• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WAWILI WAPOTEZA MAISHA KUTOKANA NA MLIPUKO WA UGONJWA WA KUHARISHA NA KUTAPIKA

Posted on: June 18th, 2024

Jumla ya Wagonjwa 47 Kati yao Wanaume 22, Wanawake 25 wamefikishwa katika vituo vya kutolea huduma za Afya kwa ajili ya kupata matibabu kutokana na uwepo wa mlipuko wa ugonjwa wa kuharisha na kutapika ambao umegundulika  kwenye kitongoji Cha Miesi, Kijiji Cha Mbangala Kata ya Lupaso halmashauri ya Wilaya ya  Masasi Mkoani Mtwara.

Hata hivyo Kati ya Wagonjwa hao 47, Watoto walio chini ya umri wa miaka 5 jumla ni ( 7) miaka 5 -15 jumla ni watano (5)  miaka 15-49 wapo 32 na miaka 50- kuendelea ni Watatu (3).

Aidha taarifa inaeleza kuwa Wagonjwa wawili Me na Ke tayari wamepoteza maisha kutokana na uwepo wa mlipuko huo wa ugonjwa wa kuharisha na kutapika.

Akisoma taarifa katika kikao cha dharura kilichoitishwa na  Kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya Masasi mapema Leo June 18,2024 Afisa Afya na Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Bw.Said Ame amesema kuwa mnamo tarehe 10/06/2024 Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji ilipokea taarifa kutoka kwa Mganga mfawidhi wa utimbe juu ya uwepo wa ugonjwa wa kuharisha na kutapika katika kijiji cha Mbangala, kitongoji Cha Miesi ambapo baada ya kupata taarifa hiyo timu ya dharura ya haraka (RRT) akiwemo na Afisa Afya mazingira, Daktari wa hospitali ya Halmashauri na mtaalamu Kutoka RUWASA walitembelea eneo la tukio katika Kijiji Cha Miesi na kuchukua sampo ya Maji yanayotumika (Mto Miesi) kwa ajili ya kufanyia vipimo vya Maabara.

Amesema pia tarehe 11/06/2024 katika kituo Cha Afya Chiungutwa walipokelewa Wagonjwa Watatu (3) wenye dalili za kuharisha na kutapika na hatmaye zikachukuliwa sampo kutoka kwa Wagonjwa na kupelekwa Maabara ya Ndanda kwa ajili ya kufanyiwa vipimo vya kimaabara na kubainika kuwa na vibrio cholerae.

Amesema kwa upande wa maiti iliyofariki kituo Cha Afya Chiungutwa ilifanyiwa vipimo vya haraka vya ugonjwa huo wa kuharisha na kutapika na kubainika uwepo wa vijidudu vya Vibrio cholerae.

Ameongeza pamoja na hayo kwamba zipo hatua mbalimbali ambazo zimechukuliwa Ili kudhibiti mlipuko huo ikiwemo kukutana na uongozi wa Kijiji na Kata kwa ajili ya kuelimisha na kuwakumbusha majukumu yao wakati wa mlipuko pamoja na kuwafahamisha uwepo wa Kambi ya matibabu ya Wagonjwa wa kuharisha na kutapika katika kitongoji Cha Miesi.

-Elimu juu ya Afya ya kujikinga dhidi ya Magonjwa ya mlipuko imetolewa kwenye mkutano wa Kijiji, maeneo yenye mkusanyiko,. maeneo huduma za vyakula na ngazi ya kaya katika Kijiji Cha Mbangala.

- Ugawaji wa vidonge 1580 vya water guard katika kaya 193 za Kijiji cha Miesi, kila kaya imepewa jumla ya vidonge viwili.

- Uhamasishaji wa Jamii juu ya ujenzi wa vyoo,ilani imetolewa kila kaya kuwa na choo ifikapo June 20/2014.

 -Kwa kushirikiana na RUWASA kiasi Cha maji lita 20,000 kimesambazwa Kijijini Miesi.

 -Kushiriki Shughuli za kutakasa maiti zote zilizohusishwa na ugonjwa wa kuharisha na kutapika ikiwemo na kusimamia maziko

-Kutembelea vituo vilivyopata Wagonjwa wa mlipuko kwa ajili ya kuelekeza na kuchukua tahadhari wakati wa mlipuko na taratibu zingine ikiwemo usambazaji na maelekezo ya matumizi ya dawa za utakasaji.

- Kufunga vilabu vya pombe za kienyeji kwa mujibu wa Sheria ndogo ya Afya na usafi wa mazingira ya Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.

-Kuelimisha Wananchi umuhimu wa kunawa mikono Maji tiririka kutumia vibuyu chirizi na kutembelea kaya zilizopata Wagonjwa wa mlipuko kwa ajili ya kutakasa eneo na vyombo alivyotumia mgonjwa.

Hata hivyo katika kuhitimisha Taarifa yake Afisa Afya na Mazingira ameelezea baadhi ya changamoto ambazo zinazikabili hatua ambazo zimechukuliwa katika kupambana na mlipuko huo ni kwamba bado wapo baadhi ya Wagonjwa kutoka Miesi kuendelea kupata matibabu utimbe licha ya kuanzishwa Kambi Miesi, kuhama kwa wakazi kutoka Miesi kwenda Tandahimba hivyo kupelekea ugonjwa kusambaa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya ulinzi na usalama ambaye ndiye Mkuu wa Wilaya ya Masasi mhe.lauteri Kanoni pamoja na kumuagiza  mkurugenzi aendelee Kutoa taarifa kwenye Vijiji na Kata zote juu ya uwepo wa mlipuko wa ugonjwa huo ili wananchi wapate taarifa na waweze kuchukua tahadhari namna ya kujikinga pia amelekeza uongozi wa Kijiji kuweka ulinzi getini ambao utahusika kuelekeza wanaotafuta matibabu utimbe kwanza waende kupata matibabu Kambini badala ya kwenda zahanati Moja kwa Moja

Pia ameendelea kuwasisitiza Wananchi wahakikishe ifikapo tarehe 20/6/2024 kila Nyumba inakuwa na choo bora na baada ya tarehe hiyo msako utafanyika wa vyoo kwa kila Nyumba.

Hata hivyo waliofariki ni Akili Issa Namwawa umri miaka 70 na Hadija Stamili Kitenge umri miaka 40.


Imeandaliwa na:

Winifrida Ndunguru

Afisa Habari MDC

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa