• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAAFISA MAENDELEO YA JAMII NGAZI YA KATA WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU MIKOPO

Posted on: October 5th, 2024


Maafisa maendeleo ya jamii ngazi ya kata Leo tarehe 05/10/2024 wamepatiwa mafunzo kuhusu usimamizi na utoaji wa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa vikundi vya wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu.


Mafunzo hayo ambayo yamefanyika katika ukumbi wa zamani wa Halmashauri hiyo uliopo Masasi mjini yamehusisha Maafisa maendeleo ya jamii kutoka kata zote 34 za Halmashauri ya Wilaya ya Masasi huku lengo kubwa likiwa ni kuimarisha uelewa kuhusu mikakati ya usimamizi wa maendeleo ya jamii, hususani katika kusimamia mikopo ya asimia 10 kwa kufuata taratibu zote zinazotakiwa.


Aidha wawezeshaji wa mafunzo hayo ni Maafisa maendeleo ya Jamii ngazi ya Halmashauri hiyo wakiongozwa na Bw. Rashid Njozi ambaye ni Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, ambapo  amesisitiza umuhimu wa mikopo hiyo katika kuboresha maisha ya wanajamii, na kuwataka  maafisa hao kuyazingatia mafunzo ili kuboresha zaidi utendaji kazi wao katika kusimamia mikopo hiyo.


 “Mikopo hii inatoa fursa kwa vikundi vya wanawake, vijana, na walemavu kujiendeleza kiuchumi na hivyo kuchangia katika maendeleo ya jamii nzima, ni matumaini yangu kwamba mafunzo haya mtaongeza mara dufu utendaji wenu na pia yatasaidia kuleta mabadiliko chanya.” amesema Njozi


Mbali na hayo, katika kipindi cha mafunzo, washiriki wamehusishwa moja kwa moja katika mijadala, ambapo wameweza kutoa mawazo na maswali kuhusu usimamizi wa mikopo hiyo, pia mafunzo hayo yametoa fursa ya kubadilishana uzoefu na kukuza mbinu bora za kazi.


Awali akifungua mafunzo hayo Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo ya Wilaya ya Masasi Bi. Beatrice Mwinuka amewaasa washiriki wa mafunzo kuhakiksha wanakwenda kuhamasisha vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kuunda vikundi Ili waweze kunufaika na fursa za mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri.

Mwinuka amesema kuwa halmashauri itaendelea kutoa mikopo kwa  walenga lengo kuona makundi hayo yananifaika kiuchumi.


" Kwa mafunzo hayo mliopata hapa leo naomba nendeni mkawe mstari wa mbele katika kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa fursa ya mikopo hii ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kwani serikali inatoa fedha nyingi kupitia fursa hii,"...alisema Mwinuka.


Hata hivyo maafisa hao wa maendeleo ngazi ya kata pamoja na mambo mengine wamepata nafasi ya kujifunza taratibu za kuandika maombi ya mikopo pamoja na namna ya kusimamia fedha hizo kwa ufanisi ili kufikia malengo yaliyokusudiwa .

Katika hatua nyingine maafisa hao pia wamekula kiapo cha uadilifu katika kusimamia kile wanachokwenda kukitekeleza juu ya usimamizi na uhamasishaji wa mikopo ya asilimia 10 kwenye maeneo na mwisho wamehimizwa kuendeleza elimu waliyoipata kwa vikundi vyao ili kuhakikisha rasilimali zinatumika ipasavyo na kusaidia katika kuboresha maisha ya jamii.


Halmashauri ya Wilaya ya Masasi inaamini kuwa mafunzo hayo yatakuwa chachu ya mabadiliko chanya katika maendeleo ya jamii, kwasababu yana umuhimu mkubwa wa kuimarisha ushirikiano Kati ya Halmashauri na vikundi vya Maendeleo.


@.. Masasi DC

05/10/2024


     

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa