• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

USHIRIKIANO KATI YA MASASI NA ENZKREIS UJERUMANI WABORESHA SEKTA YA AFYA KWA KUWEKA UMEME WA SOLA ZAHANATI ZOTE

Posted on: September 6th, 2017

Tatizo la umeme katika vituo vyote  vya kutolea huduma za afya vilivyopo maeneo ambayo hayana umeme na nyumba za watumishi wa idara ya afya katika Halmashauri ya wilaya na Mji Masasi  litakuwa historia baada ya Halmashauri hizo kwa kushirikian na halmashauri rafiki ya Enzkreis ya nchini ujerumani kuweka umeme jua  katika  vituo hivyo lengo ikiwa ni kuboresha utoaji wa huduma za afya nyakati zote  yaani usiku na mchana kwa ufanisi .

Hayo yamezungumzwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Changwa M.  Mkwazu baada ya kuwapokea wageni kutoka halmashauri  rafiki ya Enzkreis  iliyopo ujerumani wakiwa na lengo la kukagua miradi ambayo inatekelezwa kwa ushirikiano kati ya halmashauri za masasi na ya enzkreis.

Mkwazu alisema katika ushirikiano huo wamekubaliana kutekeleza miradi ya utunzaji wa mazingira ambapo kuna miradi ya uwekaji umeme jua kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya na nyumba za watumishi ili kuboresha utoaji wa huduma za afya na utunza mazingira pamoja na matumizi ya biogas ambayo inatumia kinyesi cha wanyama kutengeneza nishati  umeme kwa ajili ya mwanga, kupikia na matumizi mengine.

Pamoja na kwamba mradi huo utasaidia kupunguza uharibifu wa mazingira lakini pia kwa halmashauri zetu tutakuwa tumetatua tatizo kubwa la umeme kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ambapo huduma hizi zitatolewa wakati wote yaani yakati za usiku na mchana tofauti na sasa ambapo baadhi ya vituo vya kutolea huduma za afya havina umeme, hivyo uwekaji wa umeme jua kwenye zahanati zetu ni utasaidia watumishi wa afya kuwahudumia  wagonjwa wakati wote.

Kwa upande wake mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Gimbana Ntavyo alisema kuwa anaishukuru halmashauri ya enzkreis  kwa misaada wa vitu mbalimbali kwa ajili ya kuboresha huduma za afya ambapo wameweza kuweka umeme jua eneo chumba cha maabara na chumba cha watoto njiti, ujenzi wa chumba cha uasuaji,  uletaji wa vifaa vifaa na uboreshaji wa huduma za afya katika hospitali.

Aidha kutokana na ushirikiano baadhi ya wanamasasi wamehamasika kutumia m=nishatinishati ya Biogas kwa matumizi ya mwanga na  kupikia kutokana urahisi wa gharama za kupata nishati hiyo ukilinganisha na umeme wa viwandani.

Kwa upande wake ndugu Mwita ambaye ametengeneza biogas nyumbani kwakwe kama njia ya kupata nishati ya umeme, na ameeleza kuwa umeme anaopata kupitia njia hiyo ni mwingi na hauna gharama kwani kinachohitajika nikuwa na mifugo inayoweza kuzalisha kinyesi kwaajili ya kukoroga tu.

“Napenda kuwahamasisha wananchi wa masasi na shemu nyingine kutengeneza mtambo wa biogas ili waweze kupata nishati ya umeme  ya uhakika na kwa bei nafuu” alisema Mwita

Uwekaji wa umeme jua katika zahanati umeanza na utoaji wa mafunzo kwa vijana wa vijijini ili waweze kufanya kazi za uwekaji na matengenezo ya vifaa pale inapotokea tatizo kwa mda wa miaka mitatu lakini wakati huohuo wanaendelea kufanya shughuli za ufundi kwa watu walio nje ya mradi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA YAANZA VIZURI MASASI DC

    June 17, 2025
  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa