisha inawahudumia  wananchi kwa kutatua kero zinazowakabili ikiwemo ya upatikanaji wa maji, ambapo imedhamiria kumtua mama ndoo kichwani kwa kuwaondolea wananchi tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao.

Tanzania kupitia  mpango wa kunusuru kaya masikini  awamu ya tatu katika Mradi wa ajira ya muda (PWP) imefanikiwa kutekeleza miradi mbalimbali inayoibuliwa na wananchi ikiwemo miradi ya maji katika vijiji mbalimbali vinavyonufaika na mradi lengo ikiwa ni kwaajili ya kuongeza kipato kwa walengwa kwa kulipwa ujira baada ya kufanya kazi katika kipindi cha hari na kupata fursa na ari ya kushiriki shughuli za maendeleo.

Halmashauri ya wilaya ya masasi ni kati ya Halmashauri zinazotekeleza mpango wa TASAF III ambapo jumla ya vijiji 97 vinanufaika na mradi kwa kupata ruzuku lengo ikiwa ni kupunguza umasikini kwa wananchi kwa kuweza kumudu huduma za chakula, elimu na afya mahitaji ambayo ni ya msingi kwa mwananchi kwa kutekeleza miradi mbalimbali kulinda vyanzo vya maji, uchimbaji wa visima vya maji na upandaji wa miti kwenye vijiji vyao kwa ajili ya uhifadhi wa mazingira.

Wananchi wa kijiji cha mwena katika halmashauri ya wilaya ya masasi mkoani mtwara  ni kati ya wananufaika wa mradi wa PWP ambapo kupitia mradi huo wameondokana na shida ya maji  ya muda mrefu baada ya utekelezaji wa mradi wa usambazaji wa maji katika kijiji hicho kukamilika katika awamu ya kwanza kupitia Miradi ya Ajira za muda (PWP) kwa walengwa wa mpango wa kunusufu kaya masikini TASAF  awamu ya tatu.

Kufuatia utekelezaji wa mradi huo wananchi wa  kijiji cha Mwena wameipongeza serikali kwa kuanzisha utaratibu wa miradi ya ajira ya muda huo ambao wamesema licha ya kuinua kipato chao lakini umetatua shida ya maji kijijini hapo kupitia mradi wa kusambaza maji ulioanza kutekelezwa mwaka 2017 ambapo walifanikiwa kusambaza maji katika vitongo vyake kwa kuweka vituo  saba vya kuchotea maji.

Akiongea kwa niaba ya walengwa wengine Mtendaji wa kijiji Kelvin Milanzi alieleza kuwa walengwa wanaonufaika na mpango wa kunusuru kaya masikini pamoja na wananchi wa kawaida waliamua kuibua mradi huo wa kusambaza maji kwenye vitongoji vyao kutokana na wananchi kutumia muda mwingi kutafuta maji wakati kuna miundombinu ambapo kazi iliyokuwa imebaki ni kuchimba mitaro na kulaza mabomba ili watu wapate maji

“Mradi unalenga kuwaongezea kipato wananchi masikini katika kijiji hiki kwa kufanya kazi kwenye mradi tulioibua lakini mradi baada ya kukamilika unanufaisha wananchi wote ,hivyo pamoja na kwamba tumeongezewa kipato lakini pia wananchi tunapata maji” alisema Kelvin.

Kwa upande wake ndungu Esha Elifa Salum ambaye ni mnufaika wa mradi wa kunusuru kaya masikini alisema uwepo wa miradi ya ajira ya muda katika kijiji cha mwena umeisaidia jamii nzima kwa kuwezesha upatikanaji wa maji huduma ambayo ilikuwa haipatikani kwa urahisi japo kuwa walengwa wamepata faida mara mbili kwa kuboresha maisha  lakini pia kwa kupata huduma ya maji.

Usambazaji wa maji katika kijiji hicho cha mwena umegharimu shilingi  32,796,400 ambapo jumla ya shilingi 26,882,400  sawa na asilimia 75 zilitumika kulipa ujira kwa walengwa  na shilingi 5,914,000  Sawa na asilimia 25 zilitumika  kununua vifaa vya mradi kama mabomba koki na vitu vingine.

Mpango  wa TASAF III ni kuwatoa watanzania katika hali ya umaskini kwa kuwapa ruzuku itakayowasadia kupata huduma muhimu ikiwa ni pamoja huduma za afya, kuwasaidia watoto wao waweze kwenda shule lakini baadhi ya wanufaika wamekuwa wakitumia fedha hizo kulewa badala ya kuanzisha miradi midogo midogo kama ufugaji wa kuku, mbuzi na kondoo pamoja na kilimo ili miradi hiyo iwasaidie kuwaongezea kipato

Jumla ya kaya 10,570 zilibainishwa katika vijiji 97 vya  Halmashauri ya wilaya ya Masasi  ambapo kaya hizo kaya 3,068 zimejiunga na mfuko wa afya ya jamii(CHF) nakuziwezesha kaya hizo kupata huduma ya afya kwa gharama nafuu ambapo watu sita wa kaya moja wanalipia elfu kumi tu (10000) kupata huduma za afya kwa kipindi cha mwaka mzima kwenye mamlaka ya utekelezaji husika.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa