• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA NA KUIMARISHA HUDUMA ZA KIJAMII: DKT.SAMIA SULUHU HASSAN

Posted on: September 24th, 2025

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan leo tarehe 24 Septemba 2025 ameendelea na mikutano yake ya kampeni Mkoani Mtwara, ambapo akiwa katika Jimbo la Ndanda lililopo  Halmashauri ya Wilaya ya Masasi,  amewahakikishia Wananchi kuwa Serikali itaendelea na juhudi za  kuboresha na kuimarisha huduma za kijamii hususani  katika sekta ya Afya, elimu na maji ili Wananchi wapate huduma hizo kwa karibu.

Amesema Serikali itaendelea kusimamia utoaji wa huduma muhimu za kijamii kwa Wananch wote "Kama kuna maeneo hayajapata maji tuwahakikishie maji yatapatikana, maeneo ambayo umeme haujafika wakandarasi wapo kazini na kazi inaendelea hivyo itabaki wewe mwenyewe (mwananchi) kuuza korosho na kuvuta umeme nyumani".

Aidha ameongeza kuwa maeneo ambayo vituo vya Afya havipo Serikali itaendelea kujenga na kukamilisha maboma yote ya Zahanati pamoja na vituo vya Afya ili kuhakikisha Wananchi wanapata huduma karibu na makazi yao.

Pia katika Sekta ya Elimu amesema kwamba Serikali itaendelea na sera yake ya elimu bure bila malipo na kuimarisha elimu Jumuishi kwa Watoto wenye mahitaji maalumu ili waweze kupata elimu .

Katika eneo la Ndanda ameitaja shule maalumu ya Lukuledi ambapo amesema" natambua hapa Ndanda kule Lukuledi kuna shule yenye watoto wenye mahitaji maalumu, lakini inashida kidogo nimeambiwa haina uzio, gari la usafiri  na karakana ya mafunzo kwa vitendo ili kuboresha mazingira ya ujifunzaji kwaiyo niwahaidi vyote hivyo tutavikamilisha".alisema Samia.

Aidha akizungumzia suala la maji mhe.Dk.Samia Suluhu Hassan amewaeleza Wananchi kuwa kwasasa tayari Serikali imetoa fedha kiasi cha Shilingi Milioni 360 kwa ajili ya ujenzi wa machujio ya maji katika eneo la mradi wa Mwena- Liloya ili kuhakikisha Wananchi wanapata maji safi na salama mwaka mzima.

"Miaka mitano iliyopita tulijitahidi Serikali ilitoa fedha shilingi bilioni 13 tukatekeleza miradi 64 hapa, lakini bado miradi mingine inaendelea, lakini natambua katika Miradi ile tatizo letu kubwa maji yanakuwa ni machafu hivyo Serikali imeanza ujenzi wa machujio mawili ya maji, ikiwemo mradi wa Mwena- Liloya na pia tumeshamaliza usanifu na utafiti katika eneo la Ndanda na Nanganga ".


Hata hivyo amesisitiza kuwa huduma hizo za kijamii ni wajibu wa kawaida wa Serikali kwa Wananchi wake, na kwa hiyo haziwezi kuhesabiwa kama kazi ya Maendeleo bali ni haki ya msingi ya kila Mtanzania.


Kwa upande wake Mgombea Ubunge Jimbo la Ndanda kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Ndg.Faraji Buriani Nandala amesema kuwa tangu Serikali ya awamu ya sita iingie madarajani imepandisha sana thamani ya zao la korosho kwa kuwapatia pembejeo bure, hali ambayo imeongeza uzalishaji na kuleta tija kwa Wakulima sanjari na uwepo wa mfumo wa uuzaji wa korosho wa stakabadhi ghalani  umesaidia wakulima kupata stahiki zao kwa wakati.


#Kazi na Utu tunasonga mbele#..


24 Septemba 2025.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • TUNAWAHIMIZA TUMIENI SMART TOILET KWA ULINZI WA AFYA YA MAZINGIRA: AFISA AFYA MAZINGIRA

    September 28, 2025
  • AFISA AFYA MAZINGIRA: HAKIKISHENI MNAJENGA NA KUTUMIA VYOO BORA ILI KUEPUKA KUPATA MAAMBUKIZI YA MAGONJWA.

    September 28, 2025
  • Dkt.Samia Suluhu Hassan azuru kaburi la Rais wa awamu ya tatu Hayati Benjamin William Mkapa :Lupaso

    September 24, 2025
  • SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA NA KUIMARISHA HUDUMA ZA KIJAMII: DKT.SAMIA SULUHU HASSAN

    September 24, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa