• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

NAIBU KATIBU MKUU OR-TAMISEMI AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI UPANUZI WA KITUO CHA AFYA NAGAGA

Posted on: June 7th, 2018

NAIBU KATIBU MKUU  OR-TAMISEMI  AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI UPANUZI WA KITUO CHA AFYA  NAGAGA.

“Wahenga walisema kilio lia na mwenyewe, mlilia, tukasikia, na kutokana na kilio chenu tukaja tulie pamoja na hatimaye zikaletwa fedha  shilingi milioni 400 kwa ajili ya  upanuzi wa kituo cha afya cha Nagaga na majengo yanaonekana, nawapongeza”   alieleza  Naibu Katibu Mkuu  OR- TAMISEMI  Dr. Zainabu Chaula wakati alipotembelea utekelezaji wa mradi wa  upanuzi wa kituo cha afya Nagaga unaolenga kukifanya kituo hicho kutoa huduma bora kwa wananchi wa  Kata ya Namalenga na vijiji jirani.

Dr. Chaula amesema, utekelezaji wa mradi huo umezingatia thamani ya fedha iliyotolewa kwani  majengo ni mazuri na yana ubora unaotakiwa hivyo adhima ya serikali ya kuboresha miundombinu na huduma za jamii kwa ujumla inatekelezeka kwa vitendo baada ya kuona majengo ambayo yamejengwa katika kituo hicho cha Nagaga.

Pia Dr. Chaula amewapongeza wananchi  wa Nagaga kwa ushirikiano wanaoutoa katika utekelezaji wa mradi huo na hivyo inaashiria wananchi kuwa wanatambua mipango ya serikali na kuiunga mkono kwani suala la maendeleo linahitaji ushirikiano kati ya serikali, wadau wa maendeleo na wananchi wenyewe na sio kuiachia serikali pekee.

Katika mradi huo jumla ya majengo matano ikiwemo jengo la maabara, upasuaji, wodi ya wazazi,  jengo la kuhifadhia maiti na nyumba ya mtumishi kwa gharama ya shilingi milioni 400.

Aidha Dr Chaula amewaeleza wananchi kuwa, majengo hayo yamejengwa na mafundi wa kawaida kwa kushirikiana na wataalamu hivyo nawakumbusha vijana wenye ujuzi kujiunga kwenye vikundi ili waweze kupata fursa za kupata  mikopo, kandarasi za ujenzi wa miradi na  huduma mbalimbali  kwani serikali imedhamiria kuwainua vijana kwa kuwapa fursa mbalimbali za kushiriki kwenye shughuli za maendeleo na kuwaongezea kipato.

Akizungumzia kwa niaba ya wananchi wa kijiji cha Nagaga  ndugu Afati Mangochi alisema kuwa wananchi wanaipongeza serikali kwa kuleta fedha za kupanua kitu hiki cha afya ambacho kikikamilika kitasaidia utoaji wa huduma za uhakika kwa  wananchi wa Nagaga na walio nje ya nagaga wapatao 129,609 sawa na 47% ya wakazi wote wa masasi.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Namalenga mhe. Arafath Ismail Hassani ameahidi kuendelea kusimamia miradi huo mpaka utakapokamilika pamoja na kuhamamsisha wananchi kujitolea kwa hali na mali kuunga mkono serikali katika kuboresha na kusogeza huduma za jamii kwa wananci ikiwemo usimamizi wa miradi inayotumia fedha za serikali na wadau wa maendeleo.

Halmashauri ya wilaya ya Masasi ina jumla ya vituo vya kutolea huduma ya afya  47 ambapo kati ya hivyo vituo vya afya ni 2, na zahanati 31 zinazomilikiwa na serikali vingine 14 vinamilikiwa na wadau wenngine kama dini na watu binafsi.

Nyumba ya mtumishi  kituo cha Afya Nagaga

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa