• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mbunge wa Mkoa wa Mtwara aongoza Zoezi la ugawaji wa taulo za kike Halmashauri ya Wilaya Masasi

Posted on: September 25th, 2024

Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Mtwara Mhe.Agnes Hokororo Leo tarehe 25/09/2024 ameongoza zoezi la ugawaji taulo za kike kwa wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi huku akimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi.Beatrice Mwinuka  kwa kutenga fedha za ndani kwa ajili ya ununuzi wa taulo za kike.

Zoezi hilo ambalo ni endelevu katika Shule zote zilizopo Halmashauri ya Wilaya Masasi, pamoja na mambo mengine  limeanzia katika Kata ya Mbuyuni na wanufaika wa msaada huo ni wanafunzi shule ya Msingi mbuyuni, Mitonji pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mbuyuni.


Akizungumza kabla ya ugawaji wa taulo hizo kwa wanafunzi hao wakike ambao wame wawakilisha  wanafunzi wa shule zingine mhe.Hokororo ameanza kwa kumpongeza na kumshukuru Mkurugenzi Mtendaji pamoja na timu yake nzima ya Uongozi kwa kuchukua hatua ya kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa taulo za kike katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi.

Amesema Halmashauri ya Wilaya ya Masasi kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali kwamba kila Halmashauri lazima itenge fedha hivyo na Kwa kuona umuhimu imeweza kuweka bajeti ya shilingi Milioni 20 na kuanza kununua taulo za kike kwa ajili ya kuwastili Watoto wakike ambao wanakumbana na changamoto mbalimbali na hasa wakiwa katika mazingira ya shuleni.


" Hivyo rai yangu kwa Halmashauri iendelee kutenga fedha za ndani kupita mfuko wa elimu kwasababu kwa kufanya hivi zitaendelea kuwasaidia Watoto wetu wa shule za Msingi na Sekondari ".


Aidha mhe.Hokororo akatumia fursa hiyo pia kuzungumza na Wazazi/walezi ambao wamejitokeza katika zoezi hilo la ugawaji wa taulo za kike kwa wanafunzi, ambapo amewakumbusha Wazazi watambue kuwa watoto wana haki za msingi na ipo Sheria  inayowalinda ambayo imetungwa na bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikielekeza kupitia haki ya Kwanza ya kuishi kwa kuwapatia chakula, malazi na mavazi.


" haki ya pili ni kuwalinda kwa kuhakikisha mambo yao yote na ustawi wa watoto unakuwa chini yenu  Wazazi na kuwahakikishia usalama kwa kuwalinda na kuwapatia mahitaji yao ya msingi  hususani taulo za kike ambazo ni moja ya mahitaji muhimu ambayo Mtoto anatakiwa kuwa nayo hivyo ni wajibu wenu  kuhakikisha Watoto wanatimiziwa mahitaji hayo."


Bi.Ashura Mrope ni mzazi Pamoja naye Vaileth Sijaona ambaye ni mwanafunzi pamoja na kushukuru kupatiwa Elimu ya afya na malezi kwa Watoto pia wameshukuru kwa msaada huo wa taulo za kike walizopatiwa wanafunzi hao kuwa utawasaidia kujistiri katika siku zao na hasa siku za masomo tofauti na hali ya sasa huwa mara nyingi wanabaki nyumbani na kufanya kukosa vipindi.


25/09/2024


@.. Masasi DC

Kazi iendeleeee!

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa