• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BI.BEATRICE MWINUKA AKABIDHI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA NDG ALPHAXARD MASHAURI ETANGA.

Posted on: February 11th, 2025


Imeandaliwa na:

Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini.


Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Bi.Beatrice Claver Mwinuka amekabidhi rasmi Ofisi kwa Mkurugenzi mpya wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Ndg.Alphaxard Mashauri Etanga.

Makabidhiano hayo yamefanyika Leo tarehe 11/02/2025 katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa Halmashauri

hiyo Mhe.Ibrahimu Chiputula ambaye pia ni Diwani wa kata ya Mpeta, huku baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo nao wameshiriki.

Awali akizungumza kwenye makabidhiano hayo Bi.Beatrice Mwinuka ameendelea kumshukuru mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumuamini na kumteua tena kwenda kuiongoza Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa na kwamba kwa uzoefu alioupata wakati akiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi anaimani kubwa anakwenda kuivusha Kilosa kwa Maendeleo zaidi.

Vilevile pamoja na kutumia nafasi hiyo kumkaribisha Mkurugenzi mpya wa Halmashauri hiyo Ndg.Alphaxard Etanga pia amewashukuru Watumishi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi pamoja na Baraza zima la Madiwani kwa ushirikiano mkubwa waliompatia kwa kipindi chote alichohudumu katika Halmashauri hiyo na kwamba yupo tayari kutoa ushirikiano pindi watakapohitaji mawazo yake, na wao pia waendelee kumpa ushirikiano kama walivyokuwa wakimpatia yeye.


Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Ndg.Alphaxard Etanga pamoja na kumshukuru mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kumteua kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, pia amehaidi kushirikiana na timu yake ya Wataalamu pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri kuendeleza kile ambacho yeye amekifanya ili kuona Halmashauri ya Wilaya ya Masasi inaendelea kupiga hatua kimaendeleo kupitia Miradi ambayo inatekelezwa.

"Mimi nikuombe Bi.Beatrice kwamba nimepokea taarifa hizi ambazo umenipa, nitazipitia kwa kina,nitashirikiana na timu yangu ya Wataalamu pamoja na Mwenyekiti wetu wa Halmashauri na baada ya hapo tutaendeleza kila kizuri ambacho umekifanya, tunatambua kwamba umefanya kazi kubwa kwa kipindi kifupi, kuna Miradi ambayo umeitekeleza na kuanzisha mimi nakuhaidi nitaiendeleza"....alisema Ndg.Etanga


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe.Ibrahimu Chiputula akizungumza kwa niaba ya Baraza la Madiwani amesema, wana Masasi bado wataendelea kumkumbuka Mwinuka kwa mazuri aliyoyafanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi na hivyo wanamuombea kwa Mwenyezi Mungu kheri na afya njema kwenye majukumu mapya ya kazi.

"Wape salamu Kilosa, tunaamini yale mazuri uliyotufanyia huku basi tunatamani ukawafanyie wanakilosa, nakushukuru tumefanya kazi kwa ushirikiano "


Pia Chiputula akahitimisha kwa kumkaribisha katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi,  Mkurugenzi huyo mpya Ndg.Alphaxard Mashauri Etanga na kumueleza kwamba wana Masasi wanamatumaini makubwa kutoka kwake hivyo washirikiane katika kuijenga Halmashauri ya Wilaya ya Masasi na wanatamani yale mazuri yanayoonekana katika maeneo mengine yapatikane katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.

"Nakukaribisha, unatimu ya Menejimenti, utakuwa pia na Madiwani hivyo karibu sana tufanye kazi ili tuivushe Halmashauri yetu katika viwango".


Ikumbukwe kuwa tarehe 24 /01/2025 mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan alifanya uteuzi kwa baadhi ya Viongozi mbalimbali, na katika uteuzi huo Ndg Alphaxard Etanga alikuwa ni miongoni mwa walioteuliwa na kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi huku Beatrice Mwinuka akihamishwa na kupelekwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro .

11/02/2025

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa