• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SIKU YA WAZEE DUNIANI LEO YAAMBATANA NA ZOEZI LA CHANJO YA UVIKO-19 MASASI DC

Posted on: October 1st, 2021

Tarehe 1 Oktoba ya kila mwaka, ni kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani iliyoanzishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 14 Desemba 1990. Maadhimisho haya ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Vienna wa Mwaka 1982 kwa Ajili ya Wazee Duniani, “The Vienna International Plan of Action on Ageing” ulioboreshwa tena na Mkakati wa Madrid, Hispania wa Mwaka 2002 ili kuweza kupambana na changamoto za wazee katika Karne ya 21 na kuendelea mchakato wa maendeleo fungamani ya binadamu kwa ajili ya wote. Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani ni moja kati ya jitihada za Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN) katika kutambua na kuhamasisha jamii kuweza kulinda na kutetea haki msingi za wazee duniani. Maadhimisho ya Mwaka 2021 yananogeshwa na kauli mbiu “Matumizi Sahihi ya Kidigitali kwa Ustawi wa Rika Zote.”

Mh.Mariam Chaurembo (Mkuu wa Wilaya ya Nanyumbu) ambaye alikuwa Mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo ya Siku ya Wazee Duniani akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Brigedia Jenerali Marco Gagut yaliyofanyika Leo tarehe 01.10.2021 ambapo Kimkoa yaliadhimishwa katika kijiji cha Nagaga  kilichopo katika kata ya Lulindi Halmashauri ya Wilaya ya Masasi akiongea na Wazee hao alisema, kwa sasa kuna ongezeko kubwa la wazee Duniani jambo ambalo limezidisha changamoto nyingi kwa wazee kama vile mauaji kwa wazee yatokanayo na imani za kishirikina katika Maeneo mbalimbali,kutokwepo kwa huduma bora za kiafaya,Kipato Duni, Kuachiwa mzigo Mkubwa wa kulea watoto Yatima, Aliendelea kusema kwa kuziasa Halmashauri zote ndani ya Mkoa kuwa kuanzia Novemba 30 Mwaka huu kuchukua hatua mbalimbali ili kuwasaidia wazee ikiwemo kuanzishwa kwa Mabaraza ya Wazee ya katika ngazi zote , kubaini wazee wote wenye mahitaji Maalumu na kuwapatia kadi za Bima ya Afya ili waweze kupatiwa Matibabu bila malipo 

Hii ni siku ambayo imetumika pia kwa ajili ya maboresho ya afya ya wazee sehemu mbalimbali za dunia, kwa kuwapima magonjwa kama vile: Kisukari, BP, Tezi Dume pamoja na kupatiwa huduma za msaada wa kisaikolojia sanjari na elimu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya Ugonjwa wa Virusi vya Korona, UVIKO-19. Bado kuna haja ya kuendelea kuboresha huduma ya afya, elimu, lishe, kipato na makazi kwa wazee wengi, ili waweze kuishi kwa amani, furaha na utulivu na kuwaasa Wazee wote kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kupata chanjo ya Uviko-19 katika maeneo mbalimbali ya Vituo vya kutolea huduma.

Lakini pia alitumia siku ya leo Mbele ya Wazee hao kwa kuwataka Kujiandaa kwa ajili ya Ujio wa Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi, zoezi ambalo linategemewa kuanza  Mwakani Mwezi oktoba 2022, japo Maandalizi yake yanategemewa kuanza hivi karibuni kwa kufanya Sensa ya Majaribio katika Baazi ya Maeneo nchini Mwisho aliwashukuru Wazee wote kwa kuendelea kutoa Michango yao kwa kuendelea kujijenga kiuchumi na kuujenga uchumi wa taifa kwa ujumla .

Kaimu Mkurugenzi wa Halamshauri ya Wilaya ya Masasi Ndugu Joshua Sanga (Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya Masasi) akiwakaribisha Wageni wake Kutoka Maeneo Mbalimbali wakiwemo Wazee leo tarehe 01.10.2021 katika Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani ambapo Kimkoa Sherehe hizi Zimefanyika katika Kijiji cha Nagaga Halmashauri ya Wilaya ya Masasi yenye Kauli Mbiu “Matumizi Sahihi ya Kidigitali kwa Ustawi wa Rika Zote.” ambapo pia Kaimu Mkurugenzi alichukuwa nafassi hii kuwaasa Wazee na Vijana Kujitokeza kwa wingi Kushiriki kwenye Zoezi la Chanjo ya Uviko-19 Katika Vituo vyetu mbalimbali vya Kutolea huduma.

Mratibu wa Chanjo wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Bi.Brandina Mpunga akiwa amesimama mbele ya Wazee akiwaasa juu ya kupatiwa Chanjo ya Uviko-19  akitumia fursa hiyo pia kwa kutoa Elimu kwa Wazee hao juu ya Umuhimu wa kuchanja na kuondokana na Imani potofu zinazoenezwa Mitaani juu ya Chanjo hizo, ambapo kwa siku ya leo ambayo ni Uzinduzi wa chanjo awamu ya Pili Muitikio kwa Wananchi Umeonekana kuwa Mkubwa sana katika Maeneo mbalimbali ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.

Daktari akiwa na mmoja kati ya Wazee walio hudhulia kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani akitoa huduma ya Vipimo bure kwa wazee hao kwa magonjwa kama vile: Kisukari, BP, Tezi Dume pamoja na kupatiwa huduma za msaada wa kisaikolojia sanjari na elimu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya Ugonjwa wa Virusi vya Korona, UVIKO-19.

 
Kikundi cha Sanaa za Ngoma za Asili kikitumbuiza mbele ya Wazee, pamoja na Meza Kuu kwa kutoa Burudani mbalimbali wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani  ambayo hufanyika kila Mwaka tarehe moja Mwezi Oktoba yenye Kauri mbiu Mwaka huu “Matumizi Sahihi ya Kidigitali kwa Ustawi wa Rika Zote.”


Muguzi wa Afya akiendelea na Zoezi la Kutoa Chanjo ya UVIKO-19 kwa Wazee Waliojitokeza leo tarehe 01.10.2021 katika kuadhimisha Siku ya Wazee Duniani ambapo Kimkoa ilifanyika Katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Katika KIjiji cha Nagaga

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa