• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAIS MSTAAFU WA TANZANIA BENJAMIN MKAPA AZIKWA KIJIJINI KWAKE LUPASO

Posted on: July 30th, 2020

Tarehe 29.07.2020 Rais mstaafu wa Tanzania awamu ya tatu, Benjamin William Mkapa amezikwa kijijini kwake  Lupaso, Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara baada ya kufariki dunia  tarehe 24.07.2020 kwa mstuko wa moyo akiwa hospitali jijini Dar es Salaam alikokuwa anatibiwa ugonjwa wa Malaria.

Katika mazishi hayo, Mamia ya waombolezaji  kutoka maeneo mbalimbali  ya wilay ya Masasi na mikoa jirani  walijitokeza kuuaga mwili wa rais huyo kwa kutoa heshima za mwisho kabla ya kumzika katika makaburi yaliyopo nyumbani kwake kijiji cha lupaso alikozaliwa.

Wananchi wakifuatilia shughuli ya Mazishi ya Rais mstaafu wa Tanzania awamu ya tatu, Benjamin William yaliyofanyika nyumbani  kwake  Lupaso 

Mazishi hayo yamehudhuriwa na Rais wa Jamuhuri ya muungano wa  Tanzania Dkt John Magufuli pamoja na marais wastafu Jakaya Kikwete na Ali Hassan Mwinyi, ambao wamemsifu kiongozi huyo kwa mchango mkubwa katika ujenzi wa taifa hilo, kupitia nafasi mbalimbali alizozishikilia.

Katika shughuli ya mazishi hayo Mhe. Rais wa Tanzania John Magufuli amewataka watanzania waendelee kumuombea Hayati Rais Mkapa na kuwasisitiza kuiga tabia zote njema alizokuwa nazo wakati wa uhai wake ikiwa pamoja kuwa mzalendo wa kweli na kupenda nyumbani kwao.

Rais wa Jamuhuri ya muungano wa  Tanzania Dkt John Magufuli ( wa kwanza kushoto)pamoja na marais wastafu Jakaya Kikwete na Ali Hassan Mwinyi akitoa heshima baada ya kuweka shada la maua kwenye kaburi la Hayati Benjamin Mkapa

Magufuli amesema Mkapa aliyaishi maisha yenye upendo wa kweli na alipenda nyumbani kwao kwani hata pale serikali ilivyojaribu kutenga eneo maalumu la kuzikia viongozi wa kitaifa jijini Dodoma alipinga wazo hilo na kuagiza atakapofariki azikwe kijijini kwao kwenye makaburi ya familia.

Kwa upande wake Rais mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete, amemuelezea Hayati Benjamin Mkapa kama kiongozi aliyechukia nchi na watu wake kuwa maskini na kulipa kipaumbele suala la uchumi kwa  kuanzisha dira ya taifa ya kufikia uchumi wa kati ifakapo mwaka 2025 na pato la mtanzania kufikia dola 3000.

Kikwete alifafanua kuwa “Niliendeleza sera hiyo katika uongozi wangu na kwa sasa Rais Wetu wa awamu ya Tano anaendelea nayo ambapo sasa Tanzania ni moja ya nchi zenye uchumi wa kati, tunaenda vizuri”

Ameongeza kuwa Hayati Benjamin Mkapa alikuwa kiongozi mwenye utambuzi na manufaa kwa wananchi wake kwa kuwa alipenda kusikiliza, kushughulikia changamoto na kutoa mrejesho.

Akizungumza katika shughuli ya mazishi ya Mkapa, rais mstaafu wa awamu ya pili. Mzee Ali Hassan Mwinyi alisema hayati Benjamin Mkapa alikuwa mwanadamu na ana makosa yake kama wengine hivyo aombewe kwa Mwenyezi Mungu.

"Huenda alifanya makosa asiyopenda Muumba wetu, tumuombee msamaha kwa mwenyezi Mungu amsamehe madhambi yake, amuwie radhi, Mkapa alikuwa mtu mwema na mkrimu, asiependa masihara kwenye kazi," alisema Mwinyi.

Rais mstaafu wa Tanzania awamu ya tatu, Hayati Benjamin William Mkapa alizaliwa mwaka 1938  kijiji cha lupaso katika Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara.

Viogozi mbalimbali  wa Serikali wakiwa kwenye hafla ya Mazishi ya Benjamin Mkapa


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa