• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KILIMO CHA MKATABA NI SULUHISHO LA SOKO LA MAZAO MCHANGANYIKO KWA MKULIMA

Posted on: August 5th, 2017

Kwa mujibu wa hotuba ya mgeni rasmi wa maonesho ya sikukuu ya wakulima nanenane 2017 waziri wan chi ofisi a rais  TAMISEMI Mhe George Simba Chawene  alisema kuwa Sekta ya kilimo ni sekta yenye mchango mkubwa sana katika kukuza uchumi wa nchi na wakulima kwa ujumla kama  takwimu za mwaka 2015  zinavyoonesha kuwa sekta ya kilimo iliweza kuchangia pato la taifa kwa 29% na mwaka 2016  ikiwa ni 29.1% 

Kwa upande wa chakula mwaka 2015 nchi ilikwa na utosherevu wa chakula kwa  123% na mwaka 2016 ilikuwa 120%  nah ii imetokan na ongezeko la  mazao ya chakula kwa 6.7%  hivyo kilimo ni sekta muhimu sana katika kufikia uchumi wa kati kwani taifa lenye njaa haliwezi kujishughulisha katika shughuli za maendeleo.

Kwa upande wa ajira, sekta ya mifugo na uvuvi  asilimia  65 watanzania  wamejiajiri kupitia  shughuli mbalimbali za kilimo mifugo na uvuvi.  Hivyo  kama sekta hii ikisimamiwa vizuri inauwezo wa kupunguza tatizo la ajira kwa watanzania wengi hususani vijana ambao ni nguvu kazi katika  uzalishaji wa malighafi kwaajili ya viwanda vya ndani.

Pamoja na mafanikio makubwa ya kilimo wakulima wameendelea kuwa na changamoto kubwa ya kupata masoko ya uhakika ya kuuza mazao yao baada ya kuzalisha kwa tija. Uzoefu unaonesha kwamba mkulima anatumia nguvu na mali  nyingi kuhakikisha anazalisha kwa tija lakini baada ya kuvuna hakuna soko la uhakika la kuuzia bidhaa zao.

Kwa kipindi cha msimu wa mwaka 2016/2017 wakulima wamekuwa na changamoto ya kushuka kwa bei ya mazao mchanganyiko ikiwemo choroko, mbaazi na mengine yameuzwa kwa bei ya ndogo sana kutokana na bei ya soko kushuka bila kuzingatia gharama alizotumia  mkulima katika uzalishaji, hali hiyo imewakatika tama wakulima wa maeneo mengi ikiemo wakulima wa masasi.

Katika kuhakikisha wakulima wanakuwa sehemu ya kutatua changamoto za ukosefu wa masoko hasa kwa wakulima, kampuni ya TEMNAR Company Limited  inayojishughulisha na usindikaji wa mbegu za mafuta na kuzalisha mbegu imeamua kuwaelimisha  wakulima kujikita katika kilimo cha Mkataba ili kujihakikishia soko la mazao yao.

Akizungumza wakati wa maaonesho sikukuu ya wakulima maarufu kama Nanenane mhasibu na mwelimishaji kutoka kampuni ya  TEMNAR Company Limited bi Bahati Hassan Mohamed alisema  kuwa kampuni yao iliamua kujikita  katika kuelimisha wakulima kulima kilimo cha mkataba ambacho  kinampa nafasi mkulima kupanga  bei ya mazao yake  na kampuni  kabla ya kuzalisha hali inampa uhakika wa kuuza kwa faida tofauti na kutegemea soko huria ambalo halimpi mkulima nafasi ya kupanga bei japo amezalisha kwa tija.  

Bahati alisema kuwa kampuni yao baada ya kuona wakulima wanapata shida ya masoko waliamua kuanzisha kilimo cha mkataba ambapo mkulima anazalisha akiwa anauhakika wa soko la mazao yake kwa kujaza mkatababa na kuuziana mazao kwa bei ambayo mkulima haimpi hasara lakini pia kuwawezesha kupata mbegu bora pamoja na kuwafuatilia kuhakikisha wanazaisha wa tija na viwango katika vikundi.

“Kilimo cha mkataba kimewavutia wakulima wengi alioweza kufikiwa na eimu hiii katika mikoa ya Mtwara na Lindi ambapo na wakulima wanazalisha kwa tija lakini pia wanapata faida tofauti na kuuza kwenye soko huria na kampuni inapata malighafi ya kutosha ya kusindika bidhaa za mafuta” alisema Bahati

Pamoja na kuwa mkulima anapata uhakika wa soko lakini pia kampuni hiyo inakuwa na uhakika wa kupata malighafi ya kusindika mafuta kutokana na mazao ya ufuta, karanga na alizeti. Hivyo kilimo hiki kinamfaidisha mkulima na kinafaidisha kampuni kwani mkulima anauhakika wa kuuza mazo yake lakini pia kampuni inauwezo wa kuzalisha kwa wingi kutokana na uwepo wa malighafi za uhakika.

Wakati tunawahamasisha wakulima kuzalisha kwa tija mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi ni vizuri pia tukawahamasisha wakulima kujikita katika kilimo cha mkataba ambacho kitawahakikishia soko kwa mazao yao na hatimaye mkulima atajikomboa kupitia kilimo tofauti na hali ilivyo sasa ambapo mkulima hana nafasi ya kuuza kwa tija kama alivyozlisha kwa tija.

Ili kuitekeleza kwa vitendo kaulimbiu ya maonesho ya nanenane mwaka huu 2017 inayosema “Zalisha kwa tija mazao na bidhaa za kilimo, mifugo na uvuvi ili kufikia uchumi wa Kati”  uzalishaji huu uende sambamba na uhakika wa soko kwa kujita katika kilimo cha mkataba ambacho kinamhakikishia mkulima kuona matunda ya alichofanya.

Hivyo makampuni ambayo yanahitaji kununua mazao kwa mkulima ni vyema yakaingia mikataba na wakulima walioko kwenye vikundi ili baada ya kuzalisha mfanyabiashara aweze kununua mazao kwa mkulima kwa bei waliokubaliana na sio  kuwapangia kwani  mauzo hayataenda kinyume na mkataba waliowekeana awali 

Ili kufikia uchumi wa kati, mkulima aangaliwe zaidi asipangiwe bei na wafanyabiashara/mnunuzi , watumie begu bora, kuzuia ununuzi holela na kusimamiwa vizuri kulima kilimo cha kisasa ili mazao yanayozalishwa yawe na ushindani katika soko.

 

 

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA NeST NA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI

    March 12, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa