• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

SEKRETARIETI YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA YAWAJENGEA UWEZO VIONGOZI WANAWAKE MTWARA

Posted on: September 24th, 2018

Sekretarieti ya maadili ya viongozi wa umma kanda ya kusini imeamua kuwajengea uwezo viongozi wanawake wa ngazi mbalimbali wakiwemo madiwani na wakuu wa idara  katika  wilaya 5  na Halmashauri 7 za Mkoani Mtwara lengo ikiwa ni kuwaongezea uelewa kuhusu maadili ya viongozi wa umma katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo yaliyofanyika tarehe 21 setemba 2018 wilayani Masasi, Katibu Msaidizi Ofisi ya Rais Maadili ya Viongozi Kanda ya Kusini ndugu Mayina Henjewele alisema kuwa mafunzo hayo yatatoa fursa kwa viongozi hao kujua majukumu na wajibu wa sekretarieti ya maadili pamoja na mambo muhimu ya kuzingatia katika utumishi wa umma ikiwemo sheria na kanuni

Mwezeshaji kutoka ofisi ya maadili   Mtwara ndugu Ramadhani Ramadhani akitoa mafunzo kwa viongozi wanawake mkoa wa Mtwara  yaliyofanyika wilayani masasi

Henjewele alifafanua sababu za mafunzo hayo kuwa ni baada ya kufanyika utafiti mwaka 2015 kupitia taasisi yao ya kukuza  uelewa kwa wananchi kuhusu  majukumu ya sekretarieti hiyo ambapo ushiriki wa wananwake katika kutoa taarifa za ukiukwaji wa maadili kwa viongozi wa umma ulikuwa mdogo sana ukilinganisha na wanaume.

“Matokeo yalionesha kuwa asilimia moja tu ya wananwake katika maeneo ya vijiji na miji walioweza kutoa taarifa za ukiukwaji wa maadili miongoni mwa viongozi wa umma”

Alisema hali hiyo ililazimu Sekretarieti ya maadili ya viongozi wa umma kuandaa mafunzo hayo katika mikoa yote inayotekelezwa mradi huo ikiwemo  Mtwara. "Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uelewa viongozi wanawake katika mamlaka za Serikali za mitaa kuhusu maadili ya viongozi wa umma ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maadili.

Aidha, Henjewele alisema kuwa viongozi wananwake kuna wakati wanashindwa kutekeleza majukumu yao kama viongozi  kwa kuwa hawana uelewa wa mambo mbaimbali ya kimaadili “tunawajengea uwezo wa kujiamini kwa kujua sheria na taratibu lakini pia kufahamu wajibu wao kama viongozi katika kutumikia wananchi”


Mwezeshaji kutoka ofisi ya madili  ndugu Irene Triplow akitoa mafunzo kwa viongozi wanawake mkoa wa Mtwara yaliyofanyika wilayani masasi

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya masasi Emmanuel Ryoba  wakati akifungua mafunzo hayo, aliwaeleza viongozi hao kusikiliza kwa makini mafunzo hayo ili   baada ya kupata mafunzo hayo i wakawahamasishe na kuwaelimisha wanawake wengine katika ngazi za chini kwenye mitaa na Kata itanisaidia kuwajengea ujasiri wa kutoa taarifa kwenye mamlaka husika pindi wanapokumbana na ukiukwaji wa maadili

Ryoba aliwakumbusha viongozi hao kuwa Wananchi wanawategemea  hivyo ni vema wakatumia nafasi zao kuleta maendeleo ikiwemo kuelimisha wananchi juu ya mambo mbalimbali, ni lazima wawe mfano wa kuigwa, kwa kuwa wawazi na kuwajibika ipasavyo pamoja na kuzingatia ahadi za uadilifu walizoapa baada ya kupata dhamana hizo.

Akiongea kwa niaba ya madiwani wenzake mhe. Asha Rashid Tebwa diwani wa viti maalum kata ya milongodi wilaya ya Tandahimba alisema kuwa “Mafunzo ni mazuri yatatusaidia katika utendaji kazi wetu ikiwemo kufuata sheria na taratibu lakini Elimu ya maadili inapaswa ipelekwe kwenye ngazi ya vijiji na kata maana huko ndiko kwenye wananchi wengi”

  Mhe. diwani Asha Rashid Tebwa diwani wa viti maalum kata ya milongodi wilaya ya Tandahimba akichangia hoja wakati wa mafunzo

Mhe Asha amewashauri wanawake wenye ndoto za kuwa viongozi lazima wafahamu sheria na taratibu za kuwa viongozi bora, lakini pia wajiamini kutoa maoni katika vikao mbalimbali vya maamuzi na kutetea hoja zao badala ya kuwaachia wanaume waamue badala yao. “Hakuna aliezaliwa kiongozi Uongozi ni kujifunza”

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa