• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI YATOA MKOPO WA MIL. 115,645,000 KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE NA VIJANA

Posted on: November 16th, 2017

Katika kutekeleza kauli mbiu ya Serikali ya kufikia uchumi wa kati kwa kuanzisha viwanda kila mkoa na halamshauri , Halmashauri ya Wilaya ya Masasi mkoani mtwara imeanza kutekeleza kwa vitendo Agizo  hilo kwa kuwezesha vikundi 42 vya wananwake na vijana vinavyojishughulisha na shughuli za ujasiliamali kwa kutoa mikopo ya riba nafuu katika robo  ya kwanza ya  mwaka wa fedha 2017/2018.

Akizungumza kabla ya kukabidhiwa hundi  za mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 115,545,000/=  kwa vikundi hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Changwa M. Mkwazu  alisema kuwa  ni vema kila kikundi kikafahamu kuwa  kina nafasi kubwa ya kuanzisha viwanda vidogoviogo kwani mtaji wa kuanzia wamepata ili waweze kufikia uchumi wa kati kwa kuzalisha bidhaa mbalimbali zenye ushindani katika soko.

Mkwazu alisema kuwa utoaji wa mikopo hiyo kwa  vikundi vya wananwake na vijana ni utekelezaji wa agizo za serikali la kutenga asilimia kumi (10%) ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi kama njia ya kuimarisha uchumi wa wananchi kupitia shughuli za ujasiliamali.

“Halmashauri imekuwa ikitoa mikopo hii kila mwaka japo kuwa changamoto kubwa ni urejeshwaji wa fedha hizo kwa wakati  inayopelekea kutofikia lengo la kuiwezesha jamii kiuchumi kutofikiwa kwa kiwango kikubwa, kwani mikopo inayotolewa inakuwa midogo tofauti na malengo kusudiwa, hivyo niwaase wananvikundi mnaopata mkopo leo mhakikishe mnarejesha kwa wakat ili na wengine waweze kukopeshwa” alisema Mkwazu.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira Diwani wa kata ya Lukuledi Mhe Victor Antapa  waliwatahatharisha wanavikundi kuwa mikopo hiyo imetolewa kisheria na watapaswa kurejesha kwa wakati ili kutoa fursa kwa vikundi vingine kupata mikopo yenye thamani kubwa zaidi na hivyo kuweza kufanya uzalishaji kwa kiwango kikubwa zaidi.

Mhe. Antapa aliwaeleza wanavikundi kuwa kama watafanya shughuli zao kwa uaminifu wanauwezo wa kuanzisha SACCOS ili waweze kutuza fedha zao na hivyo kuongeza mitaji na uzalishaji hatimaye kukuza uchumi wa wanakikundi, jamii  na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Hamashauri hiyo Sity Mtalemwa alisema kuwa  jumla ya vikundi vya VICOBA endelevu 15  vimefanikiwa kuunganishwa na taasisi za fedha ikiwemo benki ya  posta na Mfuko wa wananchi(MEF)  na vimekopeshwa jumla ya shilingi  Milioni 152,000,000 na idara imeendelea kutoa mafunzo ya ujasilia mali wa VICOBA  na vikundi ili kupata uelewa wa mambo mbalimbali ya ujasiliamali.

Mtalemwa alisema  vikundi vya wananwake na vijana katika  halmashauri ya wilaya ya masasi vimeendelea kufanya vizuri katika masuala ya ujasilia mali ampapo kikundi cha LEMACHI kilichopo ijiji cha Nambawala kimefanikiwa kuwa mshindi wa kwanza katika maonesho ya Ujasiliamali (SIDO) kanda ya kusini ambapo mikoa ya Dar es salaam, morogoro,pwani,lindi na mtwara ilishiriki.

 Kwa mwaka 2015/2016 jumla ya shilingi milioni 160,770,000 zilikopeshwa kwa vikundi 95 na kurejeshwa jumla ya shilingi 155,432,150 sawa na asilimia 96% na  mwaka 2016/2017 jumla ya shilingi milioni 380,050,000 zilikopeshwa kwa vikundi 102 na zikarejeshwa shilingi 69,379,500 sawa na asilimia 26% .

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa