• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TUNAISHUKURU SERIKALI KWA KUTUPATIA FEDHA KIASI CHA SH.67,300,000.00 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA MRADI WA UJENZI WA VYUMBA 2 VYA MADARASA NA MATUNDU 6 YA VYOO VYA WANAFUNZI WA AWALI:CHIKUKWE

Posted on: January 10th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Masasi imeendelea kumshukuru mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia fedha kiasi cha shilingi milioni 67,300,000.00 kwa ajili ya kutekeleza mradi wa ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa na matundu 6 ya Vyoo vya wanafunzi wa awali katika Shule ya msingi Chikukwe.

Kwa mujibu wa taarifa ya ujenzi wa mradi huo iliyosomwa na mwalimu mkuu wa shule ya msingi Chikukwe Eliomega Rosiaeli Akyoo mbele ya Kamati ya Siasa(CCM)  mkoa ambayo ilifanya ziara hivi karibuni ya kutembelea miradi mbalimbali inayotekekezwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya Masasi,  amesema kwamba mnamo tarehe 18/06/2024 shule ya msingi Chikukwe ilipokea fedha kiasi cha shilingi 67,300,000.00 ikiwa shilingi milioni 66,300,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa miundo mbinu ya wanafunzi wa awali na kiasi cha shilingi milioni 1,000,000.00 kwa ajili ya Usimamizi wa miradi ngazi ya shule kupitia fedha za programu ya BOOST.

"Mradi huu ulitakiwa kutekelezwa ndani ya siku 90 ila kwakuwa wakati fedha hizi zinaingizwa ilikuwa ni kipindi cha mwisho wa mwaka wa Serikali hivyo fedha hizi zilianza kutumika Kama bakaa ya fedha za mwaka 2023/2024, kwenye bajeti ya mwaka 2024/2025 hivyo utekelezaji wa mradi huu ulianza tarehe 15/08/2024 na ulitakiwa kukamilika tarehe 15/11/2024 hivyo mpaka sasa kiasi cha shilingi 57,637,376.00 kimetumika na kiasi kilichobaki ni shilingi 8,662,624.00 na kinaendelea kutumika." alisema mwalimu Akyoo

Amesema mradi huo ambao unatekelezwa kwa njia ya force account, kwasasa mradi upo katika hatua ya umaliziaji, na kazi inayoendelea ni kufanya skimming na upakaji wa rangi.

Ameongeza kuwa katika utekelezaji wa mradi huo umepitia changamoto ya mfumo wa manunuzi wa NeST kwani zabuni mbalimbali za vifaa zilikuwa zinatangazwa na kurudiwa zaidi ya mara moja, Lakini upatikanaji wa wazabuni ulikuwa mgumu na ikizingatiwa muda wa utekelezaji wa mradi huo ulikuwa unapotea hivyo Halmashauri ililazimika kufanya manunuzi kwa njia ya Quatation ili kukamilisha mradi.

Ndg.Said Nyengedi ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mtwara akizungumza Kwa niaba ya Kamati hiyo amesema kwa pamoja wanaishukuru serikali ya awamu ya sita ya chama cha Mapinduzi inayoongozwa na Rais Dokta Samia Suluhu Hassan kwasababu haikumuacha mtu yeyote na hii si hapo tu Chikukwe bali ni katika maeneo mengi maendeleo yanaonekana ili hata mtoto mdogo mzazi wake asipate shida yakuacha kwenda katika Shughuli zingine bali wawapeleke shule ili wapate elimu, na hilo ni jambo la kujivunia sana.

" Na hii niwaombe wazazi muwalete watoto shule, wakati mwingine tunasema watoto wa siku hizi mmomonyoko wa maadili, lakini kumbe mmomonyoko huu wa maadili unaanzia kwetu sisi wazazi, ukimpeleka mtoto maeneo haya atakuwa analelewa katika mazingira ya shule na atakuwa na nafasi ya kujifunza tabia njema , na hakuna kitu muhimu cha kumrithisha mtoto zaidi ya elimu ambayo itamsaidia katika maisha yake, niwaombe sana wananchi wa Chikukwe mliopo hapa muwe mabalozi kwa wananchi wengine msikubali watoto wenu wabaki majumbani bali waje wapate elimu hapa tena katika mazingira mazuri kabisa "..alisisitiza Nyengedi

Shule ya msingi Chikukwe ina jumla ya wanafunzi 747 ambapo wavulana ni 370 na wasichana 377.

10/01/2025

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa