• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MASHINDANO YA UMITASHUMTA KANDA YA MASASI YAZINDULIWA,WANAFUNZI WAKUMBUSHWA UMUHIMU WA MICHEZO

Posted on: June 9th, 2017

Wananfunzi wa shule kutoka katika Wilaya za Masasi na Nanyumbu wamehimizwa kushiriki michezo kikamilifu kutokanana na michezo kuwa njia nzuri kwa wananfunzi hao kuwa na afya njema ya akili na mwili hali ambayo itawasaidia kutimiza ndoto zao za kielimu na kuendeleza vipaji vyao.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halamashauri ya Wilaya ya Masasi  bibi Changwa M Mkwazu wakati wa uzinduzi wa mashindano ya  michezo ya UMITASHUMTA kanda ya Masasi  yanayofanyika katika shule ya sekondari Abbey Ndanda kuanzia jana tarehe 8.06.2017 ambapo wanafunzi kutoka wilaya  ya Masasi na Nanyumbu wanashiriki katika michezo ya aina mbalimbali.

Bibi Changwa aliwaeleza wanamichezo hao kuwa michezo ina faida kubwa katika maisha yenu kiafya ambapo kupitisha michezo mtaepuka kupata mgonjwa  yanayotokana na kutofanya mazoezi kama vile shinikizo la damu, kuwa na uzito mkubwa zaidi na mengine ambayo yatasababisha mshindwe kutimiza ndoto zenu za kielimu lakini pia kusababisha kifo.

“Suala la michezo ni mhimu kwa ustawi wa afya zetu na uchumi kwani jamii yenye watu ambao hawana afya njema itakuwa masikini kwani hataweza kushiriki kikamilifu katika shughuli za uchumi hali ambayo itapelekea kuwa na watu masikini, kutokana na hali hiyo ndio maana serikali imefanya kila jumamosi ya pili kila mwezi kuwa siku ya mazoezi nchi nzima” alifafanua Changwa.

Changwa aliongeza kuwa pamoja na kuwa michezo kuwa ni  afya lakini pia ni chanzo cha ajira kwani wenye vipaji vya mchezo  Fulani watapata fursa ya kuchaguliwa kuwa wachezaji wa timu mbalimbali za ndani na nje kama baadhi ya watanzania wenzetu ambao wanachezea timu za taifa, vilabu mbalimbali na wanapata kipato kikunbwa kama vile Mbwana Samatta (Mtanzania),Ronaldo wa Ureno, Messi wa Algentina na wengine wengi.

Bibi Changwa alitoa rai kwa wanamichezo wote kuwa na nidhamu katika michezo, alisema “ mmetoka kwa wazazi wenu mkiwa salama, msituangushe, msije mkawa vijana wabaya mkapata maradhi lakini pia mjiepushe utumiaji wa lugha chafu na matusi, uvaaji mbaya mkazitia aibu wilaya zenu”.

Aliwaomba Maafisa Michezo na walimu walezi wa watoto hao kuhakikisha watoto wanatunzwa vizuri ili kufanya lengo lao linafikiwa na kurudi salama kwa wazazi wao ili kujenga imani kwa wazazi , waepuke kabisa na mambo ambayo yatawatoa nje ya lengo la michezo, alisema “ nina maana kwamba watoto walelewe kwa kujali jinsia zao kama ambavyo tunalea watoto wetu na baada ya michezo hii kuisha hatutapenda kusikia kesi zozote za utovu wa nidhamu na maadili”.

Alitumia fursa hiyo kuwashukuru waliotoa ufadhili wa hali na mali ambo ni mkuu wa shule ya sekondari ya Abbey kwa kuruhusu kutumia eneo lake kwa mashindano, pia mwalimu mkuu wa shule ya msingi Ndanda na Njenga kwa kutoa huduma mbalimbali ikiwemo malazi kwa siku zote za mashindano.

Akisoma risala mbele ya mgeni rasmi mratibu wa mashindano hayo kwa upande wa Halmashauri ya wilaya ya masasi Mwalimu Fadhili Swalehe (Shule ya msingi Mkalapa) alisema mashindano haya yalianza toka ngazi ya shule, kata na sasa kanda na kisha yatafanyika katika ngazi ya mkoa ambapo baada ya kupata wachezaji bora watakwenda kushindana ngazi ya Taifa.

Mwalimu Swalehe alisema katika ngazi hii ya kanda kuna jumla ya wanafunzi 180 na walimu 27 kutoka halmashauri tatu(masasi, Nanyumbu na Masasi Mji) na baada ya mashindano hayo wanategemea wanamichezo 100, walimu wa michezo na viongozi 11 ambao jumla yao ni 111, hawa ndio watakaoenda kushindana ngazi ya mkoa  na baadaye kupata timu ya mkoa itakayoenda kushindana kitaifa mkoani Mwanza.

Pia alisema pamoja na kufikia hatua hii ya mashindano, timu hizo zimekumbana na hali ngumu ya kifedha ili kupata timu hizo, alimuomba Mkurugenzi Mtendaji kwa kutumia mabaraza ya Waheshimiwa Madiwani waone ni namna gani wanaweza kusaidia kuwa na mfuko wa michezo wa wilaya kwa kutumia vyanzo mbalimbali vya mapato ili miaka ijayo maandalizi yafanyike mapema na kwa ufasaha zaidi na hatimaye timu zetu zitafanya vizuri zaidi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa