• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MKUU WA MKOA WA MTWARA APONGEZA KASI YA UANDIKISHAJI ORODHA YA WAPIGA KURA MASASI DC

Posted on: October 16th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara mhe.Kanali Patrick Sawala amewataka Wananchi wote wenye sifa ambao bado hawajajiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura wa Serikali za Mitaa unatarajia kufanyika Nov 27,2024 kuendelea kujitokeza kujiandikisha kwenye vituo vilivyopo katika maeneo Yao  ili wapate sifa ya kuchagua viongozi bora watakao waletea Maendeleo.


Mhe.Sawala amesema hayo Leo tarehe 16, 2024 katika muendelezo wa ziara yake ya kukagua na kuhamasisha uandikishaji katika Halmashauri za Mkoa wa Mtwara ambapo akiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi ameweza kutembelea Kata ya Mpeta kwenye Kijiji Cha masuguru kitongoji Cha msikitini pamoja na Kijiji Cha mpeta ambapo pamoja na kuwasalimia Wananchi pia amepata fursa ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa Shughuli za uandikishaji wa orodha ya wapiga kura kutoka Kata ya Mpeta ambapo ameonyesha kufurahishwa na taarifa ya Kata nzima kuwa  Wananchi wamehamasika kwa kiasi kikubwa kujiandikisha na wanajua umuhimu wa kujiandikisha na wapo tayari kuendelea kutoa hamasa kwa Wananchi ili waendelee kujitokeza kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura kwa siku zilizobakia ili waweze kufikia malengo.


"Nimekuja hapa ndugu zangu Pamoja na kuwasalimia lakini pia nimekuja kufuatilia ili kuona je Shughuli hii ya uandikishaji kwenye orodha ya wapiga kura Kwa ajili ya uchaguzi wa viongozi wetu wa Serikali za Mitaa, je unakwenda kwa utulivu, unakwenda kwa amani, je kuna changamoto zozote ili kama zipo tushauriane na kuona namna ya kuziondoa"... alisema Mkuu wa Mkoa


Amesema hata hivyo anayo furaha kubwa kuona zoezi hili la uandikishaji linakwenda kwa amani na utulivu,hakuna fujo Wala vurugu" hongereni sana wanampeta na Wana Masasi wote kwa ujumla kwa kufanya mchakato wa kujiandikisha kwa amani na utulivu"


Aidha mhe.Sawala ameongeza kuwa " inawezekana sisi tumejiandikisha Lakini  wapo baadhi ya ndugu, jirani, marafiki n.k ambao wana sifa ya kupiga kura ikiwemo umri wa Miaka 18 na kuendelea, awe ni raia wa Tanzania, awe mkazi wa eneo husika na sifa Nyinginezo, hivyo nitoe rai kwenu  wana Mpeta msifanye kosa tarehe 27 Nov,2024 wa kutokwenda kupiga kura, hamtakiwi kufanya majaribio, nendeni mkapige kura na kuwachagua viongozi watakao endana na hatua za mhe. Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, anataka nini kwa Wananchi wake, anaye jua matarajio na matamanio kwa Wananchi, kiongozi anaye jua kutafsiri nini matarajio ya mhe.Rais na hivyo kiongozi kiongozi atatoka miongoni mwenu.


"Niwaombe sana mkajiandikishe na mkisubiri kuchagua kiongozi Bora."


Naye  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Masasi ambaye pia ndiye Diwani wa Kata hiyo ya Mpeta Mhe.Ibrahimu Chiputula akizungumza kwaniaba ya Wananchi wa Kata hiyo amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mtwara kwa kuwatembelea na kuzungumza nao juu ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa hivyo wanahaidi katika siku chache zilizosakia  wataendelea kuwahamasisha Wananchi kuendelea kujitokeza kujiandikisha kwenye orodha ya wapiga kura ili ifikapo Nov 27,2024 watimize wajibu wao kikatiba kuwachagua viongozi Bora.


Hata hivyo, Zoezi la uandikishaji orodha ya wapiga kura limeanza rasmi Oktoba 11, 2024 na litahitimishwa tarehe 20,2024.


Ifahamike kuwa Kata ya Mpeta ambayo inaunda Vijiji 4 ambavyo ni Mpeta, Makanyama, Masuguru na Huwe

ni miongoni mwa kata 34 za Halmashauri ya Wilaya Masasi ambapo inapatikana katika Jimbo la Lulindi, tarafa ya Chiungutwa huku ikiwa na jumla ya idadi ya watu 5,871 Kati ya watu hao wanaune ni 2,779 na Wanawake 3,092. Aidha Kata ya Mpeta Ina jumla ya kaya 1,847 zenye wastani wa watu 3.2

@ Masasi DC 

16/10/2024

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa