• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MATUMIZI YA MBEGU BORA YA MUHOGO FURSA YA KUKUZA UCHUMI NA UPATIKANAJI WA CHAKULA

Posted on: March 7th, 2018

Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara wametakiwa kuwahamasisha wananchi wao kulima kilimo cha muhogo kinachotumia mbegu ya kisasa aina ya kiroba badala ya mbegu za asili ambayo inastahimili ukame na magonjwa   lengo ikiwa ni  kueongeza kipato na kuwa na uhakika wa chakula.

Viongozi hao walielezwa hayo kwenye warsha iliyoendeshwa na taasisi ya  kimataifa ya  kilimo inayojihusisha na utafiti wa masuala ya kilimo IITA kwa kushirikiana na MEDA na wizara ya kilimo iliyolenga kuwahamasisha viongozi hao kuweka mipango ya kuwekeza katika mbegu bora za muhogo ili kuweza kutosheleza mahitaji ya mbegu hizo kwa wakulima na kuongeza uzalishaji.

Akizungumza na viongozi hao  ndugu Davis Mwakanyamale kutoka taasisi ya IITA alisema tafiti ya mbegu hizo ilikuja kwa ajili ya kutatua changamoto nyingi zinazowakabili wakulima wa muhogo  kwa kutumia mbegu bora za kisasa ambazo hazishambuliwi na magonjwa kwa kuwezesha upatikanaji wa mbegu hizo katika ngazi ya vijiji na kata badala ya kutegemea taasisi zinazozalisha mbegu pekee.

Mwakanyamale alisema kuwa mbegu za asili zinashambuliwa sana na magonjwa kama Batobato na Michirizi Kahawia  hali inayopelekea  uzalishaji wa zao hilo  kutokuwa na tija, wakati mbegu ya kiroba ambayo inastahimili magonjwa, kuzalisha kwa wingi (tani 20-30 kwa hekta moja), zinakomaa kwa muda mfupi (Hukomaa miezi tisa tu baada ya kupanda) ukilinganisha na mbegu za asili ambazo pamoja na kushambuliwa na magonjwa lakini pia uzalishaji  wake ni mdogo ambapo hekta moja inazalisha chini tani tano tu.

 Mwakanyamale alisema kutokana na umuhimu wa zao la muhogo serikali imeliweka zao la Muhogo  miongoni mwa mazao ya kipaumbele ya kuzalishwa kibiashara katika awamu ya pili ya mapango wa maendeleo ya sekta ya kilimo(ASDP)  hivyo ni wakati mwafaka kwa halmashauri kuweka mkakati wa kuzalisha mbegu bora ili kurahisisha upatikanaji wa mbegu hizo kwa wakulima.

Kwa upande wa mtaalamu kutoka taasisi ya MEDA inayojihusisha na utayarishaji wa mbegu bora za muhogo ndugu Erick Mwongolo alisema waheshimiwa madiwani ndio watakaosaidia kufikisha ujumbe wa hamasa kwa wakulima juu ya uzalishaji na matumizi ya mbegu bora  za muhogo ili kutumia fursa hii kuongeza kipato na upatikanaji wa chakula wa wananchi wao.

Mihogo  ya asili ni ile iliyoendelea kulimwa miaka mingi iliyopita na kurithiwa vizazi kwa vizazi. Mihogo hii ina sifa kadhaa ikiwemoHutoa mavuno wastani wa tani kwa Hekta, Mingi inachukua muda mrefu kukomaa, inahifadhika shambani kwa muda mrefu bila kuoza, hushambuliwa na magonjwa kama Ugonjwa wa michirizi ya ki-kahawia, batobato na blaiti, Hushambuliwa na wadudu milibagi na imezoeleka na wakulima hivyo wanaijua tabia yake na jinsi ya kuitunza.

Kuna  zaidi ya aina 45 za mihogo zinajulikana nchini Tanzania. Zaidi ya asilimia 80 ya mihogo ni ya asili. Hivyo ni kusema wakulima wengi hawatumii mbegu bora. Ingawa wakulima wengi pia hupendelea kulima mihogo michungu kwa sababu haishambuliwi sana na wadudu ama magonjwa shambani na makopa yake yanahifadhika kwa urahisi, zaidi ya asilimia 70 ya mihogo ni mihogo baridi

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa