• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

KIKAO CHA WADAU WA ELIMU MASASI

Posted on: January 5th, 2018

  WADAU wa sekta ya elimu wilayani Masasi mkoani Mtwara wameshauri kuongeza kasi ya kuwa na ushirikiano wa pamoja katika kutatua changamoto zinazoikabili sekta hiyo ili kuweza kufanikisha lengo la kuinua kiwango cha elimu wilayani Masasi.

  Aidha,wadau hao wamezitaja baadhi ya changamoto ambazo zimekuwa ni moja ya sababu inayochangia kushuka kwa kiwango cha elimu wilayani Masasi kuwa ni walimu kutokuwa na hari ya ufundishaji, wazazi na walezi kutothamini thamani ya elimu,watendaji wa idara ya elimu kutokuwa na ushirikiano wa karibu na walimu.

  Ushauri huo waliutoa jana kwenye kikao cha pamoja cha wadau wa elimu wilayani Masasi kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya Masasi  na kuhudhuriwa na makundi mbalimbali ambao ni wadau wa sekta hiyo ambao ni walimuwakuu wa shule za sekondari na msingi,watendaji wa kata,maafisa elimu msingi na sekondari,waratibu kata elimu,wakuu wa idara,walimu wastaafu,viongozi wa dinina  wazee maarufu.

  Walisema moja ya sababu ambayo  inayochangia kushuka kwa kiwango cha elimu wilayani Masasi ni kukosekana kwa ushirikiano wa pamoja baina ya wadau wenyewe wa elimu katika kupanga na kutekeleza mikakati na maazimio yanayowekwa kwenye sekta ya elimu wilayani humo na kwamba kila mmoja hufanya anavyotakahali inayopeleka kutokuwa na makakati wa pamoja na kusababisha elimu kushuka.

 Wameeleza kuwa wazazi na walezi pia wanatakiwa kutambua kwamba na wao ni wadau wakubwa wa sekta ya elimu hivyo lazima waone umuhimu wa kuchangia elimu kwa ajili ya watoto wao kwani urithi wa mtoto ni elimu na badala ya kufikiri kuwa kila kitu kinapaswa kufanya na serikali peke yake.

  Wadau hao walisema ni wakati muafaka sasa kkuanza kujitathimini na kuwa kitu kimoja kwa kushirikiana kwa ukaribu ili kuweza kuzitatua changamoto hizo na hatimaye kuwa katika ramani nzuri ya kitaaluma kama ilivyo kwa wilaya nyingine  nchini badala ya kuendelea kushika mkia na kunyoosheana vidole.

 Walisema wilaya ya Masasi kupitia halmashauri zake mbili ya wilaya na ile ya mji Masasi kwa miaka ya hivi karibuni 2016 pamoja na mwaka 2017 zimekuwa hazifanyi vizuri katika sekta ya elimu kuanzia shule za msingi na sekondari hasa katika matokeo ya darasa la saba pamoja na kidato cha nne kuanzia ngazi ya wilaya,mkoa na taifa.

  Akichangia mada katika kikao hicho mwalimu wa shule ya msingi Mkomoindo,Joseph Chikawe alisema watendaji wa idara ya elimu pamoja na uongozi wa serikali ya wilaya wana wajibu wa kukutana na walimu kwa njia nyingine ili walimu hao waweze kueleza kero zao ambazo zinawafanya wasiwe na hari ya kujituma katika ufundishaji kwenye shule zao.

  “Walimuwana kero nyingi sana ndani ya nafsi zao ambazo kero hizi ni moja ya sababu inayowafanyawashindwe kuwa na morali ya kazi kwenye shule zao, hapa kamwe hawawezi kuzisema kwa sababu wakuu wa idara wapo lakini kama uongozi wa serikali na wakuu waidara hao tukikutana pamoja tutaweza kuzisema wazi,”alisema.

  Akifungua kikao hicho mkuu wa wilaya ya Masasi, Selemani Mzee alisema bado watendaji wa idara ya elimu wilaya humo wanayo kazi kubwa ya kufanya ilikuhakikisha sekta ya elimu inaondokana na changamoto zinazoikabili sekta hiyo na kusababisha kushuka kwa kiwango cha elimu.

   Mzee alisema serikali itaendelea kuisimamia sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na kuwashawishi wadau wa elimu kuweza kuachangia masuala mbalimbali katika elimu ili elimu iweze kuthaminiwa na kuwa katika matokeo mazuri.

 Kwa upande wake afisa ukaguzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Masasi aliomba halmashauri kutenga fedha na kuzitoa kwa idara ya ukaguziili iweze kufanya shughuli za ukaguzi kwa ufanisi zaidi ukilinganisha na hivisasa ambapo kitengo hicho kinafanya kazi katika mazingira magumu.

   Kwa pamoja wakurugenzi wa halmashauri hizo mbili, halmashauri ya wilaya na ya mji , Bi. Changwa Mkwanzu na Bi. Gimbana Ntavyo walisema wao kama wakurugenzi wamezipokea changamoto na ushauri uliotolewa na wadau hao hivyo kama wao ni wasimamizi wa halmashauri hizo wanaahidi kuzifanyia kazi kwa nguvu moja ili kurudisha hali ya kitaaluma wilayani humo ambayo kwa sasa imeshuka kwa kasi.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa