• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TALAKA YATAJWA KUWA CHANZO KIKUBWA CHA UNYANYASAJI WA WATOTO MASASI

Posted on: June 16th, 2017

Wazazi na walezi Wilayani Masasi Mkoani Mtwara wametakiwa kuacha tabia au mazoea ya kupeana talaka bila sababu za msingi kwani hiyo ni sasabu kubwa inayopelekea watoto wengi kukosa haki zao za msingi ikiwemo kupata malezi bora,  elimu, mavazi na huduma za afya na hivyo kupelekea watoto wengi kukosa fursa sawa kama kauli mbiu ya maadhimishao haya inayosema “Maendeleo Endelevu 2030 Imarisha Ulinzi na Fursa sawa kwa Watoto”

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya  ya masasi  Mh. Selemani  Mzee wakati akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha mbuyuni Halmashuri ya Wilaya ya Masasi  kwenye  kilele cha maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika  katika Halmashauri hiyo na kuwaeleza kuwa hiyo tabia ni inafanya watoto kukosa haki za msingi huku wazazi wao wakianzisha maisha mengine wakati watoto wanabaki na bibi zao au walezi ambao mara nyingi wanauwa hawana uwezo wa kuwapatia mahitaji ya msingi.

“Tabia ya wanandoa  kutalikiana au kwa msemo wa masasi kumwagikana iachwe mara moja  watu mkioana na kupata watoto ni vizuri mkabaki pamoja ili mlee watoto lakini pia mnakuwa mfano bora kwa watoto hata wakija kuwa na famila zao watadumu katika ndoa zao”  alisema Mzee.

Mhe. Mzee alisema jamii inapaswa kuimarisha ulinzi kwa watoto wote pale inapoonekana kuna dalili za  unyanyasaji na kupinga  mambo yote yanayohatarisha ustawi na usalama wa watoto wote wawe na furaha wakati wote kwa kuwapenda na kuwajali.

Aidha selemani alitoa  rai kwa jamii kupinga na kukemea kwa nguvu zote unyanyasaji wa kijinsia kama kuwanyanyasa watoto kingono, kuwabaka au kuwaingilia kimwili watoto wa kike an unyanyasaji unaweza kuwa wa kihisia mfano kutukana mbele ya watoto au kupigana, kuwatukana, kuwatisha, kuwapuuza, kuwatenga au kuwafanya kichekesho.

Jamii inapaswa kuwapatia elimu watoto kwani hakuna kitu chenye thamani na urithi bora kwa watoto kama elimu, mambo yote wafanye ila elimu liwe ni kipaumbele cha kwanza kwenye kila familia kwa kuhakikisha watoto wanapelekwa kweny program za elimu ya awali, kuwapatia elimu ya msingi na sekondari ambayo kwa sasa Serikali inatoa elimu hii bure lakini pia ni muhimu watoto wanaomaliza darasa la saba kuwapeleka kwenye shule za ufundi stadi.

Pia wazazi/walezi na jamii kwa ujumla wanapaswa kuhakikisha mazingira wanayoishi watoto yanakuwa safi na salama kuanzia wao wenyewe hadi mavazi yao na kuwa wepesi kuwapeleka watoto wao hospitali pindi tu wanapougua lakini wasisite kuwapeleka watoto kupata chanjo za magonjwa kama kifua kiuu, polio, kifaduro, donda koo homa ya ini, tetenasi nk. Kwani chanjo hizo huzuia watoto wasiambukizwe na magonjwa hayo.

Amekemea tabia ya baadhi ya wananchi kuwaajiri na kuwafanyisha kazi ngumu watoto lakini amewaomba kuungana kwa pamoja kuwaepesha watoto na kazi zote hatarishi na badala yake watoto waweze kusaidia kazi ndogondogo na si vinginevyo.

Bibi Changwa Mkwazu, Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Masasi akitoa taarifa mbele ya Mkuu wa Wilaya, alisema kwa mwaka 2016/2017 halmashauri ya wilaya ya masasi imeendelea kuwasaidia watoto walio katika mazingira hatarishi ambapo katika bajeti yake imetenga Tsh. 7,984,000 kwa ajili ya kuwasaidia kupata huduma muhimu za shule kama vile kalamu, daftari na sare.

Pia halmashauri ya wilaya ya masasi kupitia Idara ya afya imefanikiwa kuwapatia sare za shule, kalamu watoto wapatao 150 zenye thamani ya Tsh. 2,250,000 na kuwakatia kadi za Bima ya afya ya Jamii (CHF) zenye thamani ya Tsh. 250,000 kwa lengo la kuwawezesha watoto hao kupata huduma za msingi.

Halmashauri ya wilaya ya masasi imefanikiwa kutoa chanjo ya Vitamini A  kwa watoto 3742 walio chini ya miaka mitano kati ya watoto 2449 waliotarajiwa, pia imetoa chanjo ya kuzuia Kifua Kikuu kwa watoto 3548 kati ya watoto 2449 waliotarajiwa sawa na asilimia 144.

Pia halmashauri imetoa chanjo ya Polio kwa watoto 3361 kati ya watoto 2449 waliotarajiwa, chanjo ya kuzuia kifaduro, dond koo, homa ya ini na tetenasi kwa watototo 3396 kati ya watoto 2449 tarajiwa sawa na asilimia 138

Bi Changwa alisema kupitia kitengo cha Ustawi wa Jamii, halmashauri imefanikiwa kushughulikia matatizo mbalimbali ya ya watoto yahusuyo ukatili na unyanyasaji wa watoto ambapo imefanikiwa kutatua na kutoa ushauri wa kisaikolojia kwa watoto wapatao thelathini na mbili na kutoa msaada wa kisheria kwa watoto kumi na moja.

Kwa naiaba ya halmashauri ya wilaya ya masasi yaliyashukuru mashirika yasiyo ya kiserikali (NG’OS na CBO’S), waheshimiwa madiwani, viongozi wa kata na wadau wengine waliowezesha halmashauri ya wilaya ya masasi kufikia mafanikio hayo nab ado anawaomba kuendeleza ushirikiano ili kuwafanya watoto kupata ulinzi na furaha sawa na hatimaye Tanzania ipate maendeleo endelevu.

Siku ya mtoto wa afrika duniani huadhimishwa na kukumbuka mauaji ya watoto zaidi ya mia sita (600) yaliyotokea huko nchini afrika ya kusini kwenye kitongoji cha soweto mwaka 1976”, mhe. selemani mzee, mkuu wa wilaya ya masasi alisema.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa