• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TUNZENI MIUNDO MBINU YA SHULE HII YA SEKONDARI YA MPETA: NYENGEDI

Posted on: January 8th, 2025


Kamati ya Siasa (CCM) Mkoa wa Mtwara leo tarehe 08/01/2025 imefanya ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama hicho  (CCM) kwa kutembelea miradi mbalimbali ambayo inatekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.


Ziara hiyo ambayo ni ya siku moja katika Halmashauri hiyo awali imetembelea na kukagua ujenzi wa vyumba 24 vya Madarasa na matundu 14 ya Vyoo katika Shule ya Sekondari Mpeta ambayo inatekelezwa kwa njia ya Force account ambapo hadi sasa tayari ujenzi huo umekamilika na Shughuli iliyobaki ni ukamilishaji wa viti na meza 960.


Akisoma taarifa fupi ya ujenzi wa mradi huo mbele ya Kamati hiyo ya Siasa Mkoa, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mpeta Mwalimu Rajab Bakari Nampoto amesema Shule ya Sekondari Mpeta ilipokea shilingi 594,000,000.00 mnamo tarehe 30/03/2024 kutoka Serikali kuu kupitia fedha za ruzuku ya miradi ya Maendeleo kwa ajili ya ujenzi wa vyumba 24 vya Madarasa na matundu 14 ya Vyoo, ambapo mradi ulianza kutekelezwa tarehe 25/04/2024 na ulitakiwa kukamilika tarehe 19/07/2024.

"Mradi umepitia changamoto ya ukosefu wa Maji na mbao kwa ajili ya kukamilisha viti na meza za wanafunzi, Lakini kwa kushirikiana na Viongozi pamoja na Wataalamu mbalimbali kutoka Halmashauri na TFS wameendelea kushughulikia utatuzi wa mbao kwa ajili ya viti na meza" alisema mwalimu Nampoto


Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mtwara Ndg.Said Nyengedi amesema anamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Taifa Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwa na mapenzi makubwa na Watanzania na hasa Wananchi wa Mkoa wa Mtwara kwa Kutoa fedha nyingi ambazo zimewezesha kujengwa kwa mradi huo.

" Fedha alizotoa kwenye mradi huu ni nyingi sana, haya ni mapenzi kwetu,.vijana wetu wanakuja kusoma kwenye mazingira mazuri sana ambayo sisi wengine hatukusoma kwenye mazingira kama haya, hatuna budi kukiunga mkono Chama cha Mapinduzi, kumuunga mkono mhe.Rais wetu, Lakini tuna kila sababu ya kukiunga Chama chetu Cha Mapinduzi kwa mambo makubwa yanayofanyika katika nchi Lakini katika mkoa wetu na moja wapo ni hili ".

"Mradi huu utekelezaji wake kwakwelii tumefurahishwa na tumeupokea kwa mikono miwili hivyo niwaombe muitunze Miundo mbinu ya shule hii, ni ya kwenu Wananchi wa mpeta, Serikali imewajengea na nyinyi sasa Katika kuitunza miundo mbinu hii mnatakiwa kuhakikisha mnapanda miti.

Nao baadhi ya wananchi waliojitokeza katika mapokezi kwa Kamati hiyo kwenye mradi huo wa vyumba 24 vya Madarasa na matundu 14 ya Vyoo katika Shule ya Sekondari Mpeta wameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kwa kutoa fedha za kutekeleza mradi huo ambao una tija kubwa kwao.

Shule ya Sekondari Mpeta ilisajiliwa rasmi tarehe 17/11/2022 ikiwa na namba ya usajili S.5936, ina Jumla ya wanafunzi 467 ambao wasichana ni 242, wavulana ni 225 kati Yao wanafunzi wa kidato cha,I_III ni 222 na kidato cha IV - VI ni 245.

08/01/2024

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa