• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WIKI YA FAMILIA HALMASHAURI YA WILAYA MASASI YAANZA KWA KISHINDO

Posted on: May 2nd, 2024

Katika kuelekea kilele Cha maadhimisho ya Siku ya Familia Duniani, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara kupitia Divisheni ya Maendeleo ya jamii imeendelea Kutoa Elimu kwa umma kwa kufanya vipindi vya Redio, midahalo na mijadala ya wazi Katika vijiwe vya boda boda, mashuleni, na vijijini Lengo likiwa ni kuwajengea uwelewa  na kuwakumbusha wajibu na mchango wao Katika Maendeleo ya Familia zao, jamii na Taifa kwa ujumla.


Akizungumza Katika mkutano wa hadhara ambao umefanyika Leo tarehe 02 /05/2024 katika Kijiji Cha Mitonji, Kata ya Mbuyuni  Halmashauri ya Wilaya Masasi Bw. Muhsini Kombo ambaye ni Afisa Maendeleo ya jamii wa Halmashauri hiyo amesema kwamba, kwa mujibu wa kauli mbiu ya maadhimisho hayo ya wiki ya familia kwa mwaka huu yanasema Tukubali tofauti zetu kwenye familia, kuimarisha Malezi ya Mtoto, imelenga sana Moja kwa Moja kuijenga Familia yenye ubora kwa kutengeneza usawa wa familia iliyo na amani, upendo na kuziondoa zile tofauti mbalimbali ambazo zinajitokeza kwenye familia kama vile tofauti za kimawazo, kifikra, kipato, kitamaduni, kijamii n.k ambazo hizo ndio chachu ya kuzifanya familia zisiwe bora na kupeekea Malezi duni kwa Watoto na kutofikia mustakabali wa Familia n malengo yao kwa ujumla.


Amesema"tofauti hizi Sasa labda kuvunjika kwa ndoa, ukatili wa kijinsia kwa Wanawake na Watoto kwasababu Watoto hawa pia wanaweza wakakosa haki zao za Msingi Kama vile kuishi, kusomeshwa, kupata Lishe Bora n.k, hivyo basi ili kujenga au Familia ipate Malezi bora lazima tuhakikishe tunakuwa wasimamizi wazuri kwa Familia bila kujali tofauti zetu, ambapo nina imani kubwa tukifanya haya sote kwa pamoja tutapata malengo chanya ambayo yatasaidia kufikia Malezi yaliyo Bora kwa Watoto wenu, kwani Watoto hawa tunaowalea Leo hii ndio Wazazi na Walezi wa family za kesho".


Aidha Bw.Kombo ameongeza kuwa, katika kutumia fursa ya wiki hii ya Familia hadi kilele chake ifikapo tarehe 15/05/2024 ni lazima tuendelee kuhamasishana uwelewa wa matatizo ambayo yanazikumba Familia kwa ujumla kutokana na Maendeleo ya kiteknolojia, utandawazi na mitandao ya kijamii ambapo Ndani ya familia lazima utakutana na watu wa ukweli wenye kuwa na Moyo wa upendo, ukarimu na mshikamano, kwasababu upendo unapokosekana Katika Familia ndio matatizo ya baadaye huzaliwa ndani ya familia, lakini pia hata uhusiano wa Jamii kwa maana familia ni Msingi na kiunganishi Cha familia na jamii yake inayomzunguka.


Amesema pia katika Familia ni mahali ambamo kila mmoja yupo na anapata mambo ya Kweli zaidi hivyo anapenda Sana kuwahasa watanzania kutenga muda wa kutosha kukaa na familia zao ili kujadili, kushauriana na kutekeleza masuala muhimu ya kuendeleza familia zao kwani familia Ndio kitovu Cha Maendeleo na pia kama Kuna Watumishi nao wanawajibu wa kutenga muda wa kazi na muda wa kushughulikia Familia zao ili kujenga maadili na Maendeleo ya Familia.


Ameendelea kwa kusema kuwa, "Familia nyingi za kitanzania zinakabiliwa na kuwepo kwa mila na desturi zenye kuleta madhara Kama umaskini uliokithiri , mawasiliano na miundombinu mibovu ambayo husababisha hali ya maisha ya Watu kuwa duni na tegemezi na hatmaye kutumia muda mwingi wa kufanya kazi bila kujali madhara yatakayotokea kwa familia.


Bi.Mariam Said na Hatib Idrisa ni baadhi ya Wananchi ambao wameshiriki mkutano huo,  pamoja na kushukuru kwa kufikishiwa  Elimu hiyo inayohusu Familia ambayo ni muhimu kwao na hivyo kuomba suala hilo liwe endelevu, pia wameiomba Serikali kutunga Sera na Sheria Kali kwa Wazazi ambao Mara nyingi wamekuwa  wakienda kuolewa huku nyuma  wakiwatelekeza Watoto wao na kupelekea  kijilea wao wenyewe hali ambayo inawaweka Watoto hao katika mazingira magumu hususani kukosa ulinzi na Malezi bora.


Maadhimisho ya wiki ya familia yanatokana na tamko la Baraza la Umoja wa Mataifa Na.47/257 la tarehe 20 Septemba 1993 linaloidhinisha kuwa na siku maalumu kwa ajili ya familia, na Tanzania ni Moja ya wanachama wa Umoja wa Mataifa hivyo huungana na nchi Nyingine kila Mwaka kuadhimisha  siku hii .


Kwa Mwaka huu maadhimisho haya kwa Mkoa wa Mtwara yatafanyika  kimkoa katika Kijiji Cha Majengo Kata ya Ziwani Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Tarehe 15/05/2024 huku  Mkuu wa Mkoa wa Mtwara mhe.Kenan Patrick Sawala anatarajia kuwa Mgeni rasmi.


 Imeandaliwa na Winifrida Ndunguru.

    Afisa Habari Halmashauri ya Wilaya Masasi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa