• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAKARANI WAONGOZAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA MGUU SAWA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025.

Posted on: October 25th, 2025


Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Ndanda na Lulindi Ndg. Keneth Mgina amewataka Makarani waongozaji wa vituo vya kupigia kura uchaguzi kutekeleza majukumu yao kwa kufuata sheria, kanuni na maelekezo yote yatakayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) katika kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 29 Oktoba 2025.


Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku moja kwa makarani waongozaji wa wapiga kura yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Masasi-Mjini, amewataka  

 makarani wote kutumia vyema nafasi waliyopewa kwa uaminifu na weledi mkubwa.

“Ninyi mliopo hapa leo mmeteuliwa kwa mujibu wa sheria kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 74 kifungu cha sita cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, na tangu tarehe ya uteuzi wenu mnao wajibu wa kikatiba wa kutekeleza majukumu ya uchaguzi wa Rais, Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bara na Madiwani kwa niaba ya Tume katika vituo vya kupigia kura mlivyopangiwa, hivyo yawapasa mtambue kuwa  mnategemewa kuzingatia sheria, kanuni na maelekezo ya INEC mtakayopewa hadi kukamilika kwa zoezi la uchaguzi,” alisema Mgina

Aidha, aliwakumbusha makarani hao kutunza siri za taarifa na vifaa vya uchaguzi, pamoja na kuepuka vitendo vyovyote vinavyoweza kusababisha migogoro au kuathiri amani katika vituo vya kupigia kura.

Amesisitiza kuwa makarani ni kiungo muhimu kati ya wananchi na Tume ya Uchaguzi, hivyo wanapaswa kuwa mfano wa uadilifu na uwajibikaji katika kutekeleza majukumu yao.


Mafunzo hayo yamehusisha makarani wa vituo 623 vya kupigia kura vilivyopo katika kata 34 za Jimbo la Ndanda na Lulindi ambapo washiriki wamefundishwa kuhusu wajibu na majukumu ya makarani waongozaji wa wapiga kura, pamoja na namna ya kuwapokea na kuwaongoza wapiga kura katika vituo vya kupigia kura kwa kuzingatia kanuni za huduma kwa wateja.

Mgina alihitimisha hotuba yake kwa kuwataka makarani hao kwenda kuyafanyia kazi kwa vitendo mafunzo hayo, akisisitiza kuwa uchaguzi wa mwaka huu unahitaji uadilifu, umakini na uwajibikaji wa hali ya juu kutoka kwa watendaji wote wa Tume.

25/10/2025

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • KURA YAKO HAKI YAKO JITOKEZE KUPIGA KURA.

    October 25, 2025
  • MAKARANI WAONGOZAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA MGUU SAWA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025.

    October 25, 2025
  • KURA YAKO HAKI YAKO JITOKEZE KUPIGA KURA

    October 24, 2025
  • KILA LA KHERI WANAFUNZI WOTE WA DARASA LA NNE AMBAO MNAFANYA MTIHANI WA UPIMAJI KITAIFA DARASA LA NNE 2025.

    October 22, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa