• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

TAARIFA YA UCHUNGUZI WA VURUGU SHULE YA SEKONDARI CHIDYA WAKAMILIKA,BODI YATOA MAAMUZI

Posted on: September 29th, 2018

Baada ya uchunguzi kufanyika juu ya vurugu zilizofanywa na wanafunzi wa  shule ya sekondari chidya tarehe 1 septemba 2018 na kusababisha hasara ya zaidi ya milioni 18, Bodi ya shule ya sekondari chidya imefikia maamuzi ya kufukuza wanafunzi 23 huku wanafunzi 8 wakisimamishwa shule kwa muda wa siku 21.

Maamuzi hayo yametolewa tarehe 27 septemba, 2018 baada ya kupitia taarifa za uchunguzi  wa tukio hilo na kujiridhisha pasipo na shaka yoyote kuwa wanafunzi hao wanastahili adhabu hiyo kwani wamekutwa na hatia. Aidha taarifa ya bodi imeeleza kuwa hatua hiyo inalenga kukomesha tabia za migomo shuleni hapo na kutoa fundisho kwa wanafunzi waliobaki.

Afisa elimu sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi  ambaye pia ni mjumbe wa bodi ya shule ya sekondari ya Chidya ndugu Juma Kasandiko,  ameeleza kuwa  sababu kuu zilizofanya wanafunzi  23 waliofukuzwa  shule ni majina yao kutajwa na vyombo zaidi ya vitatu vya uchunguzi, kutoka nje ya shule baada ya kufanya vulugu na kutorejea  jambo ambalo ni kinyume na sheria za shule.

Kasandiko amefafanua kuwa  wanafunzi 23  waliofukuzwa shule kati yao 6 ni kidato cha sita, 12 ni kadato cha nne na 5 kidato cha tatu.

Kwa wanafunzi wa kidato cha nne ambao wamefukuzwa shule, bodi imewapa fursa ya kurudi  kufanya mitihani yao ya kumaliza elimu ya kidato cha nne kwasababu wameshasajiliwa kufanya mtihani huo.

Kuhusu fidia ya hasara iliyosababishwa na vurugu hizo, ndugu Kasandiko ameeleza kuwa italipwa na wananfunzi wote walioshiriki mgomo yaani wanafunzi 23 waliofukuzwa shule, wanafunzi 8 waliosimamishwa shule kwa siku 21 na wanafunzi  251 walioshiriki kwenye vurugu lakini  hawakuondoka shuleni  baada ya vulugu  na hawakutajwa mara nyingi kwenye ripoti za uchunguzi kama vinara wa vurugu hizo ambapo kila mwanafunzi atatakiwa kulipa shilingi 64,000.

“Hatua hizi za kinidhamu kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Chidya waliofanya vurugu  na kusabaisha hasara na utulivu wa shule, ni fundisho kwa wanafunzi wanaobaki na shule zingine zote kwani sheria zitaendelea kuchukuliwa kwa wanafunzi wote wanafanya vurugu shuleni ikiwemo kufukuzwa shule” alisistiza Kasandiko.

Aidha ndugu Kasandiko amewasistiza walimu kuwa “ni vizuri mkasimamia sheria za shule kwa kujiwekea utaratibu wa kusikiliza malalamiko ya wanafunzi ili kubaini haraka matatizo ya wanafunzi na kuyatatua, pia kwa walimu wanaoshirikiana na wanafunzi kuhamasisha migomo tabia hiyo muache kabisa kwani sitasita kuwachukulia hatua za kinidhamu. Mfanye  kazi kwa kuzingatia sheria na miongozo ikiwemo kuwa walezi na sio kuhamasisha  wanafunzi kufanya vurugu”

Kwa upande wake Mkuu wa Shule hiyo mwalimu Zawadi Mdimbe amezishukuru kamati za uchunguzi  kwa kufanya kazi zao  vizuri  ambapo taarifa zilizowasilishwa zimeiwezesha bodi ya shule kutoa maamuzi bila upendeleo au kumwonea mtu yeyote na hatimaye sasa shule itakuwa na utulivu  na amani na kuendelea kutekeleza majukumu ya kila siku ikiwemo maandalizi ya mitihani ya kitaifa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa