• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Tume ya Taifa ya uchaguzi yasogeza mbele Zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura

Posted on: June 22nd, 2024

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetangaza kusogezwa mbele kwa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura hadi tarehe 20 Julai, 2024 badala ya tarehe 01 Julai, 2024 iliyopangwa hapo awali.


Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Kigoma leo tarehe 22 Julai, 2024, Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji (Rufaa) Jacobs Mwambegele amesema kwamba uzinduzi wa zoezi hilo utafanyika siku hiyo ya Jumamosi tarehe 20 Julai, 2024 mkoani Kigoma ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB).


Mhe. Mwambegele ameeleza kwamba uamuzi huo wa Tume umetokana na kuzingatiwa kwa maoni ya wadau walioyatoa wakati wa mikutano iliyofanyika Jijini Dar es Salaam na Mkoani Kigoma.


“Tume imezingatia maoni na ushauri wa wadau. Hivyo, zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura litaanza tarehe 20 hadi 26 Julai, 2024 badala ya tarehe 01 hadi 07 Julai, 2024, mkoani Kigoma na uzinduzi utafanyika siku hiyo ya tarehe 20 Julai, 2024 mkoani Kigoma ambapo Mgeni Rasmi atakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb),” amesema.


Akizungumzia maoni hayo ya wadau, Mhe. Mwambegele amesema Tume imefanya mikutano tisa ya wadau ngazi ya Taifa mkoani Dar es Salaam kati ya tarehe 07 hadi 15 Juni, 2024 na mkutano mmoja wa wadau ngazi ya mkoa kwa mkoa wa Kigoma uliofanyika tarehe 19 Juni 2024.


Amewataja wadau waliokutana na Tume kuwa ni pamoja na Viongozi wa Vyama vya Siasa, Viongozi wa Dini, Wawakilishi wa Asasi za Kiraia, Wahariri wa Vyombo vya habari, Waandishi wa habari, Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri, Wawakilishi wa Makundi mbalimbali ya Vijana, Watu wenye ulemavu, wanawake na Wazee wa Kimila.


“Vyama vya siasa vilitoa maoni na ushauri wa kupatiwa muda wa kutosha kwa ajili ya kuwapata mawakala wa uandikishaji ili mawakala hao waweze kushiriki katika zoezi kikamilifu. Aidha, vyama viliishauri Tume isogeze mbele muda wa kuanza kwa zoezi la uboreshaji ili kutoa fursa kwa wao kuhamasisha wananchi na wafuasi wao kujitokeza katika zoezi hilo,” amesema Jaji Mwambegele.


Amewataja wadau wengine waliotoa maoni kuwa ni pamoja na taasisi na Asasi zilizoomba kibali cha kutoa elimu ya mpiga kura wakati wa uboreshaji ambazo zilieleza kuwa kibali kinapotolewa na Tume huwa ni muda mfupi kufikia zoezi la uboreshaji kuanza na wakashauri Tume ione namna ya kutoa kibali kwa muda utakaowawezesha kupata fedha kutoka kwa wafadhili ili zoezi likianza nao waanze kutoa elimu hiyo.


Kwa upande wa Taasisi na Asasi zilizoomba kibali cha kuwa waangalizi wa uandikishaji wakati wa uboreshaji, zilieleza kuwa kibali kinapotolewa na Tume huwa ni muda mfupi kufikia zoezi la uboreshaji kuanza na wakashauri Tume ione namna ya kutoa kibali kwa muda utakaowawezesha kupata fedha kutoka kwa wafadhili ili zoezi likianza nao waanze kazi ya kutazama namna zoezi linavyoendeshwa.


Maoni mengine ya wadau yaliyopelekea Tume kufikia uamuzi huo wa kusogeza mbele tarehe ya kuanza na kuzindua uboreshaji wa Daftari ni yale ya kuishauri Tume ijipe muda wa kutosha kutoa elimu ya mpiga kura kwa wadau na wananchi kabla ya kuanza kwa zoezi lenyewe, ili wananchi wengi waweze kuelewa zoezi husika na hivyo kuwawezesha kujitokeza kwa wingi wakati zoezi litakapoanza.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa