• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MADAKTARI, WAUGUZI WAMETAKIWA KUTOA HUDUMA BORA KUPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO MASASI DC

Posted on: August 20th, 2020


Wakuu wa vituo vya kutolea huduma za afya Halashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara, wametakiwa  kutoa huduma bora kwa kuzingatia maadili ya taaluma zao  ili kupunguza vifo mama na mtoto vinavyotokea wakati wa kujifungua.

Agizo hili limetolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bibi Changwa Mkwazu wakati wa kufungua kikao kazi  kwa watumishi hao  kilicholenga kufanya tathmini ya mpango kazi wa utoaji huduma katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya  kila mwezi  na kutatua changamoto mbalimbali zilizojitokeza ili kuboresha utoaji wa huduma hizo.

Mkurugenzi  Mkwazu amewaeleze wakuu wa vituo  hao kuwa, kwa mjibu wa taarifa ya Mkoa   hali ya utoaji wa huduma,  imeonesha kuwa  kwa kipindi  cha miezi mitatu vifo 9 vya wajawazito  wakati wa kujifungua na  vifo 73 vya watoto  chini ya  miaka mitano  vimeripotiwa kutokea katika halmashauri  hiyo na kusababisha halmashauri kushika namba moja kati ya halmashauri 9 za mkoa huo.

Mkwazu  amesema kuwa “inaumiza sana kumpoteza mama au na mtoto wakati wa kujifungua wakati tungeweza kuzuia baadhi ya vifo  hivyo kwa kutoa rufaa mapema , kutoa elimu ya uzazi salama na mengine mengi,  hivyo , hizi takwimu za vifo sio nzuri hata kidogo, tekelezeni wajibu wenu ipasavyo”  

Aidha Mkurugenzi amewakumbusha wakuu wa vituo hao, kutoa elimu ya Uzazi salama kwa wajawazito ikiwemo umuhimu wa kuhudhuria kliniki, kula mlo kamili (lishe)  pamoja na kuwapima vipimo stahiki ikiwemo kipimo cha uwingi wa damu ili kupunguza vifo vinavyosababishwa na masuala hayo.

Pia Mkwazu amesema “Nawaagiza wakuu wa vituo vyote vya kutolea huduma  za afya  ambavyo havina mashine ya kupima uwingi wa Damu  vinunue haraka iwezekanavyo  kwani kuna vifo vingine vinasababishwa na mama mjamzito kutokuwa na damu ya kutosha wakati wa kujifungua”

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Bibi Miriam Cheche  amesema kuwa, kwa mujibu wa ripoti ya mkoa, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi imeongoza kuwa na vifo vingi  vya mama na mtoto  ambapo vifo 8 kati ya 9 vilitokea Hospitali ya Rufaa Ndanda na kati ya watoto 73 walifariki, vifo 33 vilitokea kituo cha afya Nagaga

Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo Bibi Miriam Cheche akitoa maelekezo kwa wakuu wa vituo vya kutolea huduma leo  tarehe 20.08.2020 kwenye kikao kazi cha tadhimini ya utoaji huduma kwa miezi mitatu iliyopita

Cheche ameeleza kuwa “sababu kubwa iliyopeleka Hospitali ya  Rufaa ndanda na kituo cha Afya Nagaga kuwa na vifo vingi ni kutokana na kuhudumia watu kutoka maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya Halmashauri lakini tutajitahidi kuongeza umakini na ubora katika kutoa huduma zetu  kwa wagonjwa hasa wajawazito “

Aidha Kaimu Mganga Mkuu huyo amewasisitiza wakuu wa vituo vya kutolea huduma za afya kutoa rufaa ya kwenda hospitali kubwa kwa haraka pale mama mjamzito anapokuwa na changamoto ya kujifungua kwenye kituo chake.



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI YAMKABIDHI PIKIPIKI MPYA AINA YA SANLG BW.YUSUF SIJAONA KARUME KAMA FIDIA.

    June 26, 2025
  • WATUMISHI WA UMMA WILAYANI MASASI WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA PEPMIS PIPMIS

    June 26, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI LAVUNJWA RASMI.

    June 19, 2025
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA YAANZA VIZURI MASASI DC

    June 17, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa