• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

AHSANTE SANA MHE.RAIS DOKTA SAMIA SULUHU HASSAN KWA KUTUPATIA FEDHA ZA UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI YA AMALI MASASI DC

Posted on: December 24th, 2024


Halmashauri ya Wilaya Masasi imeendelea kunufaika na Uongozi wa Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt.Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Mnamo tarehe 30 June 2023/2024 katika mwisho wa mwaka wa fedha Rais Dokta Samia Suluhu Hassan aliipatia fedha Halmashauri ya Wilaya ya Masasi kiasi cha Shilingi Milioni 560,552,827, na Halmashauri ililazimika kuvuka nazo katika mwaka mpya wa fedha 2024/2025 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Amali.


Halmashauri ilianza kutangaza tenda na hatmaye kumpata mkandarasi ambaye alikubali kuifanya kazi hiyo Kwa moyo mmoja  Lakini siku chache tu mkandarasi huyo akaamua kuiacha  kazi hiyo kwa ridhaa yake mwenyewe, na ndipo Halmashauri ikachukua hatua za haraka kutangaza tenda kwa mara Nyingine na kubahatika kuipata kampuni ambayo ilianza utekelezaji wa mradi huo mara Moja.

Hata hivyo Kasi ya utekelezaji wa mradi huu imeelezwa kuwa  bado ulikuwa ni wakusua sua kutokana na kampuni kubainika kuwa na vibarua vingi katika maeneo mengine tofauti na mradi huu na ndipo sasa Halmashauri ililazimika kuuvunja mkataba na kuamua Sasa kuutekeleza mradi huu kwa kutumia mafundi wa kawaida (force account).


Mradi huu ambao unatekelezwa kwa fedha za Sequip unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Mwezi January 2025 umeanza tena utekelezaji wake mapema November 2024 huku ukijumuisha ujenzi wa vyumba vya madarasa 8 huku kila Jengo likiwa na Ofisi katikati yake, Jengo la utawala 1, Jengo la maabara ya kemia na Biolojia, Nyumba ya mwalimu (single) Maktaba, Chumba Cha Tehama, Vyoo vya wanafunzi matundu 4 (wav) Vyoo vya wanafunzi matundu 4 (was) kichomea taka pamoja na Tanki la Maji ya Ardhini.

Bw.Shaban Kinyongo ni Afisa Elimu vifaa na Takwimu Halmashauri ya Wilaya Masasi ameeleza kwamba mradi huu unatekelezwa kwa awamu mbili ambapo katika awamu hiyo ya pili mradi utapata mabweni kwa ajili ya kulala wanafunzi pamoja na bwalo " kwaiyo tunasubiria baada ya awamu hii ya Kwanza kukamilisha mradi, tutapata fedha nyingine katika kuendeleza mradi huu, hivyo nasisitiza mafundi waongeze Kasi katika ujenzi ili ifikapo January mwishoni iwe imekamilika na tuanze usajili wa wanafunzi katika Shule hii ya Amali ambayo ni mpya Katika Halmashauri yetu"..alisema bw.Kinyongo

 Ameongeza kuwa malengo na matarajio ya Halmashauri ya Wilaya ya Masasi na Serikali kwa ujumla mara baada ya kumalizika kwa ujenzi wa Shule hii ya Amali na  Wanafunzi kuanza kunufaika na  Elimu itakayotolewa kutaimarisha, kupanua na kuendeleza uwelewa  kwa kina wa maarifa, stadi na  mwelekeo alioupata katika hatua ya Elimu ya Msingi.

Kukuza stadi za ufundi na ujasiriamali zitakazo mwezesha kujiajiri, kuajiriwa na kuyamudu maisha kwa kutumia vizuri mazingira yake,"shule hii itazalisha  Wataalamu wengi sana"


Kuimarisha mawasiliano kwa kutumia stadi za lugha, kukuza tabia ya kujiamini na uwezo wa kujifunza kwenye nyanja mbalimbali zikiwemo sayansi na teknolojia, maarifa ya kinadharia na ufundi, kuimarisha uwajibikaji katika masuala mtambuka ya Jamii yakiwemo Afya, usalama ,usawa wa kijinsia na utunzaji endelevu wa mazingira.

Kukuza utayari wa kujiendeleza na mafunzo ya Elimu ya amali na sanifu au Sekondari hatua ya   juu.


Hata hivyo Bw.Kinyongo pamoja na kuwakumbusha wanafunzi waendelee kusoma kwa bidii Lakini pia amewasisitiza wazazi/walezi kuwaandaa  vizuri Watoto wao ili wajiunge na shule hiyo ambayo itakuwa ni chachu kwa Maendeleo Yao hapo baadaye baada ya kuhitimu na kupata cheti kitakacho onyesha taaluma-aliyosomea lakini watapata ujuzi wa kudumu ambao utawawezesha kujiari au kuajiriwa.

Shule hii ya Sekondari ya Amali ambayo inajengwa katika Kijiji Cha mbuyuni kata ya mbuyuni Halmashauri ya Wilaya Masasi ikikamilika inatarajia kusajili Watoto takribani 400 kwa mkupuo mmoja ( Madarasa 8 @wanafunzi 50) na huku ikitoa uwanja mpana wa kuimarisha uwezo wa mwanafunzi katika stadi za vitendo ili kuwapa maarifa na ujuzi unaohitajika katika soko la ajira la kisasa.

Hata hivyo ikumbukwe kuwa katika kuhakikisha Elimu ujuzi vinachukua nafasi Serikali imeanzisha mtaala wa Elimu ya amali, hasa baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kutaka mageuzi kwenye mfumo wa Elimu .


Rais Dkt. Samia ndiye aliyeanzisha mjadala wa kitaifa aliagiza kufanyike  Mapinduzi ya mfumo wa elimu nchini na hatmaye Watendaji wake wakaanza kuingia kazini na kufanya maboresho ya mtaala wa Elimu ya Msingi na Sekondari.

Shukrani.

Halmashauri ya Wilaya ya Masasi inaendelea Kutoa shukrani za dhati kwa mhe.Rais Dokta Samia Suluhu Hassan Kwa kutupatia Fedha kiasi cha shilingi Milioni 560,552,827 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Shule ya Sekondari ya Amali ambayo inajengwa katika Kijiji Cha mbuyuni kata ya mbuyuni Halmashauri ya Wilaya Masasi.

Na: Kitengo Cha Habari na Mawasiliano (H/W) Masasi.


24/12/2024

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa