• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KUKAMILIKA KWA MRADI WA MAJI CHIPINGO KUMALIZA VIFO VINAVYOSABABISHWA NA MAMBA WA MTO RUVUMA

Posted on: October 19th, 2018

Kukamilika kwa Mradi wa Maji Chipingo – Mkaliwata  unaotarajia kuhudumia wananchi wa vijiji 8 katika kata za Chikoropola na Mnavira  sio tu utamtua mama ndoo kichwani lakini pia utamaliza tatizo la vifo vinavyosababishwa na mamba  katika mto Ruvuma wakati  wananchi hao wakiwa wanachota maji.

Hayo yamezungumzwa na waziri wa maji Profesa Makame Mbarawa wakati wa ziara ya kuKagua miradi ya maji inayoendelea kutekelezwa sasa wilayani Masasi na kueleza kuwa serikali inatumia fedha nyingi sana kutekeleza miradi ya maji lengo ikiwa ni kuwaondolea shida ya maji wananchi wa maeneo yote mijini na vijijini.

 “Mradi wa Chipingo –Mkaliwata ni mradi maalum kutokana na umuhimu wake kwa wananchi kwani utaondoa matatizo mawili ya ukosefu wa maji lakini pia vifo na ulemavu wa kudumu  unavyosababishwa na mamba wa Mto Ruvuma  pindi wananchi wanapochota maji katika mto huu,  nakuagiza mkandarasi ufanye kazi usiku wa mchana ili mradi ukamilike haraka” alisema Mbarawa.

Prof: Mkame alieleza kuwa serikali ina fedha za kutosha za kutekeleza miradi ya maji ambayo inaendelea na mipya ili kufikia lengo la vijiji vyote kuwa na huduma ya maji ifikapo mwaka 2020.

 “Naomba niwahakikishie kuwa mwezi desemba mtapata maji na kero ya maji itakuwa imeisha kabisa, nitamsimamia mkandarasi kuhakikisha anamaliza  kazi ndani ya kipindi akishindwa nitamfukuza kwani haiwezi kuwavumilia wakandarasi wasioweza kwenda na kasi inayotakiwa” alisisitiza Prof Makame

Wananchi wanapaswa kutumia muda wao mwingi kufanya shughuli za maendeleo na sio kukesha kutafuta huduma ya maji, hivyo serikali itahakikisha mradi huu unakamilika desemba 2018 ili wananchi wa chikolopola na Mnavira waepukane na adha ya kufuta maji mto Ruvuma ambako kuna  mamba wanaohatarisha maisha yao.

Aidha mheshimiwa Makame Mbarawa alitumia nafasi hiyo kuwaasa wananchi kutunza miundombinu ya maji kwani serikali inatumia fedh nyingi sana kuweka miundombinu hiyo, lakini pia utunzaji wa vyanzo vya maji ni muhimu sana wani bila kutunza vyanzo vya maji hakutakuwa na maji.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Chikolopola Mheshimiwa Edward Mahelela alimweleza Waziri kuwa zaidi ya watu 30  akiwemo watoto wameuawa na mamba wakati wengine wakipata ulemavu wa kudumu, hivyo kukamilika kwa mradi huo utaondoa kero zote mbili kwa wakati mmoja.

Mhandisi wa maji wa halamashauri ya wilaya ya amasasi Ndugu Fransis Bwire, akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo alieleza kuwa mradi huo utagharimu shilingi 3,983,700,074.22 mpaka kukamilika kwake.

Mhandisi alieleza kuwa vijiji vitakavyonufaika na mradi huo ni Chipingo, Manyuli,Rahaleo,Mapili, Chikolopola, Mkaliwata, Namyomyo na Mnavira vijiji ambapo kwa sasa wanatumia maji ya Mto Ruvuma pamoja na kununua wa bei kubwa ambapo ndoo moja inauzwa kati ya 500 hadi 1000.

Mradi wa chipingo –mkaliwata ni kati ya miradi ya miradi 6 ya maji ambayo inatekelezwa na halamashauri ya wilya ya masasi kupitia Programu ya maji na usafi wa mazingira vijijini (RWSSP).

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa