• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UJIO WA MWENGE WA UHURU MASASI KUMULIKA UWEKEZAJI KATIKA ELIMU

Posted on: June 5th, 2018

Ujio wa mwenge wa uhuru katika  Halmashauri ya Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara utakaopokelewa na kukimbizwa   tarehe 13 juni, 2018 , unatarajia kuona kwa vitendo uwekezaji katika elimu kwa kupitia miradi  ya miundombinu na jinsi jamii  inavyoshiriki katika kuboresha elimu kwa kutoa chakula mashleni  na kujenga miundombinu kama madarasa lengo ikiwa kufanya mazingira ya kufundishia na kujifunzia kuwa mazuri na hivyo kuinua ufaulu.

Akiongea ofisini kwake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi Changwa M. Mkwazu alisema, Mwenge wa uhuru ukiwa Masasi utakimbizwa kwenye vijiji 18 kata 8 na tarafa 3 na utapokelewa katika kijiji cha Mpeta na kukimbizwa katika Vijiji vya Chiungutwa, Ndwika, Nagaga, Namombwe, Mkwaya na utakesha katika kijiji cha Mnavira kata ya Mnavira ambapo katika miradi hiyo miradi ikiwemo ya  elimu iliyotekelezwa kwa fedha za serikali na nguvu za wananchi itawekewa mawe ya msingi .

Mkwazu alieleza kuwa  kwa ujumla, Mwenge wa Uhuru ukiwa  katika Halmashauri hiyo, utaweka mawe ya msingi katika miradi minne (4) , kuzindua klabu ya wapinga rushwa na kugawa hundi za mikopo kwa vikundi 41 vya wananwake na vijana zenye thamaani ya shilingi milioni 144,219,000.

Mkurugenzi aliendelea kueleza kuwa, Kama ujumbe na kauli mbiu ya mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu 2018 unalenga kuwekeza katika elimu, halmashauri ya wilaya ya masasi imeendelea kutekeleza kwa vitendo kwa kujenga miundombinu na kutoa elimu kwa jamii juu ya kushiriki katika kuboresha elimu ikiwemo kuchangia chakula  ili wanafunzi kupata chakula cha mchana.

Akifafanua juu ya miradi itakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru Mkurugenzi alisema, Miradi itayowekewa mawe ya masingi na Mwenge wa Uhuru  ni  mradi wa ujenzi wa madarasa 7, maabara 1 mabweni 2 na jengo la utawala 1 katika shule ya wasichana ndwika unaoghalimu shilingi milioni 400, ujenzi wa majengo ya wodi 1,  chumba cha upasuaji 1,maabara 1, mochwari 1 na nyumba ya mtumishi 1 katika kituo cha Nagaga unaogharimu shilingi 400, mradi wa maji makong’onda –rivango unaogharimu shilingi bilioni 1,415,000,000, ujenzi wa madarasa 3 shule ya msingi Mnavira unaogharimu shilingi milioni 26,000,000  kwa nguvu ya wananchi na halmashauri na hundi za mikopo kwa vikundi  41 vya wanawake na  vijana zenye thamani ya shilingi milioni 144,219,000

Hivyo Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2018 utapitia  miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 2,385,219,000 Alisema  Mkwazu.

Kuhusu Ujumbe  na Kauli mbiu ya  Mbio Za Mwenge wa Uhuru 2018 inayosema “UWEKEZAJI KATIKA ELIMU”  chini ya kauli mbiu inayosema  “ELIMU NI UFUNGUO WA MAISHA, WEKEZA SASA” Mkwazu ameeleza kuwa halmashauri inatekeleza kwa vitendo kwani elimu imeendelea kuboreshwa kimiundombinu lakini pia  jamii imeendelea kuelimishwa juu ya dhana ya Elimu bila Malipo ambapo wazazi wamehamasika kuchangia na kusimamia zoezi la utoaji wa  chakula mashuleni  na kujenga miundombinu kama madarasa lengo ikiwa ni kuongeza ari ya wananfunzi kupenda shule na hivyo kuinua ufaulu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa