• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATENDAJI WA VIJIJI WAPYA NA MAAFISA UGANI MASASI WAPIGWA MSASA USIMAMIZI WA MIRADI YA TASAF

Posted on: June 21st, 2018

Watendaji wa vijiji na maafisa ugani  katika vijiji 97 na kata 30 vinavyotekeleza mpango wa kunusuru kaya masikini (TASAF)  Halmashauri ya Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara wametakiwa kuwajibika ipasavyo  katika kusimamia mradi huo ili kuwaondolea umasikini wananchi kama adhma ya serikali kwa kuhakikisha kila mlengwa anapata stahiki zake kadri ya muongozo.

Watendaji wa vijiji na maafisa ugani wakifuatilia mafunzo

Maelekezo hayo yametolewa kwa watendaji  na maafisa ugani hao  katika kikao kazi kilicholenga kuwajengea uelewa juu ya mpango  huo kutokana na watendaji wengi wa vijiji kuwa wapya katika utumishi wa umma, hivyo mafunzo hayo yatawapa fursa ya kuelewa wajibu wao katika utekelezaji na usimamizi wa mradi wa kunusuru kaya masikini katika maeneo yao ya kazi kama watendaji wakuu.

mwezeshaji wa mafunzo kwa watendaji na maafisa ugani kuhusu mpango wa kunusuru kaya masikini ndugu Antony Mhando akitoa mada

Akitoa maelekezo hayo kwa watumishi hao katika kikao kazi hicho Kaimu Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri hiyo ndugu Jeremiah Lubeleje ameeleza kuwa ili mpango huo ulete manufaa kwa wananchi watendaji ndio wasimamizi wakuu kwa kuhakikisha walengwa  wanaostahili wanapata fedha zao kwa mujibu wa miongozo.

Lubeleje amefafanua kuwa, takribani watendaji wa vijiji 80 ni waajiwa wapya ,hivyo kwa ugeni wao hawajui mpango ndio maana tumeamua kutoa mafunzo elekezi juu ya mpango kwa watendaji hawa kwani ndio watendaji wakuu kwenye maeneo yao katika kutekeleza mpango huu wa kunusuru kaya masikini.

washiriki wakifuatilia kwa makini mafunzo juu ya mapango wa kunusuru Kaya masikini

“Ni vema mkafahamu kuwa lengo la serikali ni kuziwezesha kaya masikini kuongeza kipato na kukuza uchumi kupitia ruzuku na vikundi vya kuweka akiba, hivyo ni vema mkasimamia vizuri walengwa ili fedha hizo wazitumie katika matumizi yanayofaa” alisema Lubereje.

Kwa upande wa maafisa ugani,  Lubeleje ameeleza kuwa wanapaswa kuhakikisha wanatoa usaidizi wa kitaalamu katika miradi inayoanzishwa na walengwa kupitia vikundi vya kuweka akiba na kukuza uchumi ikiwemo miradi ya kilimo na mifugo kwa kutoa usaidizi juu ya mbinu bora za kulima na kufuga lakini pia namna ya kukabiliana na magonjwa ili wazalishe kwa tija.

Mratibu wa TASAF halmashauri ya wilaya ya masasi  Thobias Mkude akisisitiza jambo wakati wa mafunzo kwa watendaji na maafisa ugani kuhusu mpango.

Kuhusu miradi ya ajira ya muda, Lubeleje( kaimu mkurugenzi) amesema watendaji wa vijiji wanapaswa kuelewa kuwa baada ya mradi kukamilika jukumu la kuhakikisha mradi unahudumiwa na kuendelezwa ni la kijiji na sio walengwa pekee, hivyo miradi kama ya upandaji miti inapaswa ihudumiwe na wananchi wote badala ya kuwaachia walengwa peke yao  baada ya muda wa utekelezaji wa mradi kuisha.

Kwa upande wake Mratibu wa mpango wa kunusuru kaya masikini ndugu Thobias Mkuse amesema kuwa, jumla ya vijiji 97 katika halmashauri ya wilaya ya masasi vinanufaika na mpango wa kunusuru kaya masikini ambapo jumla ya vikundi 718 vya kuweka akiba na kukuza uchumi vimeundwa ikiwa ni namna ya kuwafanya walengwa wawe na uwezo wa kukuza uchumi hata baada ya mradi kuisha.


mmoja wa washiriki akitoa hoja wakati wa mafunzo

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa