• Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Masasi District Council
Masasi District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Asili ya Masasi
      • Historia ya Masasi Kiutawala
      • Orodha ya Viongozi
      • Ukubwa wa eneo
      • Hali ya hewa
      • Shughuli za Kiuchumi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Usafi wa Mazingira
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ugavi na Ununuzi
      • Sheria na Usalama
      • Nyuki
      • Tehama na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Agriculture
    • Construction Minerals
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Upimaji wa Ardhi
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha Utawala na Mipango
      • Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kudhibiti UKIMWI
      • Maadili
      • Elimu Afya na Maji
    • Ratiba
      • Vikao vya Kisheria vya Halmashauri
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi iliyopangwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Sheria
    • Fomu za maombi
    • Jarida
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

BILIONI 1.3 ZANUFAISHA WALENGWA 10559 WA KAYA MASIKINI, HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI

Posted on: July 11th, 2018

Walengwa wa Mpango wa kunusuru kaya maskini unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi wamenufaika na mradi huo baada ya kushiriki utekelezaji wa miradi ya ajira za muda (PWP) na kisha kulipwa ujira katika miradi iliyoibuliwa na kutekelezwa kwenye maeneo yao yenye thamani ya shilingi bilioni 1,346,672,000.

Wananchi wa kijiji cha chiwata wakichota maji katika kisima kilichochimbwa kupitia Mradi TASAF

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa miradi hiyo katika vijiji  97 vinavyotekeleza miradi ya ajira ya muda , Mratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika Halmashauri hiyo Thobias Mkude alisema kuwa katika utekelezaji wa miradi hiyo, jumla ya shilingi milioni 934,082,900 zilitumika kulipa ujira kwa walengwa walioshiriki kufanya kazi huku milioni 412,589,100 zikitumika kununua vifaa na kugharamia mafunzo na posho za wasimamizi wa miradi hiyo.

Mkude alifafanua kuwa, miradi iliyotekelezwa ni pamoja na miradi ya maji iliyohusisha uchimbaji wa visima 30, mabwawa 4, kusambaza maji ya bomba 1 na miradi ya upandaji wa miti 62 ambapo walengwa walifanya kazi katika miradi hiyo kwa muda wa siku 60 na kulipwa ujira wa shilingi 2300 kwa siku lengo ikiwa ni kuziongezea kipato kaya hizo masikini.

Mradi wa upandaji miti uliotekelezwa kupitia mradi wa TASAF kijiji cha Namajani 

Mkude ameeleza kuwa jumla ya kaya 10,559 zinanufaika na mpango huo wa kunusuru kaya masikini kupitia mradi wa Ajira ya muda (PWP), aidha kaya hizo pamoja na kupata ujira huo lakini pia zinaendelea kupata ruzuku ya kila mwezi lengo likiwa ni kuwawezesha kupata mahitaji ya msingi ikiwemo chakula, kuboresha makazi, kupata huduma za afya na elimu pamoja na kupata mtaji wa kufanya biashara.

Bibi Amina rashidi Musa ambaye ni mmoja wa walengwa wanaonufaika na mpango katika kijiji cha Namajani katika Halmashauri ya Wilaya ya Masasi alisema, anaishukuru serikali kwa kuleta mpango wa TASAF kusaidia kaya masikini kwa kuwapa ujira baada ya kufanya kazi kwenye miradi ya ajira ya muda ambayo kwa sasa inafaidisha jamii nzima na si walengwa pekee

 Amina alieleza kuwa, kwa sasa walengwa wengi wameboresha maisha yao kwani wanauhakika wa kupata chakula, kujenga makazi bora , kupata pembejeo za kilimo, kuwa na mtaji wa kufanya biashara pamoja na kukuza uchumi wetu kupitia vikundi vyao vya kuweka akiba jambo ambalo kabla ya mradi hawakuwa na uwezo huo

Bi Neema Luka Ismail akiwa Mlengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini katika kijiji cha Namajani akiwa amesimama katika nyumba yake aliyojenga kuitia mradi wa TASAF

 “Kupitia maradi huu ninakula vizuri ninalala vizuri lakini pia nimeweza kununua bati 20  na kufyatulisha tofali, lakini pia nimeweza kununua dawa za kupulizia mikorosho yangu ili kuongeza uzalishaji ,  hivyo naishukuru sana serikali kwa mpango huu maana unanisaidia sana” alibainisha Amina

Bibi amina aliongeza kuwa kutokana na fedha anazopata ameweza kujiunga na bima ya afya jamii (CHF) inayomwezesha kupata huduma za afya kwa mwaka mzima yeye na familia yake pamoja na kumununulia mahitaji ya shule mjukuu wake.

Kwa upande wake Fidelis Wiliamu Mmavele mlengwa wa mpango katika kijiji cha Namnajani, alikiri kuwa utekelezaji wa mradi wa kupanda miti katika kijiji chao pamoja na kuwezeha walengwa kuongeza kipato lakini mradi huu umesaidia jamii kupata ujuzi wa namna ya kupanda miti na umuhimu wake baada ya miti hiyo kukua vizuri na kufanya mazingira kuwa mazuri.

Wananchi wa kijiji cha chidya wakichota maji katika kisima kilichochimbwa kupitia Mradi TASAF

“Miti hii inafanya mazingira kuwa mazuri lakini pia shamba hili la miti litaongeza chachu kwa wananchi kupanda miti katika maeneo yao kwa matumizi mbalimbali katika jamii kibiashara na kijamii ikiwemo utengenezaji wa madawati na ujenzi wa miradi ”

Baada ya kukamilika kwa Mirad yote ya ajira ya Muda iliyotekelezwa katika vijiji 97 jukumu la usimamizi wa miradi hiyo unafanya na serikali za vijiji na sio walengwa kwani miradi hiyo kwa sasa ni mali ya kijiji.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA MASASI DC 2025 January 14, 2025
  • MGAWANYO WA MAENEO YA UTAWALA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TAREHE 27 NOVEMBA, 2024 MASASI DC September 18, 2024
  • MAENEO YA UTAWALA KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI September 18, 2024
  • FURSA YA MIKOPO INAYOTOLEWA NA MFUKO WA MIKOPO KUTOKA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO KWA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MASASI November 12, 2021
  • Angalia Zaidi

Habari Mpya

  • MSIGWA: MAAFISA HABARI NI SAUTI YA SERIKALI, TANGAZENI MAFANIKIO YA SERIKALI KWENYE MAENEO YENU.

    May 25, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI MNAKUWA WABUNIFU NA WAZALENDO ILI WANANCHI WAPATE HABARI SAHIHI NA KWA WAKATI.

    May 23, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MASASI DC KWA KISHINDO:WATEMBELEA MIRADI MITANO YENYE THAMANI YA TSH.MILIONI 678,844,040.00

    May 19, 2025
  • WATENDAJI WA SERIKALI TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KIKAZI,MSIJIHUSISHE NA MAMBO YA SIASA: BARAZA LA MADIWANI

    May 15, 2025
  • Angalia Zaidi

Video

KAIMU MKURUGENZI MASUMBUKO MTESIGWA AKABIZI OFISI KWA MKURUGENZI MPYA
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • RASIMU YA MPANGO WA BAJETI KWA MWAKA WA FWDHA 2021/2022 MASASI DC
  • Mpango Mkakati wa halmashauri ya wilaya ya masasi 2016/2017-2020/2021
  • Taarifa ya Hesabu ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2015/16
  • Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 Masasi DC
  • Uchunguzi wa Madai ya Korosho kwa Misimu ya 2016/17 NA 2017/18 Wilaya ya Masasi
  • Mpango Kzazi wa Manunuzi kwa mwaka wa Fedha 2017-2018 Masasi DC
  • Mwongozo wa Malalamiko
  • Sheria

Kurasa Mashuhuri

  • Ikulu
  • Mtwara Region
  • Hati ya Malipo (Salary Slip)
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya Ajira
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana nasi

    Masasi - Bomani

    Anuani ya Posta: S.L.P 60 Masasi

    Simu ya mezani: 023-2510031

    Simu ya kiganjani: 023-2510031

    Baruapepe za Watumishi: ded@masasidc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki @2017 Halmashauri ya Wilaya ya Masasi. Haki Zote Zimehifadhiwa