Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WATENDAJI WA KATA NA VIJIJI WATAKIWA KUCHAPA KAZI

Posted on: June 17th, 2017

Watendaji wa Vijiji na Kata wa Halamshauri ya Wilaya ya Masasi wametakiwa  kuchapa kazi kwa kuboresha usimamizi wa  shughuli zote katika maeneo yao ikiwemo  ukusanyaji wa mapato na usimamizi wa miradi  kwani wengi wao wanatekeleza kwa kasi ndogo sana hali ambayo inapelekea  wananchi kulalamikia serikali kwa kukosa huduma.

Hayo ameyasema leo Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi ndugu Jeremiah Lubeleje leo wakati  akiwasilisha mada kuhusiana na Mwongozo wa fedha za LGCDG na Usimamizi wa miradi ya maendeleo tarehe 17.06.2017 wilayani masasi kwenye mafunzo ya watendaji kata na vijiji ya kuwajengea uwezo yaliyoendeshwa na Halmashauri hiyo  baada ya kuona kuwa miradi mingi inayotekelezwa katika ngazi ya jamii haitekelezwa kwa wakati na kwa viwango stahiki.

“ni vema tubadilike tuwe watendaji wanaohudumia wananchi kwa kutumia nafasi zao vizuri ili kuwa na maendeleo katika maeneo yenu kwani serikali ya sasa inataka watumishi wafanye kazi kwa bidii akini pia kwa kazi kubwa” alisema Lubeleje.

Kuna baadhi ya vijiji Halmashauri imepeleka fedha za kutekeleza miradi tangu mwezi januari lakini mpaka saivi mradi haujaanza kutekelezwa, hali kama hii inaonesha mtendaji hutoshi kukaa kwenye nafasi hiyo maana moja  ya majukumu yako ni kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa wakati na kwa kiwango kinachokubalika kama kuna watendai bado wako hivyo ni vema wabadilike haraka sana.  

Lubeleje alisema, ruzuku ya Maendeleo isiyo na Masharti (LGCDG) ilianza mwaka 2004/2005 na ilisaidia sana kuziongezea Serikali za Mitaa uwezo katika utendaji kwa maeneo ya upangaji bajeti, usimamizi wa fedha na masuala ya manunuzi.

Alisema katika kipindi hicho, miradi mingi iliyotekelezwa katika sekta za afya, elimu, maji na kilimo lakini bado kulikuwa na changamoto za miradi mingi kuachwa viporo, vipaumbele vya nguvu za wananchi hazikuthaminiwa ipasavyo katika miradi hiyo na fedha zilizobajetiwa hazikuwa zinatolewa zote na kwa wakati na hivyo kusababisha kubaki na miradi mingi isiyotekelezwa.

Kwa sasa Serikali yetu ya awamu ya tano imefanya mapitio na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zilizojitokeza hapo awali kwa kutumia Mwongozo wa mwaka 2016 wenye malengo makuu ya Ruzuku ya Maendeleo isiyo na Masharti (LGCDG) iliyoboreshwa yenye makusudu kuwa jamii inapata huduma bora na  kwa wakati.

Afisa Mipango huyo aliwaeleza kuwa miradi inayotekelezwa na LGCDG inapaswa kuzingatia  kutoa huduma kwa jamii, Vipaumbele vya jamii vinaainishwa ipasavyo, Juhudi za jamii zitambuliwe, ziwezeshwe na kuungwa mkono ili kuifanya serikali iweze kutoa huduma kwa jamii, Mgawanyo wa fedha ufanyike kwa usawa, kuboresha usimamizi wa fedha na maeneo yenye huduma duni yawe ni yenye kunufaika kutokana na ruzuku ya fedha za LGCDG.

Bwana Lubeleje alisema kuwa msisitizo wa matumizi ya fedha hizo ni pamoja na ujenzi na ukarabati wa Miundombinu ya kilimo, maji safi na salama, elimu, afya, barabara na utawala bora kwa lengo la kutatua kero za wananchi wa ngazi ya chini.

Aidha aliwaeleza Watendaji wa Kata na Vijiji kuwa mtawanyo wa fedha za LGCDG uzingatie alimia themanini (80%) ya fedha hizo zitekeleze miradi ya maendeleo, asilimia kumi (10%)  zielekezwe kwenye kujenga uwezo na asilimia kumi (10%) zitumike katika usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo, “Tuchape Kazi, Tuache kufanya kazi kwa Mazoea”. Alisisitiza.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • PPRA YATOA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA NeST NA SHERIA YA UNUNUZI WA UMMA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI

    March 12, 2025
  • KAMATI YA SIASA YA CCM WILAYA YA MASASI YAFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    March 06, 2025
  • MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI YANATOA FURSA KILA MMOJA KUJUA HAKI YAKE YA MSINGI: MHE MAJALIWA

    March 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa