• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UFUNGAJI WA UMEME JUA (SOLAR) KATIKA ZAHANATI 27 WABORESHA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA MASASI

Posted on: August 14th, 2018

Mwakilishi wa Mkuu wa  Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara Mhe Fikiri Lukanga ameishukuru Halmashauri ya Enzkreis ya nchini ujerumani kwa msaada wao wa kuweka mifumo ya umeme Jua katika Zahanati 27 na nyumba za watumishi wa afya 51 lengo ikiwa ni kuboresha  utoaji wa huduma za afya kwa wananchi hasa kwa akina mama wajawazito kwa kuwa na umeme wa uhakika muda.

Mwakilishi wa Mkuu wa  Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara Mhe Fikiri Lukanga (mwenye shati jeusi) akizindua mfano wa sola katika tamasha la kuonesha teknolojia ya umeme jua katika kijiji cha Mijelejele wilayani masasi tarehe 13.08.2018

Lukanga ametoa shukrani hizo wakati wa tamasha la siku ya umeme jua lililofanyika katika kata ya Mijelejele wilayani humo liliolenga kuhamasisha wananchi juu ya kuongeza matumizi ya nishati ambayo ni rafiki wa mazingira na kusema kuwa anaipongeza wakala ya nishati Jadidifu Tanzania (TAREA)  kwa juhudi wanazozifanya kuhakikisha matumizi ya nishati mbadala hasa umeme wa jua yanaongezeka.

Wananchi wa kijiji cha mijelejele wakifuatilia kwa makini matumizi ya vifaa vya  umeme jua katika tamasha la kuonesha teknolojia ya umeme jua katika kijiji cha Mijelejele wilayani masasi tarehe 13.08.2018

Aidha Lukanga alifafanua kuwa nishati ya umeme ni kitu muhimu sana katika ustawi wa jamii kiuchumi na kijamii kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla hivyo uwepo wa umeme wa wa uhakika ni uhakika wa maendeleo.

Marafiki kutoka Halmashauri ya Enzkreis  Ujerumani wakisalimia wananchi kwenye tamasha la kuonesha teknolojia ya umeme jua katika kijiji cha Mijelejele 

 “Kila mtu ni shaidi kadhia kubwa zilizokuwa zinawapata akina mama wajawazito, watoto, wazee na wagonjwa kwa ujumla kutokana na kukosekana na nishati mbadala ya umeme katika zahanati zetu, hali hii inapelekea wauguzi wetu kutumia tochi za simu, vibatali na taa za chemli katika kutoa huduma nyakati za usiku”  alieleza Satmah.

Fundi wa mfumo wa Umeme Jua akitoa maelekezo ya matumizi ya vifaa vya umeme huo katika tamasha la kuonesha teknolojia ya umeme jua katika kijiji cha Mijelejele wilayani masasi 

Nae mwenyekiti wa Halmashauri  ya wilaya ya Masasi mhe Juma Satmah alieleza kuwa halmashauri za wilaya ya masasi Zinufaika sana na urafiki huo kwani pamoja na kuweka mifumo ya umeme jua pia wamekuwa wakifanya ziara za mafunzo kwa viongozi na wanafunzi lengo ikiwa ni kubadilishana mawazo lakini pia bado kuna mipango ya kufanya biashara pamoja ambapo watunaweza kupeleka bidhaa za masasi Ujerumani.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi mhe Juma Satmah akiongea wakati wa tamasha la kuonesha teknolojia ya umeme jua katika kijiji cha Mijelejele

“hii ni fursa adhimu sana kwa wanamasasi tunajivunia ushirikiano huu kati ya Masasi na Enzkreis ya Ujerumani kwani manufaa yake yananufaisha wananchi kwa ujumla” alisema Satmah

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Changwa Mkwazu amesema kuwa kupitia mradi huu wa ufungaji wa mifumo ya umeme jua kwenye zahanati 27 hali ya utoaji wa huduma umeimarika sana ambapo wananchi wanapat huduma muda wote lakini pia wataalamu wa afya wanakaa nyumba ambazo zina umeme hali ambayo inawafanya wajione wako kwenye mazingira mazingira mazuri ya kufanyia kazi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi  Changwa Mkwazu akitoa neno  kwa wananchi katika tamasha la kuonesha teknolojia ya umeme jua katika kijiji cha Mijelejele 

Wakiongea kwa niaba ya wananchi wa masasi, wananchi wa mijelejele wameishukuru serikali kufanya tamasha hilo la matumizi ya nishati ya umeme jua kwani umeme nihuduma muhimu katika kufikia maendeleo ikiwemo ya afya , kiuchumi na kijamii kwa ujumla.

Mratibu waUshirikiano kati ya Masasi na Halmashauri ya Enzkreis Ujerumani Jeremiah Lubeleje  akitoa ufafanuzi wa ushirikiano huo katika tamasha la kuonesha teknolojia ya umeme jua katika kijiji cha Mijelejele na kueleza kuwa kupitia Ushirikiano Huo zahanati 27 na nyumba 51 za watumishi wa afya zimefungwa mfumo wa umeme jua. aidha wanampango wa kufanya shughuli zingine za kimaendeleo.

Kwa upande wa Mwakilishi wa wakala ya nishati Jadidifu Tanzania (TAREA)  Emanuela Laswahi alisema kuwa TAREA iko tayari kuhamasisha  wananchi kutambua umuhimu wa kutumia umeme Jua na Nishati nyingine Jadidifu kwa lengo la kulinda mazingira,kuinua uchumi na kuboresha huduma za jamii kwa ujumla, hivyo “tunasisitiza wananchi waongeze kazi ya utumiaji wa nishati Jadidifu maana ni rafiki wa mazingira”


Naibu Katibu Mkuu wa TAREA bibi Emanuela Laswahi  akieleza jambo kwa wananchi wa Mijelejele

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa