• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

UANZISHWAJI WA BARAZA LA BIASHARA WILAYA YA MASASI

Posted on: May 26th, 2017

Na EKONI, Edwin Frank

Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mhe. Seleman Mzee amezindua Baraza la Biashara la Wilaya ya Masasi mwishoni mwa mwezi Mei 2017 lililojumuisha wajumbe kutoka sekta za umma na sekta binafsi na  yeye akiwa kama Mwenyekiti wa Baraza hilo kama chombo cha kisheria kusimamia masuala ya biashara wilayani humo.

Akizungumza kwenye kikao cha uzinduzi wa baraza hilo mwenyekiti huyo alieleza kuwa uanzishwaji wa baraza hilo ni wa kisheria kupita  waraka wa Rais Na.1 wa mwaka 2001 likiwa na lengo la kuunda jukwaa la majadiliano kati ya Sekta za Umma na Binafsi ili kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji.

Akiainisha majukumu ya baraza hilo Mkuu wa wilaya alisema kuwa baraza lina wajibu wa kuhamasisha Wafanyabiashara wengi kujiunga na TCCIA ili kuboresha huduma kwa wananchi pamoja na kuwa karibu na wafanyabiashara na wakulima ili kujua kero zao na kuwataka walipe kodi kwa maendeleo ya Taifa.

Aidha Mkuu wa Wilaya   alitumia nafasi hiyo kutoa rai kwa wajumbe wa baraza hilo kuwa wabunifu kwa kubuni na kuboresha huduma za miundombinu zinazoweza kukaribisha wawekezaji kuja kuwekeza katika maeneo ya wilaya ya Masasi.

Aidha  Mkuu wa Wilaya alimelipongeza shirika la Mamlaka ya Maji Masasi Nachingwea (MANAWASA) kwa kutoa huduma bora ya maji kwa wateja wake, aliwasihi kusambaza maji katika maeneo ambayo hayajafikiwa na huduma hiyo ili wananchi wengi zaidi waweze kunufaika na mradi huo.

Kutokana na Miundombinu ya barabara ya  masasi kutokuwa ya  uhakika, Mkuu wa Wilaya  alisema kuna haja ya baraza hilo kuona namna ya kuboresha miundombinu ya barabara ili kupunguza gharama za uzalishaji.

Kuhusu suala la umeme amewapongeza wananchi wa Masasi kwa utulivu wao licha ya kero nyingi zilizopo zinazohusiana na umeme, aliliomba shirika la Tanesco tawi la masasi kutumia fursa hiyo kuwasiliana na ngazi za juu ili kuona namana ya  kuondoa tatizo la umeme ili kuwavutia wawekezaji kwani kukosekana kwa umeme wa uhakika kunaweza kukimbiza wawekezaji na hata wageni.

Suala la masoko ni eneo linalopaswa kuangaliwa na baraza hilo kwani kuna mazao mengi hayanunuliwi na yanaharibika kutokana na kukosa soko, alisema kuna haja ya kutoa elimu ya biashara kwa wakulima wetu ili waweze kunufaika na kilimo.

Aidha aipongeza shirika la Mapato Tanzania( TRA) Wilaya ya Masasi kwa kasi nzuri ya ukusanyaji wa mapato ambapo alisema kwa mujibu wa taarifa alizonazo Masasi ipo zaidi ya asilimia mia moja (100%) ya ukusanyaji wa mapato na  aliwasihi wajumbe wa baraza hilo kuendelea kuhamasisha jamii ili walipe kodi  kwa wakati.

Kwa upande wake Katibu wa TCCIA Mkoa wa Mtwara ameeleza majukumu ya baraza la biashara katika ngazi ya mkoa na wilaya ni pamoja na kutengeneza mazingira bora ya kufanya biashara na kuwekeza, kuibua fursa za uwekezaji na  kuzindua fursa hizo kwa kupitia makongamano ya uwekezaji pamoja na kuandaa midahalo mahususi.

Katibu huyo alielezea maeneo sita ya uboreshaji wa mazingira ya biashara katika Big Result Now (BNR) kuwa ni pamoja na kuangalia upya mfumo wa kisheria na kitaasisi, upatikanaji wa ardhi na uhakika wa umilikishaji, usimamizi na uratibu wa shughuli za biashara, utitiri wa kodi, tozo na ada, kuzuia na kupambana na rushwa, sheria na stadi za kazi na usimamizi wa mikataba na sheria za kazi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa