• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WENYEVITI WA VIJIJI WAPEWA SEMINA ELEKEZI HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI

Posted on: January 22nd, 2021

Halmashauri ya wilaya ya Masasi leo Tarehe 22/01/2021 imefanya semina elekezi kwa wenyeviti wa vijiji 166 katika kata 34 zilizopo ndani ya Halmashauri hiyo, kwa lengo la kuwajengea uwezo na weredi katika utendaji kazi wao pamoja na kukumbushwa juu ya matumizi mbalimbali ya sheria zinazoongoza vijiji

Hata hivyo mafunzo yalilenga pia kujadili taarifa mbalimbali za makusanyo ya fedha  za ushuru na mapato mengine yanayokusanywa kupitia kwenye ngazi  za vijiji ambayo kwa namna moja au nyingine yanaweza kuchangia ukuaji  wa mapato kwa ngazi ya kijiji na Halmashauri kwa ujumla.

Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa zamani wa Halmashauri uliopo  Masasi Mjini

Kaimu mkurugenzi bwana Lyoba Magabe kwa niaba ya mkurugenzi  wa Halmashauri ya wilaya Masasi Bi Changwa  Mkwazu  alisema” halmashauri imeamua  kuandaa semina hii elekezi kwa wenyeviti wa vijiji ili kuwaleta karibu na wajiskie kuwa na wao ni sehemu ya menejimenti nan i watu muhimu katika kusimamia shughuli za maendeleo katika ngazi za vijiji, lakini pia kuwakumbusha katika kutekeleza wajibu na majukumu yao bila kuingilia ngazi nyingine za mamraka zilizopo kwenye kata zao”,

Bwana Magabe aliendelea kusema kuwa wengi wa wenye viti hao ni wapya hivyo baasi kupitia mafunzo haya yatawasaidia kutekeleza majukumu yao vema  kwa weredi na kujiamini pia kuwezesha kutoa huduma nzuri kwa wananchi wanao waongoza,

Sambamba na hilo Mwenyekiti wa Halamshauri ya wilaya ya Masasi Mh. Ibrahimu Issa Chiputula ambaye pia ni Diwani wa Kata ya  Mpeta alipokuwa akifungua  mafunzo hayo alikuwa na hili la kusema “Nina mpongeza sana  Mkurugenzi kwa kuona umuhimu wa kuandaa mafunzo haya ambayo yatawasaidia sana wenye viti wa vijiji katika kutambua sheria na taratibu zinazoongoza, vijiji hivyo kurahisisha utendaji kazi wao”.

 wenyeviti hao wa vijiji ameiyasa Halmashauri kupitia Mkurugenzi kuwa Mafunzo kama hayo ni muhimu sana kwao hivyo ameomba yawe yanafanyika mara kwa mara ili kuzidi kujengeana uwezo.




Wenye viti wa vijiji wakiwa wanafuatilia kwa umakini mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa kutoka kwa wawezeshaji pamoja na ufafanuzi mbalimbali uliokuwa ukitotelewa na wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya masasi siku hiyo ya semina elekezi.

Mratibu wa ICHF Bwana Peter Mushi akiwaeleza wenye viti wa vijiji kuungana na Halmashauri katika kuhimiza wananchi kujiunga na Bima ya Afya ichf iliyoboreshwa ambapo mwananchi anaweza kupata huduma za afya popote ndani ya Mkoa wa Mtwara kuanzia Zahanati, kituo cha afya, Hospitali za Wilaya na mkoa kwa shilingi 30,000/= kwa mwaka kwa idadi ya watu sita kwenye kaya moja.

Mratibu wa Tasaf ngazi ya Wilaya wa Halmashauri ya wilaya ya Masasi Bwana Thobias Mkude nae akitoa neno kwa wenye viti wa vijiji juu kuisaidia Halmashauri juu ya kuzitambua kaya masikini kweli kweli na kuacha tabia ya kuwapendekeza watu ambao wanajiweza, hata hivyo mratibu huyo aliwasihi wale wote ambao ni wanufaika na msaada huu wa tasaf kupitia kaya masikini kuhakikisha kuwa fedha wanayoipata wanaitumia vizuri kwa kubuni miradi mbalimbali ambayo itawaingizia kipato na hatimaye kuondokana na umasikini.

Mkuu wa Idara ya Mazingira Bi. Kulwa Maiga akitolea ufafanuzi juu ya mambo mbalimbali yanayohusu Mazingira mbele ya wenyeviti wa vijiji katika semina hiyo ya kuwajengea uwezo wenyeviti hao na kuwataka kuwa mabalozi wazuri wa kuhamasisha wananchi wanao waongoza katika vijiji vyao juu ya swala zima la utunzaji wa mazingira kwa ajili ya afya zetu na maendeleo yetu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa