• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

JUMUIYA YA VIJANA WA CHAMA CHA MAPINDUZI WILAYA YA MASASI WAMPONGEZA RAIS JOHN POMBE MAGUFULI

Posted on: June 22nd, 2017

Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Masasi wamefanya maandamano ya kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli kwa jitihada zake za kusimamia rasilimali za taifa  ikiwemo suala la  kuzua usafirishaji wa mchanga wa madini maarufu kama Makinikia leo  tarehe 22.06.2017 katika viwanja vya ofisi za Mkuu wa wilaya ya masasi.

Akisoma risala ya Umoja wa Vijana CCM Wilaya ya Masasi, mwenyekiti wa vijana wa  chama hicho ndugu Ahmed Matipula alisema kuwa Vijana wa CCM wanapata faraja kubwa kwa kazi mbalimbali zinazofanywa na  mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dr. John Pombe Magufuli kwamba Chama cha Mapinduzi kinaendelea kupata heshima kubwa kitaifa na kimataifa kwa kutekeleza kwa vitendo ahadi zake alizotoa wakati wa kampeni za kuomba ridhaa ya kuongoza nchi.

Matipula alisema kuwa maandamano hayo ni matokeo ya kazi kubwa anayofanya Rais katika kuwaletea maendeleo watanzania na kumfanya kila mtanzania aishi kwa haki na usawa kwani katika kipindi kifupi cha utawala wake mengi yamefanyika mambo mengi ambayo yanawafanya Jumuiya ya Vijana CCM kutembee kifua mbele hususan pale alipodhibiti matumizi yasiyo ya lazima na nidhamu ya matumizi katika fedha za umma.

Rais ameonyesha ujasiri na uzalendo wa hali ya juu katika dhamira yake ya kudhibiti raslimali za taifa ambazo zilikuwa zinaporwa kiholela hasa madini, alizuia usafirishaji wa makontena yenye mchanga wenye madini (Makinikia) na kuunda tume mbalimbali mfululizo kuchunguza uhalisia wa madini yaliyo kwenye mchanga huo lengo ikiwa ni kujiridhisha kiasi cha madini ambacho kimekuwa kikipotea kwa miaka mingi, alisema Matipula.

Kutokana na jitihada hizo za Mhe. Rais, anapaswa kupongezwa kuliko kubezwa, anahitaji kuungwa mkono na kila mtanzania mzalendo na mpenda maendeleo kwani kiasi kilichopatikana kwenye madini pekeyake kinaweza kuiwezesha bajeti ya mwaka mzima bila kutegemea wahisani.

“Fedha hizo zitasaidia kupunguza vifo vya akinamama na watoto kwa kuwa na huduma bora za afya ya uzazi, zitanunua madawa na pembejeo za kilimo, zitalipa ada za wanafunzi, zitajenga shule, zahanati na vituo vya afya na hospitali. Kwa ujumla fedha hizo zitainua kipato cha Mtanzania na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda na uchumi wa kati”. Matipula alisema.

 

Bwana Matipula alisema kuwa Jumuiya ya Umoja wa Vijana Wilaya ya Masasi inaunga mkono juhudi za Rais na Serikali yake kwa kuitendea haki Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi kwa kiwango kikubwa na kwa vitendo. Aidha anawaomba watendaji wote wa serikali na wadau wengine wa maendeleo kumuunga mkono Rais kila mmoja na eneo lake la kiutendaji.

Matipila anamuomba Rais awapuuze wale wote wenye nia ya kumrudisha nyuma katika jitihada zake za kuwatumikia watanzania na ikibidi kuwashughulikia wale wote watakaobainika wanakula njama wa wawekezaji kwa nia ya kuhujumu juhudi zake za kulinda raslimali za taifa kwa niaba ya watanzania wote.

Aidha jumuiya hiyo imeomba Rais awashughulikie wale wote waliohusika kwa namna moja ama nyingine kuiingiza nchi yetu kwenye mikataba ya kinyonyaji ambayo inaipa hasara Tanzania kama ambavyo tumeona wale ambao walihusishwa na sakata la ESCROW walichukuliwa hatua.

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • WAENDESHA VIFAA VYA BAYOMETRIKI NA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI WAPATIWA MAFUNZO ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA AWAMU YA PILI.

    May 15, 2025
  • WATAALAMU MASASI DC WAPATIWA MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO WA UJIBUJI HOJA ZA CAG.

    May 11, 2025
  • KAMATI YA FEDHA, UONGOZI NA MIPANGO YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ROBO YA III (JAN -MACHI 2025) INAYOTEKELEZWA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI.

    May 06, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa