• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

WANAWAKE WATAKIWA KUWA NA MTAZAMO CHANYA KUFIKIA USAWA WA KIJINSIA

Posted on: March 9th, 2019

Ili kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu ya Maadhimisho ya siku ya wanawake kwa mwaka 2019 isemayo “Badili fikra, kufikia usawa wa kijinsia kwa maendeleo endelevu” Wanawake wametakiwa kuwa na mtazamo chanya kufikia maendeleo  katika Nyanja mbalimbali ikiwemo kiuchumi, kisiasa, kijamii pamoja na  kuwa mfano bora kwa malezi ya watoto ili kuwa na jamii yenye maadili mema.

Kauli hiyo ilitolewa na Mgeni rasmi  Bi Emmy Rajab Ng’oura ambaye ni Afisa  Tarafa  wa tarafa ya Lulindi , Halmashauri ya Wilaya ya masasi , katika sherehe za maadhimisho ya siku ya wanawake duniani , yaliyofanyika jana machi , 8 katika  viwanja vya shule ya sekondari Namombwe kata ya Mchaulu.

Mgeni rasmi  Bi Emmy Rajab Ng’oura akishiri zoezi la ufyatuaji wa tofali kwa ajili a ujenzi wa Bweni la  wasichana katika shule ya sekondari Nambombwe

Akihutubia wananchi wakati wa sherehe hizo, Bi Ng’oura amewataka wanawake wa halmashauri hiyo, kubadili fikra hasi katika kufikia maendeleo, badala yake  watumie fursa zinazotolewa na serikali na wadau mbalimbali ikiwemo utoaji wa mikopo isiyo na riba,  elimu ya masuala ya usawa wa kijinsia  na vitambulisho vya wajasiliamali  ili kujikwamua wenyewe katika sekta zote  na kutekeleza majukumu yao bila vikwazo vinavyotokana na jinsia.

Bi Ng’oura alieleza kuwa  “Moja ya fursa ambayo serikali imeitoa ni kutoa vitambulisho vya wajasiliamali wadogo kwa bei ya shiringi 20,000 tu, nawasihi wanawake wanaojihusisha na ujasiliamali kuchangamukia fursa hii ili muweze kufanya biashara zenu bila usumbufu wa kutoa tozo zingine zozote”

Aidha  alisema kuwa , kumekuwa na matukio mbalimbali ya ukatili kwa watoto, wananwake inawapasa kuwa mstari wa mbele kupinga na kuwafichua watu wanaofanya ukatili wa kijinsia na wale waliofanyiwa ukatili kama ubakaji na ndoa za utotoni, ili kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto na sio kuungana nao kuwaficha wahalifu hao.

Wanawake wakicheza wakati wa sherehe yao

" Ni vema kutambua, wanawake ndio msingi wa mabadiliko kwenye jamii, kama wanawake tutabadili fikra zetu juu ya mambo mbalimbali  kuanzia ndani ya familia, jamii zetu  pia zitabadika, hakutakuwa na ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto, watoto wote watapata elimu sawa bila kujali jinsia na tutatokomeza ndoa na mimba za utotoni.

Ni jambo la kujivunia kuona Kadri ya siku zinavyoenda wanawake wanashika nyazifa tofauti katika sekta mbalimbali kuanzia ngazi ya kijiji hadi taifa, ambapo kwa Halmashauri hiyo jumla ya wananwake 104 wanatumikia nafasi mbalimbali za uongozi “ haya ni mafanikio makubwa tunapaswa kujipongeza” alieleza Bi Ng’oura

Mgeni rasmi  Bi Emmy Rajab Ng’oura akimvalisha kitambulisho cha ujasiliamali mmoja ya wanawake katika siku ya maadhimisho ya  wanawake duniani

Akisoma  taarifa ya utekelezaji  mbele ya mgeni rasmi, Afisa Maendeleo ya Jamii na Jinsia, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Neema Joseph amesema kuwa, Halmashauri hiyo imefanya maadhimisho hayo, huku ikiwa na mafanikio makubwa katika kuwawezesha wanawake  na vijana kiuchumi,  ambapo jumla vikundi 8,vimepatiwa mikopo ya bila riba, yenye thamani ya shilingi milioni 75, fedha zinazotokana na asilimia 10 za mapato ya ndani kwa mwaka huu wa fedha 2018/2019.

 

Afisa Maendeleo ya Jamii na Jinsia, Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Neema Joseph akisoma taarifa ya utekelezaji

Pamoja na kuadhimisha maadhimisho yaho kihalmashauri katika kata ya mchaulu, afisa maendeleo ya jamii alieleza kuwa sherehe kama hizo pia zinafanywa katika kata zingine kama Mwena, ndanda, chigugu na Nangoo, lengo ikiwa ni kuhasisha wanawake katika maeneo yote kutambua haki na wajibu katika kufikia usawa wa kijinsia ambapo wameshiriki katika shunguli mbalimbali za maendeleo ikiwemo ujenzi wa miradi, kufanya usafi , kusaidia wagonjwa na kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu

Maadhimisho hayo yenye kauli mbiu ya "Badili Fikra Kufikia Usawa wa Kijinsia kwa Maendeleo Endelevu" yamekwenda sambamba na upimaji wa afya kwa magonjwa yanayoambukizwa na yasiyoambukizwa bure, burudani mbalimbali, mashindano ya mchezo wa mpira wa miguu kwa wananwake na  mpira wa pete.  

Mgeni rasmi  Bi Emmy Rajab Ng’oura akikabidhi vifaa vya shule kwa wanafunzi waishio katika mazingira magumu vilivyotolewa na Chama cha walimu (CWT) na shirika la SWISSAID

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa