• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC MASASI AKABIDHI PIKIPIKI 34 KWA WARATIBU ELIMU KATA, HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI

Posted on: July 13th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara Mhe. Selemani Mzee amewataka  waratibu elimu kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi kufanya kazi ya  ufuatiliaji na usimamizi wa taaluma na miundombinu ya shule katika maeneo yao, ili kuboresha elimu ikiwemo kuongeza ufaulu wa wanafunzi  katika shule za Msingi na Sekondari kutokana na kuwa na usafiri wa uhakika.

Mkuu wa Wilaya ya Masasi mhe Selemani Mzee akijiandaa kuendesha pikipiki  kabla ya kukabidhi kwa waratibu elimu kata

Mkuu wa wilaya ametoa kauli hiyo wakati wa hafla fupi ya kukabidhi pikipiki 34 kwa waratibu elimu kata wa Halmashauri hiyo lengo ikiwa ni kuwawezesha  waratibu hao kuwa na  usafiri wa uhakika  kwa ajili ya kutekeleza majukumu yao ya kufuatilia na kusimamia masuala ya elimu ili  kuboresha sekta ya elimu katika shule zote  zilizopo katika kata 34 maana hakuna kisingizo cha kushindwa kuzifikia. 

“Kuanzia sasa ubora wa elimu utaongezeka kwani Waratibu elimu kata mtakuwa na uwezo wa kupita katika shule zote kuangalia mahudhurio, ufundishaji na utekelezaji wa miradi inayotekelezwa katika shule hizo za msingi na sekondari kwa fedha za Serikali au nguvu za wananchi” alieleza Selemani 

Mkuu wa Wilaya ya Masasi mhe Selemani Mzee akiendesha pikipiki  kabla ya kukabidhi kwa waratibu elimu kata

Aidha Mkuu wa Wilaya amewakumbusha Waratibu elimu kata kuwa pikipiki walizokabidhiwa ni kwa ajili ya  kuongeza kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi na masuala mengine ya elimu, hivyo  pikipiki hizo zikafanye kazi iliyokusudiwa ya kusimamia  elimu na sio  kutumia kwenye shughuli zenye maslahi yao binasfi ikiwemo kwenda nazo mashambani.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi mhe. Juma Satmah ameiishukuru Serikali kwa kutoa pikipiki kwa waratibu elimu kata 34 kwani zitasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza usimamizi wa utoaji wa elimu katika shule za Msingi na Sekondari na hatimaye ufaulu kuongezeka kwani kutakuwa na ufuatiliaji wa mara kwa mara tofauti na hapo awali ambapo waratibu hawakuwa na usafiri wa uhakika kuzifikia shule katika maeneo yao.

Mratibu elimu kata  wa kata ya Mbuyuni  Halmashauri ya Wilaya ya Masasi akiendesha pikipiki  Baada  ya kukabidhiwa leo  tarehe 13.07.2018 katika hafla ya kukabidhi pikipiki hizo kwa waratibu elimu kata 34  nje ya Ofisi za Halmashauri.

Satmah amewakumbusha waratibu kuzituma vizuri pikipiki hizo kwani hivyo ni vyombo vya moyo hivyo lazima wazingatie taratibu za kuviendesha vyombo hivyo ikiwemo kuwa na leseni.

Akisomba taarifa ya mapokezi ya pikipiki  hizo 34 za waratibu elimu kata zilizotolewa na serikali kuu  Afisa elimu  Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi  Elizabeth Mlaponi  alieleza kuwa changamoto kubwa inayosababisha kukosekana kwa utekelezaji wa mkakati wa ufuatiliaji na usimamizi wa taaluma na miundombinu shuleni in pamoja na ukosefu wa usafiri, hivyo pikipiki hizo zitarahisisha  shughuli za ufuatiliaji na usimamizi wa shughuli za maendeleo ya elimu kwani  wataweza kutebelea shule wakati wote na hivyo kuhakikisha ufundishaji na ujifunzaji unafanyika kadri ya mipango ambayo ndio njia mojawapo ya kuongeza ufaulu.

Afisa Elimu Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Elizabeth Mlaponi Akisoma taarifa ya mapokezi ya pikipiki   34 za waratibu elimu kata 

Akiongea kwa niaba ya waratibu wengine baada ya kukabidhiwa pikipiki hizo Lulu Millanzi alisema kuwa pikipiki hizo zitawasaidia sana kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi tofauti na hapo awali ambapo mazingira ya utendaji kazi yalikuwa magumu sana hali ambayo hata utekelezaji haukuwa wenye ufanisi mkubwa.


“Tunaishukuru Serikali kwa kutukumbuka na tunaahidi kufanya kazi kwa bidii kwa kuhakikisha tunafanya ufuatiliaji wa mara kwa mara shuleni lengo ikiwa ni  kusimamia masuala ya elimu  na hatimaye kuongeza ufaulu kwa wanafunzi  katika shule zetu za msingi na sekondari” alisema lulu. 

Pikipiki hizo walizopatiwa waratibu hao ni miongoni mwa pikipiki zilizotolewa na serikali kwa waratibu elimu wa Kata wote hapa nchini zenye lengo la kuboresha mazingira ya kufanyia kazi kwa waratibu hao.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa