• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATOTO 35,720 KUSAJILIWA NA KUPATIWA VYETI VYA KUZALIWA BURE ,MASASI DC

Posted on: September 20th, 2017

Mpango wa usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wa umri wa miaka mitano katika Halamshauri ya Wilaya ya Masasi unatarajia kusajili na kutoa vyeti bure  kwa watoto 35,720 wanaoishi katika halmashauri hiyo  ndani ya siku kumi na mbili (12)  kuanzia tarehe 26 mwezi huu za kampeni ya usajili na utoaji wav yeti vya kuzaliwa kwa watoto hao.

Usajili huu wa vyeti vya watoto chini ya miaka mitano  utatolewa  katika ngazi ya kata na vituo vya kutolea huduma za afya kuanzia sasa  badala ya ofisi ya mkuu wa wilaya ili kupunguza  ghrama na usumbufu kwa wananchi kupata  huduma hiyo hiyo .

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa  mafunzo ya usajili wa watoto chini ya umri wa miaka 5 Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya masasi Chagwa M Mkwazu kwa watendaji wa kata wasimamizi wa vituo vya afya na waja leo katika ukumbi wa Migongo alieleza kuwa zoezi hilo ni muhimu sana hivyo  wawezeshwaji watapaswa kuwa makini sana wakati wa utekelezaji ili kufikia lengo lililowekwa katika kipindi cha kampeni.

 “Kuwasajili watoto hawa kutasaidia serikali katika ngazi mbalimbali kupanga mipango mbalimbali ya muda mfupi na muda mrefu kwa uhakika ikiwemo kujua  mahitaji  halisi ya madarasa, madawati,  na hudma zingine katika jamii kulingana na idadi ya watu hivyo utoaji wa takwimu zisizosahihi zitaathiri upangaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo kwa jamii”. Alisema mkwazu.

Mkwazu alieleza kuwa Cheti cha kuzaliwa ni haki na ni utambulisho wa kwanza wa mtoto na nyaraka ambayo hutumika kuthibitisha taarifa muhimu za mwananchi kwani inakuwa na taarifa muhimu ikiwemo  jina, majina ya wazazi wote wawili, mahali alipozaliwa na tarehe aliyozaliwa hivyo kujua umri wake.

Mkwazu alisema kuwa utekelezaji wa zoezi hilo kitaifa  utafanyika kwa muda wa  miezi mitatu hivyo ni lazima kuzingatia umakini wakati wa zoezi  kwa kuandikisha watoto kwa ufasaha ili mwisho wa siku tuwe na takwimu sahihi za watoto watakaokuwa wamesajiliwa na kupewa vyeti vya kuzaliwa kwa mujibu wa sheria na kanuni watakazoelekezwa maana taarifa hizo zitaingizwa kwenye mfumo ambao utatumia simu za mkononi.

Katika hotuba yake,   Mkwazu alisema kuwa zoezi la kusajili watoto sasa linakabidhiwa kwenye ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri na taarifa za watoto zitaanza kuchukuliwa katika ofisi za kata na vituo vya afya na zahanati ambapo maafisa watendaji na watoa huduma watawajibika kuwatafuta watoto walio chini ya miaka mitano ili wapatiwe vyeti vya kuzaliwa bure

Kwa upande wa mwakilishi wa  Ofisa usajili kutoka makao makuu (Rita ) mariam gwaja alisema zoezi la kusajili  na kutoa vyeti vya kuzaliwa linaendelea nchi nzima, elimu inaendelea kutolewa juu ya  umuhimu wa kuwa na cheti cha kuzaliwa, wananchi wengi wanaitikia sana hivyo naamini hata masasi zoezi litafanyika kwa mafanikio makubwa.

Kwa kipindi kirefu nchini Tanzania kazi ya utoaji wa cheti cha kuzaliwa imekuwa inafanywa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na udhamini (RITA) ambapo takwimu kwa mujibu wa sensa ya Watu na makazi ya mwaka 2012 watoto chini ya miaka mitano asilimia 13 tu wamesajiliwa nchi nzima na asilimia  9 kwa mkoa wa Mtwara, hali hii inaonyesha na kuashiria kuwa watoto wengi hawapo ndani ya mfumo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa