• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BARAZA LA MADIWANI LAPOKEA NA KUPITISHA TAARIFA YA FEDHA INAYOISHIA TAREHE 30 JUNI 2024

Posted on: August 29th, 2024

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Leo tarehe 29/08/2024, limeketi na kupokea taarifa za fedha Kwa mwaka unaoishia tarehe 30 Juni 2024.

Kwa mujibu wa kifungu Na.40 cha sheria ya fedha za Serikali za Mitaa ya Mwaka 1982, pamoja na agizo katika kanuni za fedha za Serikali za Mitaa Na.31(the local authority Financial Memorandum of 2009) zinaeleza halmashauri zote nchini kufunga mahesabu yake ya mwisho wa mwaka na kuwasilisha kwa Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali kabla au ifikapo tarehe 30 Agost ya kila mwaka.

Pia kupitia kanuni au mwongozo wa fedha za Serikali za Mitaa (LAFM) 2009 Na.31, taarifa ya mahesabu hayo yanapaswa kuwasilishwa katika Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango na hatmaye kwenye Baraza la madiwani kwa ajili ya kujadiliwa na kupitishwa na ndipo hesabu hizo kuwasilishwa kwa Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali.

Bw.Joseph Maduhu ni muhasibu Halmashauri ya Wilaya Masasi awali akisoma taarifa hiyo ya fedha za mwisho wa mwaka kwenye Kamati ya Fedha uongozi na Mipango na hatmaye mbele ya baraza la Madiwani amesema hesabu za Halmashauri za kuishia juni 2024 zimefungwa kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya utayarishaji wa hesabu za umma pamoja na Kanuni za Fedha za Serikali za Mitaa.

Amesema katika hesabu za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi za kuishia juni 2024 mizania (statement of Financial Position) inaonyesha hali halisi ya Halmashauri kwa tarehe 30 Juni 2024.

Amesema " Halmashauri ilimaliza mwaka wa fedha 2023/2024 tarehe 30 Juni 2024 ikiwa na albaki ya jumla ya shilingi Bilioni 4,063,544,626.00 katika akaunti zake za BoT, CRDB na NMB pamoja na akaunti za Shule, Vituo vya Afya, zahanati na Vijiji"

"Pia Halmashauri ilikuwa inadai jumla ya shilingi 534,649,716.67 toka Katika taasisi mbalimbali na Watumishi kwa mchanganuo ufuatao:

*Mikopo vikundi vya Wanawake na Vijana shilingi 458,481,606.57

*Wadaiwa wa ushuru wa korosho (Vyama vya Msingi) sh.76,168,110.00

Aidha Bw.Maduhu ameongeza kuwa, Halmashauri imefunga mwaka wa fedha 2023/2024 ikiwa na vifaa mbalimbali vilivyoko stoo kama vile madawa,shajala vyenye thamani ya sh.960,169,154 huku mali za kudumu kama vile Ardhi, majengo ya Ofisi, majengo ya makazi, majengo ya zahanati, Vituo vya Afya, hospital, Shule, Magari, pikipiki, mitambo n.k zikiwa na thamani ya sh.48,048,565,315 .

"Kwa mwaka 2023/2024 Halmashauri imejenga na kununua mali za kudumu zenye jumla ya shilingi 4,652,701,189.00 ambazo zimenunuliwa kwa ruzuku toka Serikali kuu Pamoja na fedha za mapato ya ndani."

Hata hivyo Bw.Maduhu katika taarifa hiyo amehitimisha kwa kusema kuwa Halmashauri pamoja na kuwa na hisa katika kampuni ya majani ya chai (TATEPA) na mtaji mwingine katika Bodi ya mikopo ya Serikali za Mitaa, kulingana na taarifa ya mwenendo wa fedha kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya utayarishaji wa hesabu mapato yalifikia sh.44,259,839.00 na matumizi sh.33,422,883,885.00 hivyo kufanya ziada ya sh.10,836,955,504.00 Kwa mwaka wa fedha ulioishia tarehe 30/06/2024.

Nao kwa upande wao waheshimiwa Madiwani baada ya kupokea na kujadili taarifa hiyo na hatmaye kuipitisha, wote kwa Umoja wao wameonyesha kuridhishwa na namna ambavyo imeandaliwa taarifa hiyo Kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya utayarishaji wa hesabu.

Baraza hilo la madiwani la kupokea taarifa za ufungaji wa mahesabu ya fedha za mwisho wa mwaka limefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo uliopo mbuyuni Masasi huku likiwashirikisha Madiwani, Wakuu wa Idara na vitengo, Viongozi wa vyama vya Siasa, Maafisa Tarafa, Kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya Pamoja na wadau wengine.

29/08/2024

@... Masasi DC

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa