• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SHILINGI BILION 7.5 KUGHARIMU UJENZI WA HOSPITALI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI

Posted on: January 16th, 2019

WANANCHI wa Kijiji cha Mbuyuni, Kata ya Mbuyuni Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara wametoa jumla ya hekari 200 za mashamba yao bila fidia yoyote ambapo hekari 98 kati ya hizo wametoa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya halmashauri ya wilaya ya Masasi na hekari 102 kwa ajili ya shughuli nyingine za maendeleo.

Hayo yalibainika wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Gelasius Byakanwa jana tarehe 15/01/2019 aliyoifanya kwa ajili ya kuzindua ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya wilaya inayojengwa katika kijiji cha Mbuyuni kata ya Mbuyuni ambapo ujenzi huo tayari umeshaanza kutekelezwa kwa hatua za awali.

Akisoma taarifa ya ujenzi huo wa hospitali ya Halmashauri ya wilaya mbele ya Mkuu wa Mkoa, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, Dkt. Charles G. Mkombe alisema mradi huo wa ujenzi wa hospitali ya wilaya utagharimu jumla ya Shilingi bilioni 7.5 hadi kukamilika na kuwa na jumla ya vyumba 22 vya kutolea huduma.

Dkt.Mkombe alisema serikali imeshatoa jumla ya kiasi cha fedha Shilingi bilioni 1.5 kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza Halmashauri imepokea Shilingi Milioni 500 mwezi Novemba 2018 na mwezi disemba 2018 Halmashauri ilipokea Shilingi bilioni 1.

“Baada ya kupata kibali kutoka Tamisemi cha kuturuhusu kuanza ujenzi na kwamba jengo la kwanza litakuwa la utawala, jengo la pili ni la wagonjwa wa nje, stoo ya dawa, jengo la maabara, jengo la vipimo vya mionzi, na jengo la wadi ya wazazi,” alisema Dkt.Mkombe

Alisema hadi sasa tayari jumla ya fedha Sh.173 milioni zimeshatumika kwa ajili ya shughuli mbalimbali za ujenzi ambazo zimeshaanza kutekelezwa ikiwemo ununuzi wa mchanga, mawe, kokoto, saruji mifuko, nondo na vifaa vingine mbalimbali, aidha wananchi wameendelea kushiriki ujenzi huo kwa asilimia 100.

Awali akizungumza na wananchi hao kwenye eneo hilo la ujenzi wa hospitali, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa aliwapongeza wananchi hao ambao wameamua kujitolea kutoa eneo la hekari 98 ili serikali iweze kujenga hospitali hiyo ya wilaya na kwamba kitendo kilichofanywa na wananchi hao ni cha kizalendo.

Alisema, kitendo cha wananchi kuamua kushiriki ujenzi huo kwa asilimia 100 ni faraja kwake na serikali kwa ujumla. Hivyo serikali itaendelea kuwapatia huduma zote za msingi kwa vile maamuzi yao ni taswira nzuri na kwamba iwapo wananchi wakihamasishwa wanaweza kufanya mambo ya maendeleo bila kushurutishwa.

Wananchi wameipongeza serikali kwa uamuzi wa kutoa fedha kwa ajili ya kujenga hospitali ya halmashauri ya wilaya, na katika kuiunga mkono serikali yao wameona ni bora wao kama wananchi wajitolee kutoa eneo ambalo awali lilikuwa ni mashamba yao ya kilimo ili serikali iendelee na mchakato wake wa kujenga hospitali hiyo kwani maendeleo ni kwa ajili ya wananchi wote.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mhe. Juma Satmah amebeba tofali alilofyatua katika uzinduzi wa ujenzi wahospitali ya Halmashauri tarehe 15/01/2019 katika kijiji cha Mbuyuni.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mhe. Juma Satmah akiwa amebeba tofali alilolifyatua katika uzinduzi wa ujenzi wa hospitali ya Halmashauri, uliofanyika katika kijiji cha Mbuyuni tarehe 15/01/2019.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa